Ikumbukwe Simba SC imetolewa hatua ya robo fainali Club Championship

Hapa ndipo tunapokosea. Simba amecheza klabu bingwa afrika na hakucheza na Azam, Lipuli, mbao wala Yanga. Kipimo chake ni Klabu bingwa Afrika. Hesabu za Simba zimekuwa za hovyo sana hasa alipotegemea uwanja wa nyumbani tu. Ni hiviiii, ingekuwa ni mashindano ya mtoano kuanzia game one basi ni dhahiri simba angemtoa AS Saoura tu maana mechi dhidi ya wapinzani wake wengine kachapika sawasawa. Hii timu ibadilishe falsafa na iachane mtazamo wa kinyumbani. Pole sana wana Msimbazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pia ikumbukwe simba imechezea vichapo vikubwa sana ugenini! Jumla ya mabao ktk mechi za ugenini kuanzia hatua ya makundi ni 16 ( 5 + 5 + 2 +4)! Wastani wa goli 4 ktk kila mechi ! Duu ni karekodi pia

Sent using Jamii Forums mobile app
Ambao hamjawahi chezea hivyo vichapo mliishia wapi..na nyinyi mlifika robo fainali??
 
CAF imetuhujumu kwa kubadili marefa, matokeo yatafutwa ushindi utakuja msimbazi..... tuendelee kujitekenya.

Usile Mbegu.
 
 
BILA SHAKA SIMBA WAMELIELEWA SOMO..

Anaandika Xavi Hernàndez Alcantara

Kabla sijaanza kuandika hichi ambacho nimekusudia najiuliza unaanzaje kuwalaumu Simba? Hasa katika hatua hii ambayo wamefikia na kuishia unapata wapi ujasiri wa kuwazomea au kuna lingine tofauti na hili? Binafsi hakuna nacho wadai Simba kwa hatua hii ambayo wamefikia na kumaliza nayo Robo Fainali si jambo dogo tena si robo fainali ya FA ni Robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika wachache sana wanaweza kunielewa nachoandika..

Nafikiri Simba kuna somo ambalo wamepatiwa baada ya leo kukamilisha hatua hii ya Klabu Bingwa Afrika kwa kutolewa na TP Mazembe ya nchini Congo kabla ya kuwazomea tusisahau kuwapongeza hatua kama hizi tumezoea kuwaona Al Ahly,TP Mazembe,Raja Casablanca lakini msimu huu tumewaona Simba katika hatua kama hii..

Bila shaka kuna somo Simba wamelipata kwa ajili ya msimu ujao kama watamaliza wakiwa mabingwa ndani ya TPL msimu ujao watarudi wakiwa wanajua ni nini cha kufanya watakuwa wanafahamu tabu ambazo wamezipitia hili ni somo tosha kwa Simba ambalo wamelipokea sita shangaa msimu ujao wakifanya vizuri tena kama msimu huu..

Anazungumza kocha Patrick Aussems baada ya kupokea timu kutoka kwenye mikono ya Mfaransa Pierre Lechantre anasema nina malengo mawili kwa klabu hii kwanza ni kuhakikisha timu inafika katika hatua ya makundi ya klabu bingwa na pili, ni kuhakikisha timu inatetea ubingwa wa ligi kuu hapa nchini ulimuelewa Patrick Aussems?

Simba ikaifunga Mbabane Swallows na kuwatoa katika hatua ya awali kuyatafuta makundi ya klabu bingwa na baadae Simba ikawafunga Nkana Red Devil's katika hatua ya mwisho kuelekea makundi ya klabu bingwa na Simba ilifuzu hatua hiyo ya Klabu bingwa Afrika unayakumbuka maneno ya Patrick Aussems? Lengo la kwanza la kocha lilikuwa limetimia

Ghafla Simba wanafuzu katika hatua ya Robo Fainali Patrick Aussems akiwa kama kocha anavuka malengo ambayo alijiwekea na lengo la pili ni kuhakikisha anatetea ubingwa wa ligi kuu hapa nchini hili pia bado lipo ndani ya uwezo wake Aussems huu si muda wa Simba kulaumiana kuanzia ndani ya klabu hadi nje ni muda wa Simba kulielewa somo..

Nimeutazama vyema mchezo wa Robo fainali ya pili uliopigwa kule Lubumbashi nimewataza Simba wakipambana mpaka pale pumzi ilivyokata na neno nusu fainali kwao likiwa linapotea tarabitu kupitia miguu ya Jackson Muleka mshambuliaji wa TP Mazembe tatizo linaweza kuwa ni lile lile tu na si vinginevyo..

Katika mechi za Makundi ambazo Simba alicheza hakuwai kucheza vyema ugenini alijitaidi kucheza vyema zaidi nyumbani kuliko ugenini hilo jambo zuri lakini hawakufanya hivyo katika mechi ya robo fainali dhidi ya TP Mazembe bahati mbaya Simba wanapoteza makali yote wakicheza ugenini somo linaanzia hapa kwa upande wa kikosi cha Simba.

Katika Dimba la As Vita hadi kufika mapumziko kila mtu alifahamu uhatari aliokuwa nao Jean-Marc Makusu Mundele alinyanyasa safu ya ulinzi jinsi atakavyo tukamuona Fabrice Ngoma akifanya majukumu kama ya Mesut Ozil nae tuliona ubora wake hata Nelson Munganga alitufunza namna ya kiungo mkabaji anavyotakiwa kuwa na goli 5 zilifungwa..

Simba walivyokwenda Alexandria Kule nchini Misri wakati wa mapumziko baadhi yao walizima TV ulikuwa unyanyasaji mkubwa miguu ya El Shehat ilikuwa kwenye ubora wa juu shahidi Assist 3 ilizopiga Simba walishindwa namna ya kucheza ugenini hivyo hivyo goli mbili kwa Js Saoura kule nchini Algeria Lakini timu zote katika hatua ya makundi zilifungwa na Simba Dar.

Hili ni somo tosha ambalo Simba wamejifunza na watakapo-Rudi msimu ujao watajua kwa kuanzia Somo hili hili leo limewanyima Simba kwenda katika hatua ya nusu fainali tatizo ni lile lile tu namna ya kucheza katika ardhi ya ugenini kama siku za nyuma dhidi ya Al Ahly,As Vita,Js Saoura na leo hii TP Mazembe bila shaka wataanzia hapa..

Leo dhidi dhidi ya TP Mazembe Simba walicheza kwa kupambana lakini Team Work ya TP Mazembe imeamua huku ikichangiwa na uwezo wa mchezaji mmoja mmoja licha ya Simba kuwa wa kwanza kupata goli kupitia kwa Emanuely Okwi..

TP Mazembe ni wazuri sana kwenye Flanks(pembeni) kuliko maeneo mengine na ndio sehemu ambayo mashambulizi yao mengi yamekuwa yakipitia na kuweza kupata magoli rejea katika mashambulizi yao ambayo walikuwa wanayafanya leo Wakitoka na shoot on targert 16 na Corner 9 jinsi gani walikuwa wanafanya mashambulizi sana sana

Walimtumia zaidi Meschak Elia pamoja na Rainford Kalaba alafu Jackson Muleka akiwa kama Mshambuliaji lakini anaetembea pande zote alafu Tresor Mputu akicheza kama Playmaker chini akisaidiwa na Nathan Sinkala pamoja na Mika Miche katika kiungo mkabaji ndani ya kikosi cha TP Mazembe..

Haikuwa rahisi kwa Zana Coulibaly Mbele ya Elia winga mwenye kasi sana na Control ya hali ya juu mechi ya kwanza hapa Dar alitokea Benchi na alisumbua sana ngome ya Simba leo alikuwa katika kiwango cha juu mno yeye pamoja na Jackson Muleka ambaye alipoteza pia nafasi za wazi pia ubora wa Aishi Manula ni wakuuheshimu sana..

Goli la kusawazisha la TP Mazembe ni Poor Marking ya Simba iliyofanywa ni goli rahisi sana Simba imepoteza mchezo kwa makosa yale yale ni namna ya kucheza ugenini Simba hawafanyi vizuri bahati mbaya walikuwa hawana mtaji wa goli hata moja hili pia lilichangia kwa kiasi kikubwa ni muda wa Simba kulielewa Somo walilopatiwa..

Ngoja niishie hapa..

SPANISH PASS MASTER

WAPO WANANIELEWA MPAKA HAWAJIELEWI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…