Alwatan kamba
Member
- Nov 16, 2020
- 70
- 236
Katika kuboresha sekta ya elimu nchini, ni wakati sahihi wa serikali kupitia wizara ya elimu na tamisemi kuachana na mpango wa kutoa mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti almaarufu 'grade A'
Sababu ni hizi,
1. Mafunzo ya ualimu wa 'grade A' hayawaandai walimu hao kuendana na soko la dunia kwenye ajira. Sababu ni kwamba mafunzo wanayopata hayawawezeshi kufanya kazi popote katika dunia ya leo kwani mataifa mengi kwa sasa yameachana na mpango wa kuzalisha walimu wa ngazi ya cheti na hivyo elimu hiyo haitambuliki kidunia.
2. Ualimu ngazi ya cheti 'grade A' unazingatia zaidi mahitaji ya nchi lakini hauzingatii matakwa ya dunia kwani walimu wanaozalishwa kupitia mafunzo hayo huishia tu kufundisha watoto ndani ya nchi na sio vinginevyo.
3. Walimu wengi wa 'grade A' hawakufanya vizuri katika mitihani yao ya kidato cha nne hivyo wanatakiwa kuboreshwa angalau kwa kiwango cha elimu ya stashahada ili kuwaongezea umahiri zaidi kitaaluma na kuendana na matakwa ya kidunia.
4. Ualimu ngazi ya cheti 'grade A' pia unachangia kufeli kwa wanafunzi. Kutokana na uwepo wa mafunzo haya ya 'grade A' wanafunzi wengi huzembea katika masomo kwa kujua hata wakifanya vibaya kwa kupata ufaulu hafifu wa daraja la nne 'division four' wataenda kusomea ualimu huo.
5. Mafunzo ya 'grade A' pia yanachangia kudharaulika kwa kada ya ualimu na kuonekana kama kada kimbilio la watu waliofeli kwani walimu wengi wanaodahiliwa na kuajiriwa kupitia mafunzo ya ngazi ya cheti huwa na ufaulu wa kawaida sana katika matokeo yao ya kidato cha nne.
Kufuatia sababu hizo na nyingine ambazo si vizuri kuzitaja ni vema sasa mafunzo ya 'grade A' yakafutwa rasmi na wizara ya elimu ikaendelea na mchakato wa kuboresha elimu kwa kuboresha walimu wa 'grade A' walioko kazini angalau wawe na kiwango cha elimu ya stashahada kama ilivyoainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi 2020-2025.
Kauli mbiu ya sera ya elimu na mafunzo inasema,
" Elimu bora na yenye tija kwa maendeleo ya Taifa inawezekana, wote tutekeleze wajibu wetu"
Sababu ni hizi,
1. Mafunzo ya ualimu wa 'grade A' hayawaandai walimu hao kuendana na soko la dunia kwenye ajira. Sababu ni kwamba mafunzo wanayopata hayawawezeshi kufanya kazi popote katika dunia ya leo kwani mataifa mengi kwa sasa yameachana na mpango wa kuzalisha walimu wa ngazi ya cheti na hivyo elimu hiyo haitambuliki kidunia.
2. Ualimu ngazi ya cheti 'grade A' unazingatia zaidi mahitaji ya nchi lakini hauzingatii matakwa ya dunia kwani walimu wanaozalishwa kupitia mafunzo hayo huishia tu kufundisha watoto ndani ya nchi na sio vinginevyo.
3. Walimu wengi wa 'grade A' hawakufanya vizuri katika mitihani yao ya kidato cha nne hivyo wanatakiwa kuboreshwa angalau kwa kiwango cha elimu ya stashahada ili kuwaongezea umahiri zaidi kitaaluma na kuendana na matakwa ya kidunia.
4. Ualimu ngazi ya cheti 'grade A' pia unachangia kufeli kwa wanafunzi. Kutokana na uwepo wa mafunzo haya ya 'grade A' wanafunzi wengi huzembea katika masomo kwa kujua hata wakifanya vibaya kwa kupata ufaulu hafifu wa daraja la nne 'division four' wataenda kusomea ualimu huo.
5. Mafunzo ya 'grade A' pia yanachangia kudharaulika kwa kada ya ualimu na kuonekana kama kada kimbilio la watu waliofeli kwani walimu wengi wanaodahiliwa na kuajiriwa kupitia mafunzo ya ngazi ya cheti huwa na ufaulu wa kawaida sana katika matokeo yao ya kidato cha nne.
Kufuatia sababu hizo na nyingine ambazo si vizuri kuzitaja ni vema sasa mafunzo ya 'grade A' yakafutwa rasmi na wizara ya elimu ikaendelea na mchakato wa kuboresha elimu kwa kuboresha walimu wa 'grade A' walioko kazini angalau wawe na kiwango cha elimu ya stashahada kama ilivyoainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi 2020-2025.
Kauli mbiu ya sera ya elimu na mafunzo inasema,
" Elimu bora na yenye tija kwa maendeleo ya Taifa inawezekana, wote tutekeleze wajibu wetu"