Ili kuinua kiwango cha soka Tanzania, Simba na Yanga zifutwe

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,553
Si tu kuwa kutapatikana mwelekeo wa wapi tunaenda katika football world, bali pia kutafungua vichwa na kuleta kujitambua kwa mamilioni ya Watanzania ambao mawazo yao na upeo wao katika uelewa wa mpira wa miguu duniani ni Simba na Yanga.

Hivi vilabu vikiendelewa kuachiwa na serikali vitazidi kuharibu vizazi na vizazi. Miaka nenda rudi watu watakua wakibishana, kurushiana vijembe, kula pesa kwa kujificha kwenye kivuli cha uongozi, lakini maendeleo yeyote kimataifa hakuna.

Leo hii vilabu vichanga mfano Namungo, Gwambina vinatikisa timu hizi mbili kongwe zilizoanzishwa toka 1930's. Miaka yote hiyo ukiangalia havijafanya makubwa kwa miongo mingi lakini pia hata viwanja hazina. Kazi ni migogoro, kufukuza walimu na ubadhirifu.

Serikali iamke. Hivi vilabu ni sumu kwa wachezaji wachipukiao hapa nchini,ni sumu kwa vilabu vingine vichanga, ni sumu kwa maendeleo ya mpira wa miguu, zifutwe na tubaki na timu zingine kuliko kuendelea na timu ambazo zimekua kama dini bila vision, mbaya zaidi zinawaathiri Watanzania wengi kiakili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usawa haupo duniani mwanangu. Ujerumani kuna Bayern na Dortmund. Uhispania kuna Barca na Madrid; Ufaransa kuna PSG, Uingereza kuna mwanitesa UNTD na Liver. Sisi Simba na Yanga unaumia? Kila ligi lazima iwe na giants mwanangu.
 
Kojoa ukalale hujui kitu.usawa haupo duniani mwanangu.ujerumani kuna bayani na dotimundi,uhispani kuna basa na madrid,ufaransa kuna psg,uingereza kuna mwanitesa utd na liva sisi simba na yanga unaumia?kila ligi lazima iwe na giants mwanangu.
Hebu mwelekeze nduguyo maana kapiga bonge moja la Pumba an chaaa!
 
Mimi hua na wishi hivi vilabu one day vigawanyike zitokee team mbili kila team ili at least tuwe na club 4 zenye uwiano sawa ya mashabiki itakua fair sana kwa sasa Simba na Yanga ni moja ya tatzo la ukuwaji wa soka la Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hapo unakosea.kwa nini tusizifanye simba na Yanga zote zikawa imara?Kila nchi ina timu 2 kubwa zinazofanya vizuri zikizidi 3
Spain-2madrid barca
Misri-2 al alhy zamalek
Congo-mazembe vita
Moroco-raja waydad casablanca
South africa 3-orlando,kaizer na mamelod
Kuna nchi zina timu 1 tu na bado zinafanya vizuri kisoka.kuna nchi zina timu 5 zenye usawa kifedha na kiuweZo bado hazikojuu.
Cha kufanya ni kuzifumbua macho hizi timu ndogo namna ya kuwashawishi wapate wawekezaji hata wadogo 30.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina wasiwasi na kinywaji unachotumia, hivi Rwanda, Burundi, Malawi na msumbiji ili wapande viwango wanatakiwa waondoe team gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simba na yanga ni vilabu vya kariakoo utakuta mtu yupo mbeya na mbeya inacheza na timu moja kati ya izo mbili cha ajabu anashangilia simba au yanga,ili ndio tatizo kubwa suruhisho ni kila mtu apende timu kulingana na anakotoka ndio kukua kwa soccer la kiushindani
 
Nani wa kufuta huyu ambae ashabikii simba wala yanga,hata bungeni kuna wabunge wa simba na yanga na huwa wanacheza mechi zao wa simba na yanga,
Na bado yanga wanakalishwa kila mechi,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usawa haupo duniani mwanangu. Ujerumani kuna Bayern na Dortmund. Uhispania kuna Barca na Madrid; Ufaransa kuna PSG, Uingereza kuna mwanitesa UNTD na Liver. Sisi Simba na Yanga unaumia? Kila ligi lazima iwe na giants mwanangu.
Tafakari bro usilinganishe na huko kabisaaa ...na lengo liwe zuri tu ili nasi angalau tuweze kuwa level angalau kama hizo nchi ulizotaja....shida kubwa huku kwetu pia watu wanaweka mbele ushabiki bila kuujua/kuuelewa mchezo wa mpira wa miguu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zikifutwa wachezaji wake watastaafishwa kwa lazima ama?
Wachezaji si tatizo waende timu nyingine si zitakuwepo?shida ni kuondoa mfumo wa usimba u yanga ktk damu za watu ujue ni jambo la hatari mno...watu wanakua wajinga aisee....fikiria jana watu tunaangalia Final ya Mancity vs Aston villa baada ya villa kufungwa goli la pili watu wakabadili channel na kuweka mpira wa Simba na Kmc ...na Majority pale hawakuona ubaya sie tukahama fasta kijiwe...sasa huo si ujinga?unathubutu vipi kuondoa mechi kama ile?watu hawaelewi big match ni nini...
Wanachofikiria kwenye akili ni simba,yanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hebu mwelekeze nduguyo maana kapiga bonge moja la Pumba an chaaa!
Take it from me kwa usimba na uyanga wenu kama nchi hii itakuja kufikia kufikia hata namba 70 ya rank za Fifa mpaka wote tutaondoka hapa duniani....
Mtaishia kuwasikiliza Manara na Murro wakirushiana vijembe tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usisahau miaka ya 1970s ziligawanyika na haikusaidia. Kumbuka Pan African na Nyota nyekundu. Mbaya hizi timu zimekuwa kama dini (imani). Wakati mwingine nami nazichukia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niamini simba yanga ni tatizo.timu ndogo kila zikiibuka hapa zinauliwa na hizo timu mbili...leo hii mbeya city iko wapi...mbao...mtibwa....hata wachezaji zinaua samatta angesema abaki hapa saa hizi angekua dalali wa kupangisha nyumba
Nchi kuwa na timu kubwa sio kesi lkn si simba na yanga
Twaweza tukawa na Azam na Namungo...inawezekana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina wasiwasi na kinywaji unachotumia, hivi Rwanda, Burundi, Malawi na msumbiji ili wapande viwango wanatakiwa waondoe team gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbuka hizo nchi labda Malawi na Rwanda kidogo karibia wote Burundi na Msumbiji wako vizuri kutuzidi!
Leo hii Madagascar wapo wapi?Cape verde wapo wapi?ukumbuke miaka ya nyuma sisi tuliwafungafunga sana
Wenzetu hawaendekezi ushabiki kama dini
Tutafute namna ya kuliinua taifa kisoka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli umeona ee sasa hapa hii sumu ya hizi timu mbili imesambaa sana dawa kuiondoa kabisa kama corona tu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tangu lini taasisi inayoongozwa na mswahili ikapiga hatua.

Hivi kwanini YANGA ikomalie kukaa pale KARIAKOO Bondeni eti ilimradi tu waonekane wanakaa TOWN KARIAKOO ??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…