Ili kuwasaidia Machinga, ipo haja ya kuvisajili vitambulisho vyao BRELA na kuwapa TIN

Ili kuwasaidia Machinga, ipo haja ya kuvisajili vitambulisho vyao BRELA na kuwapa TIN

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Salaam wakuu,

Moja wapo ya Initiatives za awamu ya tano katika kuboresha maisha ya watu wake ilikuwa ni kuwatambua na kuwaruhusu wafanyabiashara wadogo qadogo, jambo hilo lilifanikiwa kwa asilimia kubwa na kuiwezesha serikali kupata mapato yake.

Awamu ya sita (6) imeonekana kutokuwa mbali sana na awamu ya tano hivyo sitegemei kuona mabadiliko makubwa katika hili.

Baada ya kuwatambua wafanyabiashara hao ili kuwawezesha kukuza mitaji na kuboresha maisha yao kwa kuweza kuipata mitaji hiyo toka taasisi mbali mbali za kifedha ni vyema sasa serikali ikaona umuhimu wa kuviboresha vitambulisho vya machinga, kwa kufanya hivyo si tu kutawasaidia machinga bali kutaifanya serikali kupanua wigo wa kodi kuliko kutegemea vyanzo vile vile vya mapato.

Kupitia brela upo utaratibu wa mtu mmoja kurasimisha biashara yake kwa kusajili jina la Biashara, (business name) utaratibu ambao utamuwezesha mhusika kuwa na namba ya mlipa kodi ama TIN.

Kumuondoa machinga kutoka kumiliki kitambulisho pekee mpaka kumiliki jina la biashara itakua hatua kubwa ya kumfanya kuwa mmoja wapo wa washiriki katika kukuza uchumi kupitia kodi na kumfanya kuongeza kipato chake kwani itakuwa rahisi kwake kuaminika na si tu taasisi za fedha ambazo anaweza pata mikopo bali na watu binafsi na jamii kwa ujumla.

Naamini kwa dhamira hii ya serikali ya kuboresha maisha ya watu itazingatia na kuufanyia kazi ushauri huu.

Wasalaam,

Statesman.
 
Alafu ukiwasajili brella wawe tin
Waendele kupanga biashara barabarani

Ova
 
Alafu ukiwasajili brella wawe tin
Waendele kupanga biashara barabarani

Ova
Tunaongeza wigo wa walipa kodi,

Au hawatakiwi kabisa kujipatia kipato Kwa njia yeyote.
 
Tunaongeza wigo wa walipa kodi,

Au hawatakiwi kabisa kujipatia kipato Kwa njia yeyote.
Watafute kipato,lakini siyo kwa kukaa mababarani
Waandalie mazingira bora ya wao kufanya biashara...

Ova
 
Tunaongeza wigo wa walipa kodi,

Au hawatakiwi kabisa kujipatia kipato Kwa njia yeyote.
Kuna mtu namjua alikujaga na idea ya kuanzisha umoja wa machinga tanzania
Mkakati wake ulikuwa kabambe na jamaa
Angefaulu angeweza kutawala nchi
Sema alipigwa pini

Ova
 
Watafute kipato,lakini siyo kwa kukaa mababarani
Waandalie mazingira bora ya wao kufanya biashara...

Ova
Hii ni moja wapo ya njia za kuboresha mazingira yao ya kufanya biashara,

Haya yakifanyika wataondoka wenyewe automatically kwani mitaji Yao itakua badala ya kutumia nguvu kuwaondoa barabarani na kusababisha sinto fahamu Kwa watu wa aina hiyo.
 
Hii ni moja wapo ya njia za kuboresha mazingira yao ya kufanya biashara,

Haya yakifanyika wataondoka wenyewe automatically kwani mitaji Yao itakua badala ya kutumia nguvu kuwaondoa barabarani na kusababisha sinto fahamu Kwa watu wa aina hiyo.
Swali linakuja watawekwa wapi?

Ova
 
Hii ni moja wapo ya njia za kuboresha mazingira yao ya kufanya biashara,

Haya yakifanyika wataondoka wenyewe automatically kwani mitaji Yao itakua badala ya kutumia nguvu kuwaondoa barabarani na kusababisha sinto fahamu Kwa watu wa aina hiyo.

Machinga mmoja aliyefanikiwa huvutia machinga wengine 50, kama unadhani kuna siku watatoka barabarani fikiria vizuri.
 
Swali linakuja watawekwa wapi?

Ova
Ukisema uwatengee maeneo Yao maalum hiyo nayo haijawahi leta matokeo chanya,

Mfano mzuri Machinga Complex pale Kuna panya tu wamejaa hakuna biashara.
 
Machinga mmoja aliyefanikiwa huvutia machinga wengine 50, kama unadhani kuna siku watatoka barabarani fikiria vizuri.
Sasa unafikiri watakwenda wapi??

Kwenda kuvunja nyumba za watu na kuiba??

So long as ni shughuli halali kabisa, Wacha wafanye,

Sio lazima tufanane na miji mingine duniani,

Tunaweza waruhusu na kuwatengenezea namna Bora ya kufanya hizo biashara.

Tukumbuke kuwa wale ni binadamu na wanamahitaji na sio Kila mtu anaweza ajiriwa au kufungua duka au supermarket.
 
Sasa unafikiri watakwenda wapi??

Kwenda kuvunja nyumba za watu na kuiba??

So long as ni shughuli halali kabisa, Wacha wafanye,

Sio lazima tufanane na miji mingine duniani,

Tunaweza waruhusu na kuwatengenezea namna Bora ya kufanya hizo biashara.

Tukumbuke kuwa wale ni binadamu na wanamahitaji na sio Kila mtu anaweza ajiriwa au kufungua duka au supermarket.

Unawaza pafupi sana.
 
Ok boresheni kama mlivyoahidi.
 
Back
Top Bottom