Ili ufukara uwaondoke Watanzania Serikali ifanye jambo hili

Ili ufukara uwaondoke Watanzania Serikali ifanye jambo hili

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Natoa ushauri huu kwa serikali, sitarudia tena maana Mimi nina kazi yangu na nina biashara zangu.

Umaskini na ufukara bado ungalipo hapa nchini.

Serikali sasa haina budi kujenga chuo Cha fundi kila kata au Kijiji na kupeleka walimu na vitendea kazi.

Vijana wasome bure, yaani kila kijana aliye tayari serikali igharamie masomo yake mpaka ngazi ya cheti cha awali, na watakaofaulu vizuri wasomeshwe mpaka ngazi ya stashahada (Diploma).

Kwa watakaotaka kuendelea na ujuzi ila hawana pass za juu wachangie asilimia kidogo na serikali iweke kilichobaki.
Hapo tutaona Mapinduzi ya viwanda kwa vitendo.

Vijana watafanya mambo ya ajabu na makubwa.

Gharama ya ndege 5 za abiria inaweza kufanya hili jambo kwa ushindi mkubwa.

Wananchi wataiheshimu serikali, wapinzani tutaiheshimu serikali.

Umaskini na ufukara vitaondoka kirahisi kabisa.

Msitujazie ma flyover huku vijana wengi hawana ujuzi wapo tu mitaani.

Hawa wamachinga hawakuzi uchumi wa Tanzania kwa asilimia kubwa bali wanakuza uchumi wa Uchina ambako bidhaa zinatoka
Hizi kozi zingine kama Human resources, Accounts, Social works and alike sasa zianze kupunguzwa na NACTE na TCU wakati wa udahili na usajili wa vyuo vipya.

Pia serikali iwe inaweka ligi ya kiufundi miongoni mwa vijana na washindi 100 au kumi kupewa zawadi kila mwaka. Zawadi hizo ziwe mitaji/fedha au vitendea kazi.
 
Mfumo wetu wa elimu upo devised especially kwaajili ya watanzania masikini ili watawala waendelee kutukandamiza.

Ndio maana wao wanasomesha watoto wao nje ya nchi ambapo elimu inayotolewa itawasaidia kuja kuendelea kutunyonya.

We are doomed.
 
Una mawazo mazuri sana.

Ila fahamu kuwa ccm na serikali yake kwa sasa wanapinduana wao kwa wao.

Huo muda wa kukuletea maendeleo yako sijui uondokane na ufukara hawana kabisa!

Kodi yako wanakula.

Tozo zako wanabugia.

Na wanaamini huna cha kuwafanya.
 
Kuondokana na umaskini ni swala la kimtazamo tu

Hii nchi ina fursa nyingi sana tatizo Sisi tulichoambiwa na kutupotosha ni kubatizwa kuwa tu wanyonge

Sasa kazi kwako kuondoka kwenye unyonge. Elimu haina msaada wowote kukutoa kwenye umaskini (unyonge)

Jiondoe kwenye Mtandao wa Wanyonge maana hata mbinguni vinyonge wala vidhaifu Yesu keshasema havitaingia

Kazi ni kwako
 
Ndani ya miaka 3 jinsi ya kuleta maendeleo na kumaliza tatizo la ajira nchini.

1.Ondoa futa kodi zote za kuingiza magari ya mizigo na abiria nchini kodi yake utaipata mara mbili yake kupitia indirect tax.Kwenye mafuta,leseni za udereva, fine za traffic, parking fee, ushuru wa stand, spare za magari, leseni na vibali mbalimbali.Gari moja uajiri si chini ya vijana 3.

2.Toa ruzuku kwenye viwanda vya kuzalisha matrekta wazalishe matreka mengi waje watuuzie wakulima kwa robo bei trekta moja uajiri zaidi ya watu wanne.

3.Jenga schemes za umwagaliaji KILA kijiji upitapo mto pande zote mbili watu walime mwaka mzima ni aibu sana kwa maji ya mito kumwaga maji yake baharini badala ya mashambani.Soko la mazao nje ya nchi lipo tele

4.Jenga vyuo vya ujuzi kila kata kopesha vijana ujuzi baada ya kumaliza darasa la saba wakapate ujuzi wautakao.

Kukopesha vijana waende chuo kikuu kisha warudi mtaani kuendesha bodaboda na kuwa machinga ni upotevu Mkubwa Sana wa kodi zetu na kuongeza idadi ya masikini nchini.

5.Fungua mipaka watu wauze watakapo nje ya nchi kuna masoko tele.Legeza masharti ya vibali Ili export ikue.

Ni sekta mbili tu zingine takataka hazifikii kilimo na madini kwa kuajiri vijana wote nchini na kuongeza pato la taifa bila kutegemea kukopa na kukamua kodi wananchi.

6.Peleka KILA kijiji mashine za kutengeneza interlocking block na vigae Ili watz wote wajenge nyumba bora kwa gharama nafuu kabisa

Mjerumani kwa miaka 15 alituletea maendeleo makubwa Sana ccm imeshindwa nini.
 
Huwa serikali inajisikiaje pale inapochezea kodi zetu kwa kuwapa wanafunzi mikopo wanamaliza vyuo kisha inashindwa kuwaajiri, wanaishia kuwa machinga, bodaboda, mamalishe ambapo hawawezi rudisha tena mikopo hio.
 
Ulikuwa vipi huo mfumo?
Tell me shortly
Elimu ya vitendo zaidi.

Watu walifundishwa study za Kazi elimu ya msingi mtu akimaliza la nane anaingia kwenye uzalishaji mali.

So unakuwa na wahitimu wengi ambao wanajitegemea zaidi na sio wengi wangoja ajira.
 

Mleta mada hauamini matokeo haya?
 
Natoa ushauri huu kwa serikali, sitarudia tena maana Mimi nina kazi yangu na nina biashara zangu.

Umaskini na ufukara bado ungalipo hapa nchini.

Serikali sasa haina budi kujenga chuo Cha fundi kila kata au Kijiji na kupeleka walimu na vitendea kazi.

Vijana wasome bure, yaani kila kijana aliye tayari serikali igharamie masomo yake mpaka ngazi ya cheti cha awali, na watakaofaulu vizuri wasomeshwe mpaka ngazi ya stashahada (Diploma).

Kwa watakaotaka kuendelea na ujuzi ila hawana pass za juu wachangie asilimia kidogo na serikali iweke kilichobaki.
Hapo tutaona Mapinduzi ya viwanda kwa vitendo.

Vijana watafanya mambo ya ajabu na makubwa.

Gharama ya ndege 5 za abiria inaweza kufanya hili jambo kwa ushindi mkubwa.

Wananchi wataiheshimu serikali, wapinzani tutaiheshimu serikali.

Umaskini na ufukara vitaondoka kirahisi kabisa.

Msitujazie ma flyover huku vijana wengi hawana ujuzi wapo tu mitaani.

Hawa wamachinga hawakuzi uchumi wa Tanzania kwa asilimia kubwa bali wanakuza uchumi wa Uchina ambako bidhaa zinatoka
Hizi kozi zingine kama Human resources, Accounts, Social works and alike sasa zianze kupunguzwa na NACTE na TCU wakati wa udahili na usajili wa vyuo vipya.

Pia serikali iwe inaweka ligi ya kiufundi miongoni mwa vijana na washindi 100 au kumi kupewa zawadi kila mwaka. Zawadi hizo ziwe mitaji/fedha au vitendea kazi.
Taratibu mnaanza kuamka kuwa yale maflai ova yake ya kujimwambafai hayana msaada mkubwa kwa watanzania walio wengi. Mama atawafanyia yote hayo mpaka mtashangaa. Akishamaliza kwenye kilimo na ufugaji, next step ni vyuo vya ufundi.
 
Taratibu mnaanza kuamka kuwa yale maflai ova yake ya kujimwambafai hayana msaada mkubwa kwa watanzania walio wengi. Mama atawafanyia yote hayo mpaka mtashangaa. Akishamaliza kwenye kilimo na ufugaji, next step ni vyuo vya ufundi.
Ok
 
Back
Top Bottom