Ilikuwa raha sana, ukiwa na girl friend ni simu za TTCL au unaenda kwao kuomba maji ya kunywa, akitoka dada unamuuliza Fulani yupo? Akitoka mama au baba unakunywa maji hata kama huna kiu unaondoka.Dah... Enzi hizo kupata dem lazima u andike barua.... Wengine wamezitunza hadi Leo.... Na wewe unazo?
Sikinde sogea ukae, watu njatanjata , miaka Hiyo komando hamza anakwenda kung'oa mtoto wa Mzee cheyo tajiri, bendi Ni bendi kweli Hiyo kigogo lodge husogei akina kajamba nani acheni tu laizoni Viatu, suruali za bugaruu suspender kiunoni .Vijana jazz usiwasahau. Pia unawakumbuka wakina Bichuka, Shabani Dede.
Sikuzile Bima Lee ilikuwa ikimilikiwa na Shirika La Bima La Taifa ( National Insurance Corporation, NIC), bendi hii ilitikisa vilivyo enzi zake, ilikuwa inakusanya nguli wengi wenye uwezo wa hali ya juu na waliochangia mafanikio makubwa katika bendi hiyo.Bima Lee
Watunjatanjata 'washirika'
'Air pambamoto' Vijana
Mambo ya long
Vijana walio zaliwa kwa mipango ya vidonge na sindano....[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]ha ha ha,ndo maana umekuwa mzito kuelewa jamaa anamaanisha nini,nikajua tu wewe ni kizazi cha wakati wa jakaya,
Umenikumbusha mbali sana mkuu.Ilikuwa raha sana, ukiwa na girl friend ni simu za TTCL au unaenda kwao kuomba maji ya kunywa, akitoka dada unamuuliza Fulani yupo? Akitoka mama au baba unakunywa maji hata kama huna kiu unaondoka.
Kulikoni mkuu.....[emoji12]
Kulikuwa na kijana mmoja alikuwa anakuja nyumbani jioni, alikuwa anatrot akifika getini anaomba maji kwa mlinzi, mlinzi akija aniambia mgeni wako amefika, kama msure yupo inabidi mlinzi apewe maji.Umenikumbusha mbali sana mkuu.
Hii ilwahi nitokea pale maeneo ya bamaga miaka ileeeee..... Nilisahau lazimika kununua maziwa (mtindi) pale nilipienda kuzoza, kisha nikamkuta Baba wa binti ndio yupo dukani.
Alafu bahati yangu mbaya, hiyo pesa (ilikua shilingi 10 ya noti) nilikua nimetumwa nikanunue chumvi dukani.....[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Mkuu enzi hizo hapo Lang'ata social hall kulikua ma ma dj's Chriss phabby na Young millionaire.Mkuu....,
Sikuzile Kinondoni ilkuwa inawaka moto kwa Vijana siku ya Jumapili. Lang'ata ambayo baadae ilikuja kuwa Club ASET na sasa kanisa, palikuwa ndo ukumbi wa Dansi za kuanzia mchana kwa Bendi ya Maquis. Ukija hapa mbele Vijana Jazz Pambamoto awamu ya pili chini ya uongozi wa Hemed Maneti walikuwa nao kila Jumapili mchana wanaporomosha Dansi, na siku hiyo ilipewa jina Vijana Day. Kwa kweli Maquis walikuwa wanajaa watu na Vijana wanajaa watu. Kulikuweko na wapenzi wa kudumu wa Vijana kama ilivyokuwa Maquis. Wakati huo nyimbo kama Ngalula, Makumbele zilikuwa zinalia Lang'ata huku Vijana wanateremsha Shingo feni, Ngapulila, Azda. Ushindani huu ulilazimisha bendi kujitahidi kupiga vizuri na kwa displine au la wapenzi wanahamia bendi jirani. Kuna wakati Vijana Jazz walikuwa wanaanza muziki saa kumi na moja jioni na kupumzika saa tatu na nusu usiku kisha kumaliza dansi saa nne. Maquis wakawa wanaanza saa kumi na kumaliza saa tano usiku. Na wakaanza kuruhusu mtu yeyote atakayekuwa kapigwa muhuri wa kuruhusu kutoka nje ya ukumbi Vijana Jazz,aliruhusiwa kuingia Maquis bure. Vijana wakabadili ratiba na kuanza kupiga saa 9 mchana, kwa mtindo wa bandika bandua, yaani muziki nonstop. Na kufuta kupumzika hadi saa tano. Hiyo ndo ilikuwa raha kwa wapenzi. Vijana haikuwa na show wakati wa Maneti, Lakini show ilikuja baadae katika kukabili show ya Maquis ambayo ilikuwq nzuri sana chini ya mwalimu wao Wabangoi. Majina makubwa yalitawala madansi hayo Maquis kulikuwa na Dekula Vumbi kwenye solo,second solo Mbwana Cox (aliyetoka Vijana Jazz), banza Mchafu Bass, Nguza Viking, Adios, Tshimanga Assossa,Parashi Lukumbule Vijana Jazz kulikwa Shaaban Wanted, Hemed Maneti, Eddy Sheggy, Adam Bakari, Kida Waziri, Abou Semhando, Rashid Pembe na wengine wengi, basi raha kila jumapili ilikuwa kama tamasha
Dah... Ulisalimika na kichapo siku hiyo?? [emoji13] [emoji13]Umenikumbusha mbali sana mkuu.
Hii ilwahi nitokea pale maeneo ya bamaga miaka ileeeee..... Nilisahau lazimika kununua maziwa (mtindi) pale nilipienda kuzoza, kisha nikamkuta Baba wa binti ndio yupo dukani.
Alafu bahati yangu mbaya, hiyo pesa (ilikua shilingi 10 ya noti) nilikua nimetumwa nikanunue chumvi dukani.....[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Dah... Atakuwa kijana wa mwendokasi huyo [emoji13] [emoji13]Kulikoni mkuu.....[emoji12]
Naona unaguna tu...[emoji23]
Wakati vitabu vya Mr and Mrs Daudi vinaanza kuingia.
Du hadithi ya Bulicheka na mkewe Eliza.
Dah... Na bora hamkuwepo...kwani Msingeweza....kulikuwa hakuna ku google .....machimbo yalikuwa vitabuni tu[emoji13] [emoji13]wengine hatukuwepo kabisa enzi hizo