Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 989
Ukittafakari mfululizo wa kalenda na matukio, basi inawezekana kuna jambo ambalo hatulijui.
Mwalimu Nyerere aliachia uenyekiti wa CCM, Friday, August 17, 1990 huku Mkutano mkuu wa CCM ukiwa kikaoni.
Mkutano huo ndiyo ulimuweka mwenyekiti mpya, Ali Hassan Mwinyi na katibu akawa Horace Kolimba. Lakini mkutano huo pia, ndiyo uliompitisha Salmin Amour agombee urais Zanzibar kwa mara ya kwanza.
Hivyo, mkutano ulipoisha, shughuli iliyofuata ni pilika za uchaguzi uliofanyika Zanzibar, Sunday, October 21, 1990 na Bara ukafanyika, Sunday, October 28, 1990.
Zikafuata pilika za kuchagua cabinets kwenye mwezi November, na baada tu ya cabinets, zikafuata pilika za haraka za Waziri mpya wa mambo ya ndani aitwaye Augustine Mrema ambaye ndani ya mwezi mmoja alishatoa amri zaidi ya nne za majukumu yatekelezeke ndani ya siku saba.
Kiserikali, tukio kuu lililofuata ni sherehe ya Mapinduzi Zanzibar yaani January 12, 1991.
Tukio lililofuata ndilo limenifanya niandike post hii, nalo ni NEC ya CCM kukutana Zanzibar kuanzia February 14, 1991. Utaona kwamba hiki ndicho kikao cha kwanza kichama baada ya mkutano ule aliong'atuka Nyerere yaani siku 181 tu tangu Nyerere aachane na uenyekiti.
Ni wazi kwamba agenda kuhusu uchaguzi ingeweza kuwemo kwenye kikao hiki. Kwa ujumla kikao hiki ni cha kihistoria kwa CCM yaani ndicho kikao cha kwanza Nyerere akiwa si mwanasiasa.
Sasa, kikao hiki cha kwanza Nyerere akiwa si mwanasiasa kiliongelea nini? Kikao hiki ndicho wengi husema kiliua Azimio la Arusha na kikapewa jina Azimio la Zanzibar. Mtakaojadili na kuingia sana kuhusu kuaawa Azimio la Zanzibar mimi si hoja yangu.
Mimi hoja yangu ni kunisaidia kujiuliza na kupata majibu kwamba, kulikuwa msukumo gani ambao ulisubiri tu Nyerere aondoke madarakani halafu Azimio lake la Arusha lifutwe kikao kinachofuata cha chama. Ajenda za kikao hiki ziliandaliwa lini?
Kama sikosei, ni wazi ajenda za kikao hiki ingewezekana Mwalimu alikuwa anazifahamu kwa kuchukulia kwamba haiwezekani uwe mwenyekiti wa chama halafu usiwe na fununu au dalili za kujua ajenda za kikao kinachofuata ziwe ni za jambo gani.
je, kuna uwezekano kwamba Mwalimu alijua kwamba kikao kinachofuata baada ya Mkutano Mkuu wa August kitakuwa ni cha kufuta Azimio la Arusha? Kama alijua basi binafsi ninaona heri lilifutwa akiwa ameshaondoka, maana sijui angesimamia vipi ajenda hiyo.
Kama mwalimu hakujua ajenda za next meeting, je, walioandaa ajenda, waliwezaje kumficha mwalimu hadi dakika anaondoka kitini, kukafuatiwa na uchaguzi na mambo ya cabinet mpya.
Nasema hivi kwa sababu ajenda ya kufuta Azimio la Arusha haikuwa ajenda ndogo. Nashindwa kuamini kwamba ajenda kubwa kama hii iibuke tu ndani ya mwezi mmoja baada ya taifa kutoka uchaguzini.
Na kama chamani walikuwa wanweza kutunza siri hadi mwalimu asijue, basi ingekuwa busara zaidi walau kusubiri hadi August 1991 ambapo ingekuwa umepita mwaka mzima na vikao kadhaa vya NEC vimeshapita na ajenda zingine walau za kufumbafumba , kuliko kusubiri kikao kinachofuata baada ya Mwalimu kuondoka ndipo makucha yaonekane.
Naamini humu JF kuna wanaoweza kujua zaidi. Narudia, najiuliza speed ya kufanya jambo lile kubwa, lionekane limekuja ghafla, wakati haikuwa rahisi kwa Mwalimu kufichwa jambo kirahisi eti alipoondoka tu kikao kilichofuata kikaamua kusema alhamdulilah paka katoka sasa panya atawale, to hell with Azimio la Arusha.
SAIDIA KUTAFAKARI
Mwalimu Nyerere aliachia uenyekiti wa CCM, Friday, August 17, 1990 huku Mkutano mkuu wa CCM ukiwa kikaoni.
Mkutano huo ndiyo ulimuweka mwenyekiti mpya, Ali Hassan Mwinyi na katibu akawa Horace Kolimba. Lakini mkutano huo pia, ndiyo uliompitisha Salmin Amour agombee urais Zanzibar kwa mara ya kwanza.
Hivyo, mkutano ulipoisha, shughuli iliyofuata ni pilika za uchaguzi uliofanyika Zanzibar, Sunday, October 21, 1990 na Bara ukafanyika, Sunday, October 28, 1990.
Zikafuata pilika za kuchagua cabinets kwenye mwezi November, na baada tu ya cabinets, zikafuata pilika za haraka za Waziri mpya wa mambo ya ndani aitwaye Augustine Mrema ambaye ndani ya mwezi mmoja alishatoa amri zaidi ya nne za majukumu yatekelezeke ndani ya siku saba.
Kiserikali, tukio kuu lililofuata ni sherehe ya Mapinduzi Zanzibar yaani January 12, 1991.
Tukio lililofuata ndilo limenifanya niandike post hii, nalo ni NEC ya CCM kukutana Zanzibar kuanzia February 14, 1991. Utaona kwamba hiki ndicho kikao cha kwanza kichama baada ya mkutano ule aliong'atuka Nyerere yaani siku 181 tu tangu Nyerere aachane na uenyekiti.
Ni wazi kwamba agenda kuhusu uchaguzi ingeweza kuwemo kwenye kikao hiki. Kwa ujumla kikao hiki ni cha kihistoria kwa CCM yaani ndicho kikao cha kwanza Nyerere akiwa si mwanasiasa.
Sasa, kikao hiki cha kwanza Nyerere akiwa si mwanasiasa kiliongelea nini? Kikao hiki ndicho wengi husema kiliua Azimio la Arusha na kikapewa jina Azimio la Zanzibar. Mtakaojadili na kuingia sana kuhusu kuaawa Azimio la Zanzibar mimi si hoja yangu.
Mimi hoja yangu ni kunisaidia kujiuliza na kupata majibu kwamba, kulikuwa msukumo gani ambao ulisubiri tu Nyerere aondoke madarakani halafu Azimio lake la Arusha lifutwe kikao kinachofuata cha chama. Ajenda za kikao hiki ziliandaliwa lini?
Kama sikosei, ni wazi ajenda za kikao hiki ingewezekana Mwalimu alikuwa anazifahamu kwa kuchukulia kwamba haiwezekani uwe mwenyekiti wa chama halafu usiwe na fununu au dalili za kujua ajenda za kikao kinachofuata ziwe ni za jambo gani.
je, kuna uwezekano kwamba Mwalimu alijua kwamba kikao kinachofuata baada ya Mkutano Mkuu wa August kitakuwa ni cha kufuta Azimio la Arusha? Kama alijua basi binafsi ninaona heri lilifutwa akiwa ameshaondoka, maana sijui angesimamia vipi ajenda hiyo.
Kama mwalimu hakujua ajenda za next meeting, je, walioandaa ajenda, waliwezaje kumficha mwalimu hadi dakika anaondoka kitini, kukafuatiwa na uchaguzi na mambo ya cabinet mpya.
Nasema hivi kwa sababu ajenda ya kufuta Azimio la Arusha haikuwa ajenda ndogo. Nashindwa kuamini kwamba ajenda kubwa kama hii iibuke tu ndani ya mwezi mmoja baada ya taifa kutoka uchaguzini.
Na kama chamani walikuwa wanweza kutunza siri hadi mwalimu asijue, basi ingekuwa busara zaidi walau kusubiri hadi August 1991 ambapo ingekuwa umepita mwaka mzima na vikao kadhaa vya NEC vimeshapita na ajenda zingine walau za kufumbafumba , kuliko kusubiri kikao kinachofuata baada ya Mwalimu kuondoka ndipo makucha yaonekane.
Naamini humu JF kuna wanaoweza kujua zaidi. Narudia, najiuliza speed ya kufanya jambo lile kubwa, lionekane limekuja ghafla, wakati haikuwa rahisi kwa Mwalimu kufichwa jambo kirahisi eti alipoondoka tu kikao kilichofuata kikaamua kusema alhamdulilah paka katoka sasa panya atawale, to hell with Azimio la Arusha.
SAIDIA KUTAFAKARI