Ilikuwaje mababu zetu wakapokea dini za kigeni hata bila kuhoji?

Ilikuwaje mababu zetu wakapokea dini za kigeni hata bila kuhoji?

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
Hakuna ubishi kuwa baada ya kukubali au tuseme kuingizwa mkenge na kupokea dini nyemelezi za kigeni, tulipoteza kila kitu.

Tulipoteza utambuliko wetu, majina yetu, utu wetu, upendo wetu, ushirikiano wetu, dini zetu na kuteuka vikaragosi vya kiimani. Leo watu wanajiita wakristo au waislam lakini si waswahili. Wanachukiana hata kuuana wao kwa wao. Wanaibiana kwa kuuza neno la mungu. Wamegeuka wavivu wa kutofanya kazi wala kufikiri na kutegemea miujiza.

Tumejenga misikiti na makanisa mengi kuliko viwanda na mashule na vitu vingine vya maana. Tulianza kuchukia vitu vyetu na wenzetu na kuabudia vya wageni hadi watu wanaapia miji ya watu utadhani hawana miji.

Tulifundishwa utakatifu feki unaowatukuza washenzi waliotuuza na kututawala. Walitwambia tusiibe, wakatuibia. Walisema tusidanganye wakatudanganya. Walisema tusie, wakatuua. Walisema tusitamani mali. ya mtu baada ya kutuibia na kutajirika. Walitufundisha kupendana wakati wakituchukia hadi leo. Orodha ni ndefu kweli kweli.

Tumepoteza kila kitu na kuwa watumwa wa dini na waliozibuni na kutuletea. Je ilikuwaje mababu zetu wakakubali ujinga huu?
 
Huwezi kumtoa FaizaFoxy kwa waarabu
Ustaarabu.

Au ulimaanisha Uislam? kuwa muwazi tu, usiuogope Uislam na Uarabu kwa kudanganywa tu.

Huna shemeji au mjomba wa Kiarabu wewe?

Au kwa siku hizi tuseme, hauna dada au shangazi wa Kiarabu? Maana siku hizi wanawake wa Kitanzania nusu yao ni Waarabu.
 
Ustaarabu.

Au ulimaanisha Uislam? kuwa muwazi tu, usiuogope Uislam na Uarabu kwa kudanganywa tu.

Huna shemeji au mjomba wa Kiarabu wewe?

Au kwa siku hizi tuseme, hauna dada au shangazi wa Kiarabu? Maana siku hizi wanawake wa Kitanzania nusu yao ni Waarabu.
Waarabu ni wachache sana unless unaishi pwani. But mail land interior sio wengi and ni wachache sana. Wengi ni wabantu
 
Waarabu ni wachache sana unless unaishi pwani. But mail land interior sio wengi and ni wachache sana. Wengi ni wabantu
hata bungeni wamejazana, au bungeni ni pwani? Upo mkoa upi Tanzania hii ambako mkorogo haujafika?

Uarabu wanaununuwa kwa pesa nyingi.
 
hata bungeni wamejazana, au bungeni ni pwani? Upo mkoa upi Tanzania hii ambako mkorogo haujafika?

Uarabu wanaununuwa kwa pesa nyingi.
Wanaopaka mkorogo ni waarabu au unaongelea waarabu kwa damu?
Bungeni wako wangapi?
 
Hakuna ubishi kuwa baada ya kukubali au tuseme kuingizwa mkenge na kupokea dini nyemelezi za kigeni, tulipoteza kila kitu.

Tulipoteza utambuliko wetu, majina yetu, utu wetu, upendo wetu, ushirikiano wetu, dini zetu na kuteuka vikaragosi vya kiimani. Leo watu wanajiita wakristo au waislam lakini si waswahili. Wanachukiana hata kuuana wao kwa wao. Wanaibiana kwa kuuza neno la mungu. Wamegeuka wavivu wa kutofanya kazi wala kufikiri na kutegemea miujiza.

Tumejenga misikiti na makanisa mengi kuliko viwanda na mashule na vitu vingine vya maana. Tulianza kuchukia vitu vyetu na wenzetu na kuabudia vya wageni hadi watu wanaapia miji ya watu utadhani hawana miji.

Tulifundishwa utakatifu feki unaowatukuza washenzi waliotuuza na kututawala. Walitwambia tusiibe, wakatuibia. Walisema tusidanganye wakatudanganya. Walisema tusie, wakatuua. Walisema tusitamani mali. ya mtu baada ya kutuibia na kutajirika. Walitufundisha kupendana wakati wakituchukia hadi leo. Orodha ni ndefu kweli kweli.

Tumepoteza kila kitu na kuwa watumwa wa dini na waliozibuni na kutuletea. Je ilikuwaje mababu zetu wakakubali ujinga huu?
Ukristo uliletwa na Yesu , si dini ya kigeni , labda una maanisha "cult" yani dini zinginezo ndio za kigeni.
 
Hakuna ubishi kuwa baada ya kukubali au tuseme kuingizwa mkenge na kupokea dini nyemelezi za kigeni, tulipoteza kila kitu.

Tulipoteza utambuliko wetu, majina yetu, utu wetu, upendo wetu, ushirikiano wetu, dini zetu na kuteuka vikaragosi vya kiimani. Leo watu wanajiita wakristo au waislam lakini si waswahili. Wanachukiana hata kuuana wao kwa wao. Wanaibiana kwa kuuza neno la mungu. Wamegeuka wavivu wa kutofanya kazi wala kufikiri na kutegemea miujiza.

Tumejenga misikiti na makanisa mengi kuliko viwanda na mashule na vitu vingine vya maana. Tulianza kuchukia vitu vyetu na wenzetu na kuabudia vya wageni hadi watu wanaapia miji ya watu utadhani hawana miji.

Tulifundishwa utakatifu feki unaowatukuza washenzi waliotuuza na kututawala. Walitwambia tusiibe, wakatuibia. Walisema tusidanganye wakatudanganya. Walisema tusie, wakatuua. Walisema tusitamani mali. ya mtu baada ya kutuibia na kutajirika. Walitufundisha kupendana wakati wakituchukia hadi leo. Orodha ni ndefu kweli kweli.

Tumepoteza kila kitu na kuwa watumwa wa dini na waliozibuni na kutuletea. Je ilikuwaje mababu zetu wakakubali ujinga huu?
Kuna sababu kadhaa za kihistoria zinazoweza kueleza ni kwa nini mababu zetu walikubali dini hizi bila kuhoji sana.

1. Ushawishi wa Kijamii na Kisiasa
Katika historia, wainjilisti wa dini hizi, hasa Wakoloni, walikuwa na mamlaka makubwa ya kisiasa. Walipokuja na nguvu hizo, waliweza kuleta mfumo wa dini wakitumia ushawishi wa serikali au hata nguvu za kijeshi. Mababu zetu waliona kuwa kukubali dini hizi ilikuwa ni njia ya kupata ulinzi, msaada wa kiuchumi, na labda pia kupata nafasi katika mfumo mpya wa kisiasa.


2. Ukosefu wa Elimu Rasmi
Wakati dini hizi zinakuja, elimu ya kisasa ilikuwa haijafika sana. Wale waliotuletea dini walikuja pia na mfumo wa elimu, hospitali, na huduma za afya. Dini hizi zilikuwa na mashiko kwa sababu zilikuja na vitu hivi ambavyo vilionekana kuwa msaada mkubwa kwa maisha ya kila siku.


3. Desturi ya Kiafrika ya Kukaribisha Wageni
Mababu zetu walikuwa na utamaduni wa ukarimu na walikuwa wanakaribisha wageni. Kwao, mtazamo ulikuwa kwamba kila mgeni ana maana, ana uzoefu na maarifa ambayo yanaweza kuwa na manufaa kwa jamii. Ni mtazamo huu wa kuheshimu mawazo ya wageni ambao ulifanya dini hizo kukubalika kirahisi.


4. Ujanja wa Wamisionari
Wamisionari walitumia mbinu za ujanja kueneza dini zao. Walitumia lugha zetu, walijaribu kuvutia kwa kutumia utamaduni wetu, na hata kujenga makanisa karibu na maeneo ya kimila. Walijua kuwa njia ya kukubalika ni kuonesha kwa kiasi kuwa wanaelewa mila na desturi za wenyeji.


5. Matumizi ya Hila na Ahadi za Mbinguni
Dini za kigeni zilitumia dhana ya maisha baada ya kifo kwa njia iliyoleta matumaini makubwa kwa mababu zetu. Wengi wao walikubali dini hizi kwa sababu walihisi kwamba zitawapatia amani ya milele baada ya kifo, jambo ambalo labda halikufafanuliwa sana kwenye imani za kimila.


6. Mapokeo na Shinikizo la Jamii
Mara nyingi, mara baada ya kikundi fulani au kiongozi kujiunga na dini, jamii nzima ilifuata mkondo huo kama ishara ya mshikamano. Mara nyingi viongozi walikuwa ni mfano kwa jamii zao, na iwapo walikubali dini, basi wengi waliifuata kwa sababu ya heshima kwa viongozi wao au shinikizo la kijamii.
 
Back
Top Bottom