Imamu kortini kwa wizi wa nyaya

Imamu kortini kwa wizi wa nyaya

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Imamu kortini kwa wizi wa nyaya


Na Yusuph Mussa, Lushoto

IMAMU wa mwalimu wa dini wa Kijiji cha Mkuzi, Kata ya Kwai wilayani Lushoto Bw. Amir Kijangwa (47) amefikishwa mahakamani akituhumiwa kuiba Nyaya za umeme zenye uzito wa kilo 19 huku zikiwa na thamani ya sh. 285,000.Akisoma
mashtaka hayo mwishoni mwa wiki kwenye Mahakama ya Wilaya ya Lushoto, Mwendesha Mashtaka, Bw. Evarist Mwamengo alisema Desemba 18, mwaka huu saa moja asubuhi Bw. Kijangwa alikamatwa na kiroba cha nyaya hizo nyumbani kwake.

Hakimu aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo, Bw. Yona Wilson alitoa dhamana kwa mtuhumiwa huyo, mara baada ya Bw. Kijangwa kukataa kosa lake na kesi inatarajiwa kutajwa tena Januari 4, mwakani.

Wakatu huo huo, Meneja wa TANESCO Wilaya ya Lushoto Bw. Said Mhando amesema wimbi la wizi wa nyaya za umeme limezidi kuongezeka baada ya watu wasiofahamika kuiba nyaya usiku wa kuamkia Desemba 20, mwaka huu.

Bw. Mhando alisema nyaya hizo zenye urefu wa mita 800 na thamani ya sh. milioni mbili ni muendelezo wa matukio hayo yaliyoanza Septemba, mwaka huu na kuwa hadi sasa yameshatokea matukio saba yaliyosababisha wikiwa nyaya zenye urefu wa mita 2,740 zenye thamani ya sh. milioni 6.8.

"Wananchi lazima waelewe TANESCO au Jeshi la Polisi hawana uwezo wa kulinda miundombinu ya umeme, na jukumu hilo ni la wananchi wenyewe kwa kuwa matokeo yake ni kukosekana huduma ya umeme.

"Lakini pia shirika linapata hasara kwa kuweka miundombinu mipya maeneo ya wizi na kuacha kuwawekea wananchi wengine wapya, lakini pia wafanyakazi wanaacha kufanya kazi mpya na kuziba mapengo ya wizi, matokeo wananchi wanalalamikia huduma inachelewa kwao," alisema Bw. Mhando.

 
Kaasi kweli Kweli!!
Anapeleka wapi hizo nyaya za wizi huyu Imamm?
 
Imamu kortini kwa wizi wa nyaya


Na Yusuph Mussa, Lushoto

IMAMU wa mwalimu wa dini wa Kijiji cha Mkuzi, Kata ya Kwai wilayani Lushoto Bw. Amir Kijangwa (47) amefikishwa mahakamani akituhumiwa kuiba Nyaya za umeme zenye uzito wa kilo 19 huku zikiwa na thamani ya sh. 285,000.Akisoma
mashtaka hayo mwishoni mwa wiki kwenye Mahakama ya Wilaya ya Lushoto, Mwendesha Mashtaka, Bw. Evarist Mwamengo alisema Desemba 18, mwaka huu saa moja asubuhi Bw. Kijangwa alikamatwa na kiroba cha nyaya hizo nyumbani kwake.

Hakimu aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo, Bw. Yona Wilson alitoa dhamana kwa mtuhumiwa huyo, mara baada ya Bw. Kijangwa kukataa kosa lake na kesi inatarajiwa kutajwa tena Januari 4, mwakani.

Wakatu huo huo, Meneja wa TANESCO Wilaya ya Lushoto Bw. Said Mhando amesema wimbi la wizi wa nyaya za umeme limezidi kuongezeka baada ya watu wasiofahamika kuiba nyaya usiku wa kuamkia Desemba 20, mwaka huu.

Bw. Mhando alisema nyaya hizo zenye urefu wa mita 800 na thamani ya sh. milioni mbili ni muendelezo wa matukio hayo yaliyoanza Septemba, mwaka huu na kuwa hadi sasa yameshatokea matukio saba yaliyosababisha wikiwa nyaya zenye urefu wa mita 2,740 zenye thamani ya sh. milioni 6.8.

"Wananchi lazima waelewe TANESCO au Jeshi la Polisi hawana uwezo wa kulinda miundombinu ya umeme, na jukumu hilo ni la wananchi wenyewe kwa kuwa matokeo yake ni kukosekana huduma ya umeme.

"Lakini pia shirika linapata hasara kwa kuweka miundombinu mipya maeneo ya wizi na kuacha kuwawekea wananchi wengine wapya, lakini pia wafanyakazi wanaacha kufanya kazi mpya na kuziba mapengo ya wizi, matokeo wananchi wanalalamikia huduma inachelewa kwao," alisema Bw. Mhando.

Mwizi ni mwizi tu hata awe imam.................. LAKINI NADHANI KILICHOMSHAWISHI KUIBA NI SHIDA ZAKE NA SI DINI YAKE............
 
Uwoo ndg zangu washambaa saasa inakuaje tena huko kaya jamani, huyu imamu si ndio mkwewe Malaria Sugu huyu..
 
watu wote huwa tunakosa jamani, na tukikosa tunapata nafasi ya kutubu. Yesu alikuja dunia na ujumbe wa "Tubani na Kuiamini Injili" kwa hili tunatambua kila mtu anadhambi na ana nafasi wakati wowote kupewa nafasi ya kutubu na kumrudia MUUMBA Mbingu na nchi.
 
Back
Top Bottom