Imani yangu imeyumba, ushauri wenu

Imani yangu imeyumba, ushauri wenu

flulanga

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2016
Posts
4,860
Reaction score
6,390
Habarini wanajf, mimi nimjasiriamali ninabiashara ambayo ninaifanya yaani nimejiajiri. Biashara ninaifanya kwenye kibanda chachuma ambacho nilikichongesha

Niende kwenye dhumuni lahuu uzi, Leo nimefika kibandani nimekutana nahali yasintofahamu.... Nimekuta pale wanaposimamiaga wateja pindi ninapowahudumia kuna damu kama matonematone kama vile damu ilikuwa inachuruzika kutoka juu.

Hakuna dalili yoyote yakama kuna watu labda walizozana pale wakapigana yaani papo shwariii kabisa ila hiyo damu ndio najiuliza imetoka wapi?

Nisiwe muongo kiukweli mawazo yangu yameenda kwenye ushirikina kabisa.

Kama kuna muelewa wahaya mambo anisaidie kiukweli naukizingatia nisehemu yabiashara.
 
Weka picha mkuu ili wataalamu wakusaidie boss. Halafu hiyo attitude uliyonayo ebu jitahidi kuiacha boss itakukwamisha sana.

Hayo mambo yapo ila siyo kuyahisi kila jambo linapokutokea. Anyway, tuone picha ya hayo matone ya damu kwanza ndo tuendelee vizuri
 
Inawezekana alisimama au alipita binadamu au mnyama kama mbwa au paka alie umia.
Punguza woga na hizo imani vinginevyo bishara yako itafilisika sababu pesa unapeleka kwa waganga wa kienyeji au kwa ciongozi wa dini matapeli.
 
Inawezekana alisima au alipita binadamu au mnyama kama mbwa au paka alie umia.
Punguza woga na hizo imani vinginevyo bishara yako itafilisika sababu pesa unapeleka kwa waganga wa kienyeji au kwa ciongozi wa dini matapeli.
Nikweli mkuu ila kusema mtu alipita sio virahisi kwasababu kibanda kipo pembeni kabisa mwabarabara, vilevile ile damu ilikuwa sehemu moja2 haioneshi imetokea wapi wala inaelekea wapi
 
Weka picha mkuu ili wataalamu wakusaidie boss. Halafu hiyo attitude uliyonayo ebu jitahidi kuiacha boss itakukwamisha sana.

Hayo mambo yapo ila siyo kuyahisi kila jambo linapokutokea. Anyway, tuone picha ya hayo matone ya damu kwanza ndo tuendelee vizuri
Nimeyamwagia maji nakuyasugua nafagio maana ilikuwa haileti picha nzurii
 
Nikweli mkuu ila kusema mtu alipita sio virahisi kwasababu kibanda kipo pembeni kabisa mwabarabara, vilevile ile damu ilikuwa sehemu moja2 haioneshi imetokea wapi wala inaelekea wapi
Kwani haiwezekani mtu akavuka barabara akaja kujihudumia hapo?
Pia inaweza kuwa kuna mtu anataka kukutisha uamishe biashara, si unajua ushindani wa biashara?
 
Kama kibanda kinahamishika kisogeze pembeni yake,Kijana ondoa woga
 
Nahisi niliwahi kuandika humu ila nitarudia.

Fremu ya bro ni ile ya mageti ya kushusha. Siku moja tunafika pale tunafungua akatoka paka ndani.

Hatukusema kitu si mimi wala yeye.

Baada ya muda siku hiyo tunafungua akatoka tena paka.

Hakimbii.

Safari hii majirani wakaona tukio mpaka mmoja akaja akamuelekeza bro kwa mganga. Alipoondoka yule jirani nikamuuliza "Unaenda kwa mganga?" Akajibu "Hapana, hili geti la kushusha inaonesha halifiki mpaka chini hivyo huyu paka anapata urahisi wa kuingia"

That simple.

So boss wazia kua viumbe karibia vyote vina damu, kikijeruhiwa kikapita eneo lako of coz utakuta damu. Au let's say kuna mwanamke alisimama hapo na period ikamjia ghafla na hizo damu ni matokeo ya hilo tukio.

Kuna maelezo mengi juu ya hiyo damu ukiamua kutoamini ni uchawi. Hata sisi tungeweza sema yule paka ni ushirikina. Kwanini? Kwa sababu lile geti linafiti kiasi ni physically impossible kwa paka kupita ila tukaamini geti halifit vizuri.
 
Habarini wanajf, mimi nimjasiriamali ninabiashara ambayo ninaifanya yaani nimejiajiri. Biashara ninaifanya kwenye kibanda chachuma ambacho nilikichongesha

Niende kwenye dhumuni lahuu uzi, Leo nimefika kibandani nimekutana nahali yasintofahamu.... Nimekuta pale wanaposimamiaga wateja pindi ninapowahudumia kuna damu kama matonematone kama vile damu ilikuwa inachuruzika kutoka juu.

Hakuna dalili yoyote yakama kuna watu labda walizozana pale wakapigana yaani papo shwariii kabisa ila hiyo damu ndio najiuliza imetoka wapi?

Nisiwe muongo kiukweli mawazo yangu yameenda kwenye ushirikina kabisa.

Kama kuna muelewa wahaya mambo anisaidie kiukweli naukizingatia nisehemu yabiashara.
Safisha hiyo damu, ombea eneo lote kuzunguka kibanda chako sawasawa na imani yako. Mtangulize Mungu kabla ya kufungua na kufunga biashara yako. Hakuna uchawi wala shetani atakae kudhuru. Nakutakia mchana mwema.
 
Nahisi niliwahi kuandika humu ila nitarudia.

Fremu ya bro ni ile ya mageti ya kushusha. Siku moja tunafika pale tunafungua akatoka paka ndani.

Hatukusema kitu si mimi wala yeye.

Baada ya muda siku hiyo tunafungua akatoka tena paka.

Hakimbii.

Safari hii majirani wakaona tukio mpaka mmoja akaja akamuelekeza bro kwa mganga. Alipoondoka yule jirani nikamuuliza "Unaenda kwa mganga?" Akajibu "Hapana, hili geti la kushusha inaonesha halifiki mpaka chini hivyo huyu paka anapata urahisi wa kuingia"

That simple.

So boss wazia kua viumbe karibia vyote vina damu, kikijeruhiwa kikapita eneo lako of coz utakuta damu. Au let's say kuna mwanamke alisimama hapo na period ikamjia ghafla na hizo damu ni matokeo ya hilo tukio.

Kuna maelezo mengi juu ya hiyo damu ukiamua kutoamini ni uchawi. Hata sisi tungeweza sema yule paka ni ushirikina. Kwanini? Kwa sababu lile geti linafiti kiasi ni physically impossible kwa paka kupita ila tukaamini geti halifit vizuri.
Sawa ngoja namimi niwaze kuwa kuna mwanamke alisimama pale akiwa siku zake
 
Safisha hiyo damu, ombea eneo lote kuzunguka kibanda chako sawasawa na imani yako. Mtangulize Mungu kabla ya kufungua na kufunga biashara yako. Hakuna uchawi wala shetani atakae kudhuru. Nakutakia mchana mwema.
Amina ndugu ubarikiwe
 
Back
Top Bottom