Imebidi Marekani na Ulaya wafungashe virago Niger

Imebidi Marekani na Ulaya wafungashe virago Niger

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mara tangazo la raisi Bazoum kushikiliwa na walinzi wake lilipotoka ilionekana kama ni jaribio la mapinduzi ambalo lingeshindwa.Lakini hata hivyo kiongozi wa kikundi hicho Gen Abdourahmane Tchiani ambaye mwanzoni alitoa tangazo akiwa kifua wazi alionekana kukaza kamba na kuungwa mkono na kada nyengine za kijeshi.
Katika tangazo hilo kikundi hicho kilitoa onyo kwamba hakitaki uingiliaji kati wa mataifa ya nje.Kama kawaida mataifa hayo hayakuacha kutoa vitisho.Miongoni mwa mataifa yaliyotaka raisi Bazoum arudishwe madarakani haraka na jeshi lirudi kambini ni umoja wa ECOWAS.
Hatimae jana taifa la Marekani limetangaza kuondoa uungaji wake mkono kwa raisi Mohammed Bazoum na baadae umoja wa Ulaya nao umefuatia kusema unaondosha ushirikiano wake wote na taifa hilo pekee lililobaki kwa nchi za magharibi ya Afrika lililokuwa na ushirikiano nao baada ya mataifa mengine jirani kuamua kuachana na kupangiwa mambo yao na mataifa hayo hasa ufaransa iliyokuwa mkoloni wao.
Miongoni mwa sababu zilizotolewa na viongozi wapya wa mapinduzi ya Niger zilizowapelekea kuamua kumuondosha raisi Bazoum ni kudorora kwa hali ya uchumi na hasa usalama hata pamoja na kuwepo vikosi vya Ufaransa nchini humo na ambapo raisi Bazoum alikuwa mshirika wao mkubwa.
Vikosi vya kijeshi vya Ufaransa baada ya kutimuliwa kutoka nchi za Mali,Chad na Burkinafaso vilihamishia shughuli zake nchi humo na kwa Upande wa Marekani ina kituo chake kikubwa cha kuongoza droni za kupambana na wale inaowaita wapiganaji wa ISIS wenye mfungamano na Alqaeda chini ya tawi la Sahel.
1690697205089.png
 
Jamaa aliwambia ECOWAS hawana msaada, viongozi wetu wametekwa kifikra, Afrika tumekuwa kama watoto yatima, tunakuwa na akili timamu pindi tukiwa watu wa kawaida, tukipewa tu kijiti cha uongozi tunasahau rasmi tulikotoka. Afrika inahitaji ukombozi wa kifikra kwanza.
 
Hako kanchi kana upuuzi mwingi sana, wao ni kupinduana tu, Mapinduzi ya 4 ya kijeshi yaliyofanikiwa na majaribio ya mapinduzi mengi. Makundi ya kigaidi na sasa mamluki wa Wagner nao wameingia huko ni vurugu tupu
Itakuwa wameona ni vurugu tu na hao magaidi hawawaoni wako wapi.
 
Jamaa aliwambia ECOWAS hawana msaada, viongozi wetu wametekwa kifikra, Afrika tumekuwa kama watoto yatima, tunakuwa na akili timamu pindi tukiwa watu wa kawaida, tukipewa tu kijiti cha uongozi tunasahau rasmi tulikotoka. Afrika inahitaji ukombozi wa kifikra kwanza.
Wamepinduana mara 4 na kila anayefanya mapinduzi anakuwa mbovu kuliko aliyepinduliwa.
 
Wamepinduana mara 4 na kila anayefanya mapinduzi anakuwa mbovu kuliko aliyepinduliwa.
Na haya mpinduzi enzi hizi yako huko Afrika magharibi tu.hakuna mapinduzi Ulaya.
 
Hako kanchi kana upuuzi mwingi sana, wao ni kupinduana tu, Mapinduzi ya 4 ya kijeshi yaliyofanikiwa na majaribio ya mapinduzi mengi. Makundi ya kigaidi na sasa mamluki wa Wagner nao wameingia huko ni vurugu tupu
Hakuna nchi hapo ni wahuni tupu
 
Hako kanchi kana upuuzi mwingi sana, wao ni kupinduana tu, Mapinduzi ya 4 ya kijeshi yaliyofanikiwa na majaribio ya mapinduzi mengi. Makundi ya kigaidi na sasa mamluki wa Wagner nao wameingia huko ni vurugu tupu
Nchi zote zilizokua chini ya mfaransa ni mapinduzi na vurugu,suala kubwa ni nishati,Niger,car,Mali Kuna uranium,gas na dhahabu
 
Hako kanchi kana upuuzi mwingi sana, wao ni kupinduana tu, Mapinduzi ya 4 ya kijeshi yaliyofanikiwa na majaribio ya mapinduzi mengi. Makundi ya kigaidi na sasa mamluki wa Wagner nao wameingia huko ni vurugu tupu
Kama serikali iliyopo madaraka inafanya ujinga ujinga kama huu wa maccm, acha igeuzwe tuuu.
 
Nchi jirani na Niger zimeamua kuiunga mkono Niger dhidi ya vitisho vya ECOWAS. Ufaransa kuona hivyo imejua sasa hali si shwari tena kwao wanaondoka rasmi.
 
Wanataka kubadilisha mkoloni. Nahisi watamwita yule atakayewapa ngano.
 
Back
Top Bottom