Pre GE2025 DC wa Ilala na Mwijaku wasema kampeni ya 'Hala Bi Mkubwa' itanadi kazi zilizofanywa na Rais Samia

Pre GE2025 DC wa Ilala na Mwijaku wasema kampeni ya 'Hala Bi Mkubwa' itanadi kazi zilizofanywa na Rais Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

upupu255

Senior Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
119
Reaction score
144
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Dar es salaam Edward Mpogoloe amesema kampeni ya ‘Hala Bi Mkubwa” iliyoanzishwa na Mtangazaji Barton Mwemba maarufu Mwijaku itasaidia kunadi kazi nzuri zilizofanywa chini ya Uongozi wa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika uzinduzi wa Kampeni hiyo, Edward Mpogolo amesema Rais Samia ameyafanya mambo mengi katika Nchi ikiwemo Wilaya ya Ilala ambako amepeleka zaidi ya shilingi bilioni mia tatu kwa ajili ya shughuli za maendeleo "pia kwenye eneo la elimu amefanya makubwa kuna shule za gorofa, nani anayeweza kuwaambia kwamba Mh. Rais amefanya hayo ? niwaombe Viongozi wenzangu huko Mwijaku anakokuja tumpe ushirikiano wa kutosha, tumpe data"

 
Baada ya Steve Nyerere, Baba Levo, Shilole, Shafii Dauda na wengine kuja na mambo ya Ajabu kuhusu Mama, sasa ni zamu ya Mwijaku.

Ambaye yeye kaamua kuja na mambo yasiyoeleweka kabisa

Screenshot_2025-02-18-14-00-15-1.png


Ila kwa vile katumia jina la Mama basi bila shaka atapiga hela za kutosha tu.

Tunamtakia kila la heri.
 
Baada ya Steve Nyerere, Baba Levo, Shilole, Shafii Dauda na wengine kuja na mambo ya Ajabu kuhusu Mama, sasa ni zamu ya Mwijaku.

Ambaye yeye kaamua kuja na mambo yasiyoeleweka kabisa

View attachment 3240778

Ila kwa vile katumia jina la Mama basi bila shaka atapiga hela za kutosha tu.

Tunamtakia kila la heri.
Wameiba sana hela kupitia 10% - 20% za miradi ya Serikali. Sasaivi wanapesa za kumwaga kufanya upuuzi wao wakati wananchi hawana maji na madawa hospitali.
 
Kwahiyo Mwijaku ataenda Namanyele huko kuwaambia kua Samia kajenga shule Shule ya Ghorofa iliyopo ILALA!!

Kwan Jamii inayoizunguka hiyo shule ,hawaioni ??
 
Huyu DC ni kilaza, eti amejenga shule za gorofa! Mshamba sana! Hela ni yake? Nchi hii watu wana laana sana!
Unaweza kukuta huyo DC ndo vijana walioingizwa kwenye system na CCM ili washike madaraka.

Sasa unajiuliza kama mtu ana akili za namna hii nchi yetu itakuwa salama dhidi ya maadui wa ndani na nje?
 
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Dar es salaam Edward Mpogoloe amesema kampeni ya ‘Hala Bi Mkubwa” iliyoanzishwa na Mtangazaji Barton Mwemba maarufu Mwijaku itasaidia kunadi kazi nzuri zilizofanywa chini ya Uongozi wa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika uzinduzi wa Kampeni hiyo, Edward Mpogolo amesema Rais Samia ameyafanya mambo mengi katika Nchi ikiwemo Wilaya ya Ilala ambako amepeleka zaidi ya shilingi bilioni mia tatu kwa ajili ya shughuli za maendeleo "pia kwenye eneo la elimu amefanya makubwa kuna shule za gorofa, nani anayeweza kuwaambia kwamba Mh. Rais amefanya hayo ? niwaombe Viongozi wenzangu huko Mwijaku anakokuja tumpe ushirikiano wa kutosha, tumpe data"

Kunadi kazi nzuri ya. . . .
Kinachonadiwa n kitu kisichojitoaheleza au sijaelewa ile methali inasema
Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza. Yaani kujitembeza ndio kwenda kujinadi huko ila kizuri kinajinadinchenyewe hapo kilipo
 
Issue hapo ni nani mkali wa kutengeneza madili kati ya ‘babalevo’ na ‘Mwijaku’ hayo mengine hatutaki kusikia.

Inabidi ianzishwe poll ya nani mkali kati ya hawa miamba miwili kwenye uchawa sijui social influencers.

Huko kwenye siasa tushakubali matokeo tumepigwa, Meya na team nzima waliwai safiri na team nzima mara tu baada ya Samia kuapishwa kwenda U.K. kwa sababu za kijinga na kufikia hotel ya 5 star (Marble Arch) London? kwa hivyo atushangai kusifia.

Issue ni nani mkali kati ya machawa tunahitaji poll.
 
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Dar es salaam Edward Mpogoloe amesema kampeni ya ‘Hala Bi Mkubwa” iliyoanzishwa na Mtangazaji Barton Mwemba maarufu Mwijaku itasaidia kunadi kazi nzuri zilizofanywa chini ya Uongozi wa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika uzinduzi wa Kampeni hiyo, Edward Mpogolo amesema Rais Samia ameyafanya mambo mengi katika Nchi ikiwemo Wilaya ya Ilala ambako amepeleka zaidi ya shilingi bilioni mia tatu kwa ajili ya shughuli za maendeleo "pia kwenye eneo la elimu amefanya makubwa kuna shule za gorofa, nani anayeweza kuwaambia kwamba Mh. Rais amefanya hayo ? niwaombe Viongozi wenzangu huko Mwijaku anakokuja tumpe ushirikiano wa kutosha, tumpe data"

Hizo kazi hazionekani mpaka huyu mdudu aje kuzinadi?
 
Back
Top Bottom