Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,478
- 3,659
Nimeangalia chanel 10 muda si mrefu, sijui kipindi walikiitaje. Ila nimeona wakazi wa moshi vijijini wakijitokeza kwa wingi sana wakati jk akihutubia. Pale uwanja wa mashujaa hadi mwenyewe kashangaa umati. Sasa najiuliza hawa wameku wenzangu inakuwaje? Nawauliza hao, mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo? Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Jueni watu wenye mavazi ya utukufu (wasio mafisadi), wanaokula raha wamo katika majumba ya kifalme (nyoyo safi). Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Nabii...? Mjipange upya. Yawezekana mlienda kumuona rais anayemaliza muda wake, ambaye mengi yamesemwa juu yake na kutokea juu yake. Bado sijajua uhusiano wa nyie kumwona na kilele cha uchaguzi mkuu