DOKEZO Inadaiwa Wananchi wa Kata ya Uyui kuwa hawajawahi kupata maji ya Bomba tangu Nchi ipate uhuru

DOKEZO Inadaiwa Wananchi wa Kata ya Uyui kuwa hawajawahi kupata maji ya Bomba tangu Nchi ipate uhuru

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
DSC_0520.MOV.00_00_01_11.Still001.jpg

DSC_0497.MOV.00_00_03_11.Still001.jpg
Wanajamvi Kata ya Uyui inapatikana kwenye Manispaa na Mkoa wa Tabora ambapo maajabu ya kata hiyo imekuwa ikikosa huduma muhimu kama Shule ya Kata, Zahanati, barabara pamoja na umeme kwa muda mrefu katika baadhi ya maeneo.

Nimefikia eneo hilo na katika stori na wenyeji wanadai tangu nchi ipate uhuru kata hiyo haijapata maji safi na salama jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

Kwenye kuzunguka kata hiyo nilifanikiwa kukutana na Wanawake kadhaa wanaopata kadhia ya kukosa maji safi na salama ambapo kwenye kuzungumza nao walidai ya kwamba changamoto ya maji katika kata yao imekuwa kubwa na nilizungumza na wanawake waishio Kijiji cha Imalamihayo ambao walielezea mengi.

Mkazi wa Kijiji cha Imalamihayo, Rehema Simon yeye alisema wanashangazwa na kitendo cha kukosa maji wakati Bomba kubwa linalosambaza maji Tabora likitokea mradi mkubwa wa maji Ziwa Victoria linapita kwenye kiji hicho.

“Kijiji chetu hiki hatujawahi kupata maji ya bomba tangu nchi yetu ipate uhuru, kinachonishangaza ni kwamba bomba la maji kutoka Mwanza linapita kijijini kwetu lakini hatupati maji safi na salama hivyo Serikali tunaiomba iangalie swala hili na ione namna ya itusaidie,” anasema.
DSC_0509.MOV.00_00_06_13.Still002.jpg

DSC_0511.MOV.00_00_02_15.Still001.jpg
Rehema anaongeza kuwa kutokana na wao kukosa maji, Wanawake wa kijiji hicho wamekuwa wakiamka usiku wa manane kutembeza zaidi ya Kilometa saba kufuata maji kwenye kisima kilichopo jirani na kijiji chao.

Wanaeleza kuwa barabarani kumekuwa hakuna usalama, mapori ya kutisha lakini kwa kuwa shida yao ni maji wamekuwa wakitembea usiku kufuata maji ili shughuli zingine zifanyike na ndio maisha yao ya kila siku.

Juma Said, mkazi wa Kata ya Uyui anasema Wanawake kwenye kata hiyo wanateseka maana hutembea umbali mrefu zaidi.

Anasema “Kata yetu hii kabila kubwa hapa ni Wasukuma na Kimila Wasukuma huacha shughuli zote kwa Wanawake, sasa apike, afue, alime n.k kiukweli Wanawake wanateseka na kukosekana kwa maji kwenye eneo hili.

“Mbaya zaidi ni kwamba Wanawake wanatumia muda mrefu kufuata maji, hivyo iko haja kwa Serikali kufuatilia na kutusaidia maji kwenye eneo letu hili.”

Watoto nao huathirika na ukosefu wa maji safi na salama.

Kuna wakati Wanawake wanalazimika kuwachukua Watoto wakachote maji, hatua hiyo imekuwa ikiwafanya wengi wao kuchelewa kufika shule na wakati mwingine wanakosa masomo kutokana na kuamka kwenda kuchota maji, wakirejea nyumbani wanajikuta wamechelewa, hivyo kuamua kutokwenda shule.

Wanafanya hivyo kwa kuwa wakichelewa wanaweza kukumbana na adhabu mbalimbali kutoka kwa waalimu wao.

MAMLAKA ZINASEMAJE?
Uchunguzi ambao niliufanya nilibaini ya kwamba Kijiji cha Imalamihayo kina vitongoji 20 ambavyo vinatakiwa kupata maji lakini kati ya vijiji hivyo ni viwili tu ambavyo vimejengwa magati kwa ajili ya kusambazia maji lakini hayajafika, hivyo Wananchi hawawezi kupata maji.

Hata hivyo, Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Tabora imeshafuatwa na wawakilishi wa vijiji hivyo mara kadhaa lakini kumekuwa hakuna ushirikiano wa kueleweka ambao angalau ungeweza kutoa mwangaza ni jinsi gai wananchi hao wangeweza kupata maji safi na salama kutokana na bomba kubwa la maji kutoka ziwa Victoria kupita kwenye kata yao huku wakiwa hawanufaiki na maji hayo.

Anachosema Diwani
Diwani wa Kata ya Uyui, Julius Nyanda anasema amejaribu kuzifikisha kwenye vikao vya Halmashauri bila majibu mahususi kutolewa jambo ambalo limewafanya wananchi hao kuendelea kuteseka kwa kukosa maji safi na salama.

Anaeleza kuwa hali hiyo inawafanya watumie maji ya visima ambayo wakati mwingine sio salama kwa kuwa yanakuwa hayajapimwa na wataalamu kuyathibitisha kama yanaweza kutumika na binadamu.

Maji yasiyo salama huweza kusababisa magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu na magonjwa mengine ya tumbo, Serikali ichukue hatua dhidi ya Wananchi hawa.

Pia soma: √ - Tabora: Kata ya Imalamihayo - Uyui maji yapo, bado gati moja katika kitongoji, kazi itakamilika Januari
DSC_0517.MOV.00_00_04_23.Still001.jpg
 
Wanajamvi Kata ya Uyui inapatikana kwenye Manispaa na Mkoa wa Tabora ambapo maajabu ya kata hiyo imekuwa ikikosa huduma muhimu kama Shule ya Kata, Zahanati, barabara pamoja na umeme kwa muda mrefu katika baadhi ya maeneo.

Nimefikia eneo hilo na katika stori na wenyeji wanadai tangu nchi ipate uhuru kata hiyo haijapata maji safi na salama jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

Kwenye kuzunguka kata hiyo nilifanikiwa kukutana na Wanawake kadhaa wanaopata kadhia ya kukosa maji safi na salama ambapo kwenye kuzungumza nao walidai ya kwamba changamoto ya maji katika kata yao imekuwa kubwa na nilizungumza na wanawake waishio Kijiji cha Imalamihayo ambao walielezea mengi.

Mkazi wa Kijiji cha Imalamihayo, Rehema Simon yeye alisema wanashangazwa na kitendo cha kukosa maji wakati Bomba kubwa linalosambaza maji Tabora likitokea mradi mkubwa wa maji Ziwa Victoria linapita kwenye kiji hicho.

“Kijiji chetu hiki hatujawahi kupata maji ya bomba tangu nchi yetu ipate uhuru, kinachonishangaza ni kwamba bomba la maji kutoka Mwanza linapita kijijini kwetu lakini hatupati maji safi na salama hivyo Serikali tunaiomba iangalie swala hili na ione namna ya itusaidie,” anasema.
Rehema anaongeza kuwa kutokana na wao kukosa maji, Wanawake wa kijiji hicho wamekuwa wakiamka usiku wa manane kutembeza zaidi ya Kilometa saba kufuata maji kwenye kisima kilichopo jirani na kijiji chao.

Wanaeleza kuwa barabarani kumekuwa hakuna usalama, mapori ya kutisha lakini kwa kuwa shida yao ni maji wamekuwa wakitembea usiku kufuata maji ili shughuli zingine zifanyike na ndio maisha yao ya kila siku.

Juma Said, mkazi wa Kata ya Uyui anasema Wanawake kwenye kata hiyo wanateseka maana hutembea umbali mrefu zaidi.

Anasema “Kata yetu hii kabila kubwa hapa ni Wasukuma na Kimila Wasukuma huacha shughuli zote kwa Wanawake, sasa apike, afue, alime n.k kiukweli Wanawake wanateseka na kukosekana kwa maji kwenye eneo hili.

“Mbaya zaidi ni kwamba Wanawake wanatumia muda mrefu kufuata maji, hivyo iko haja kwa Serikali kufuatilia na kutusaidia maji kwenye eneo letu hili.”

Watoto nao huathirika na ukosefu wa maji safi na salama.

Kuna wakati Wanawake wanalazimika kuwachukua Watoto wakachote maji, hatua hiyo imekuwa ikiwafanya wengi wao kuchelewa kufika shule na wakati mwingine wanakosa masomo kutokana na kuamka kwenda kuchota maji, wakirejea nyumbani wanajikuta wamechelewa, hivyo kuamua kutokwenda shule.

Wanafanya hivyo kwa kuwa wakichelewa wanaweza kukumbana na adhabu mbalimbali kutoka kwa waalimu wao.

MAMLAKA ZINASEMAJE?
Uchunguzi ambao niliufanya nilibaini ya kwamba Kijiji cha Imalamihayo kina vitongoji 20 ambavyo vinatakiwa kupata maji lakini kati ya vijiji hivyo ni viwili tu ambavyo vimejengwa magati kwa ajili ya kusambazia maji lakini hayajafika, hivyo Wananchi hawawezi kupata maji.

Hata hivyo, Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Tabora imeshafuatwa na wawakilishi wa vijiji hivyo mara kadhaa lakini kumekuwa hakuna ushirikiano wa kueleweka ambao angalau ungeweza kutoa mwangaza ni jinsi gai wananchi hao wangeweza kupata maji safi na salama kutokana na bomba kubwa la maji kutoka ziwa Victoria kupita kwenye kata yao huku wakiwa hawanufaiki na maji hayo.

Anachosema Diwani
Diwani wa Kata ya Uyui, Julius Nyanda anasema amejaribu kuzifikisha kwenye vikao vya Halmashauri bila majibu mahususi kutolewa jambo ambalo limewafanya wananchi hao kuendelea kuteseka kwa kukosa maji safi na salama.

Anaeleza kuwa hali hiyo inawafanya watumie maji ya visima ambayo wakati mwingine sio salama kwa kuwa yanakuwa hayajapimwa na wataalamu kuyathibitisha kama yanaweza kutumika na binadamu.

Maji yasiyo salama huweza kusababisa magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu na magonjwa mengine ya tumbo, Serikali ichukue hatua dhidi ya Wananchi hawa.
Ninakumbuka Uyui ndiyo iliyokuwa na shule pekee ya viziwi tangu kabla ya Uhuru.
 
Watumie vema kipindi hiki kabla ya uchaguzi wapate majibu ya uhakika.
Sasa hivi wasaka vyeo wanaweza kufikisha maji kila kona hata ndani ya siku mbili. Achana na madaraka kabisa...
 
Nimeishi pale uyui takribani miezi sita hivi,

Ni kweli kabisa maji ya bomba pale ni changamoto sana, maji yapo tu maeneo ya ofisi/nyumba za viongozi, ila wakazi wa pale ni mwendo wa kwenda visimani tu....
 
Wanajamvi Kata ya Uyui inapatikana kwenye Manispaa na Mkoa wa Tabora ambapo maajabu ya kata hiyo imekuwa ikikosa huduma muhimu kama Shule ya Kata, Zahanati, barabara pamoja na umeme kwa muda mrefu katika baadhi ya maeneo.

Nimefikia eneo hilo na katika stori na wenyeji wanadai tangu nchi ipate uhuru kata hiyo haijapata maji safi na salama jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

Kwenye kuzunguka kata hiyo nilifanikiwa kukutana na Wanawake kadhaa wanaopata kadhia ya kukosa maji safi na salama ambapo kwenye kuzungumza nao walidai ya kwamba changamoto ya maji katika kata yao imekuwa kubwa na nilizungumza na wanawake waishio Kijiji cha Imalamihayo ambao walielezea mengi.

Mkazi wa Kijiji cha Imalamihayo, Rehema Simon yeye alisema wanashangazwa na kitendo cha kukosa maji wakati Bomba kubwa linalosambaza maji Tabora likitokea mradi mkubwa wa maji Ziwa Victoria linapita kwenye kiji hicho.

“Kijiji chetu hiki hatujawahi kupata maji ya bomba tangu nchi yetu ipate uhuru, kinachonishangaza ni kwamba bomba la maji kutoka Mwanza linapita kijijini kwetu lakini hatupati maji safi na salama hivyo Serikali tunaiomba iangalie swala hili na ione namna ya itusaidie,” anasema.
Rehema anaongeza kuwa kutokana na wao kukosa maji, Wanawake wa kijiji hicho wamekuwa wakiamka usiku wa manane kutembeza zaidi ya Kilometa saba kufuata maji kwenye kisima kilichopo jirani na kijiji chao.

Wanaeleza kuwa barabarani kumekuwa hakuna usalama, mapori ya kutisha lakini kwa kuwa shida yao ni maji wamekuwa wakitembea usiku kufuata maji ili shughuli zingine zifanyike na ndio maisha yao ya kila siku.

Juma Said, mkazi wa Kata ya Uyui anasema Wanawake kwenye kata hiyo wanateseka maana hutembea umbali mrefu zaidi.

Anasema “Kata yetu hii kabila kubwa hapa ni Wasukuma na Kimila Wasukuma huacha shughuli zote kwa Wanawake, sasa apike, afue, alime n.k kiukweli Wanawake wanateseka na kukosekana kwa maji kwenye eneo hili.

“Mbaya zaidi ni kwamba Wanawake wanatumia muda mrefu kufuata maji, hivyo iko haja kwa Serikali kufuatilia na kutusaidia maji kwenye eneo letu hili.”

Watoto nao huathirika na ukosefu wa maji safi na salama.

Kuna wakati Wanawake wanalazimika kuwachukua Watoto wakachote maji, hatua hiyo imekuwa ikiwafanya wengi wao kuchelewa kufika shule na wakati mwingine wanakosa masomo kutokana na kuamka kwenda kuchota maji, wakirejea nyumbani wanajikuta wamechelewa, hivyo kuamua kutokwenda shule.

Wanafanya hivyo kwa kuwa wakichelewa wanaweza kukumbana na adhabu mbalimbali kutoka kwa waalimu wao.

MAMLAKA ZINASEMAJE?
Uchunguzi ambao niliufanya nilibaini ya kwamba Kijiji cha Imalamihayo kina vitongoji 20 ambavyo vinatakiwa kupata maji lakini kati ya vijiji hivyo ni viwili tu ambavyo vimejengwa magati kwa ajili ya kusambazia maji lakini hayajafika, hivyo Wananchi hawawezi kupata maji.

Hata hivyo, Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Tabora imeshafuatwa na wawakilishi wa vijiji hivyo mara kadhaa lakini kumekuwa hakuna ushirikiano wa kueleweka ambao angalau ungeweza kutoa mwangaza ni jinsi gai wananchi hao wangeweza kupata maji safi na salama kutokana na bomba kubwa la maji kutoka ziwa Victoria kupita kwenye kata yao huku wakiwa hawanufaiki na maji hayo.

Anachosema Diwani
Diwani wa Kata ya Uyui, Julius Nyanda anasema amejaribu kuzifikisha kwenye vikao vya Halmashauri bila majibu mahususi kutolewa jambo ambalo limewafanya wananchi hao kuendelea kuteseka kwa kukosa maji safi na salama.

Anaeleza kuwa hali hiyo inawafanya watumie maji ya visima ambayo wakati mwingine sio salama kwa kuwa yanakuwa hayajapimwa na wataalamu kuyathibitisha kama yanaweza kutumika na binadamu.

Maji yasiyo salama huweza kusababisa magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu na magonjwa mengine ya tumbo, Serikali ichukue hatua dhidi ya Wananchi hawa.
KATA YA IMALAMIHAYO-UYUI MAJI YAPO, BADO GATI MOJA KATIKA KITONGOJI CHA KAZI ITAKAMILIKA JANUARY 2025

Manispaa ya Tabora ni moja ya maeneo ambayo imeshafikiwa na maji kutoka ziwa Victoria.
Manispaa ina Kata 29 ikijumuisha Kata ya Uyui. Kata zote 29 zimeshafikiwa na huduma ya maji.
Kata ya Uyui ambamo kijiji cha Imalamihayo kimo ina jumla ya magati 14 ambapo, magati 13 yanatoa maji na Gati moja (1) lipo kwenye hatua ya kukamilishwa kufungiwa Bomba.

Kijiji/Mtaa wa Imalamihayo pekee kina magati matatu (3).
Magati mawili (2) yana maji na Gati moja (1) liko kwenye mradi unaoendelea wa kulaza Bomba kufikia eneo hilo.

Wizara ya Maji kupitia Mamlaka ya majisafi na Usafi wa Mazingira Tabora (TUWASA) inatarajia kukamilisha mradi huo mapema mwezi Januari, 2025. Aidha, ikumbukwe wizara inatekeleza mpango kabambe wa Gridi ya Maji ya Taifa, na inapata sapoti kubwa kwa viongozi na wadau wa maendeleo, ni maendeleo kwa wananchi wote nchini.
 

Attachments

  • uyui.jpeg
    uyui.jpeg
    63.8 KB · Views: 4
Wanajamvi Kata ya Uyui inapatikana kwenye Manispaa na Mkoa wa Tabora ambapo maajabu ya kata hiyo imekuwa ikikosa huduma muhimu kama Shule ya Kata, Zahanati, barabara pamoja na umeme kwa muda mrefu katika baadhi ya maeneo.

Nimefikia eneo hilo na katika stori na wenyeji wanadai tangu nchi ipate uhuru kata hiyo haijapata maji safi na salama jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

Kwenye kuzunguka kata hiyo nilifanikiwa kukutana na Wanawake kadhaa wanaopata kadhia ya kukosa maji safi na salama ambapo kwenye kuzungumza nao walidai ya kwamba changamoto ya maji katika kata yao imekuwa kubwa na nilizungumza na wanawake waishio Kijiji cha Imalamihayo ambao walielezea mengi.

Mkazi wa Kijiji cha Imalamihayo, Rehema Simon yeye alisema wanashangazwa na kitendo cha kukosa maji wakati Bomba kubwa linalosambaza maji Tabora likitokea mradi mkubwa wa maji Ziwa Victoria linapita kwenye kiji hicho.

“Kijiji chetu hiki hatujawahi kupata maji ya bomba tangu nchi yetu ipate uhuru, kinachonishangaza ni kwamba bomba la maji kutoka Mwanza linapita kijijini kwetu lakini hatupati maji safi na salama hivyo Serikali tunaiomba iangalie swala hili na ione namna ya itusaidie,” anasema.
Rehema anaongeza kuwa kutokana na wao kukosa maji, Wanawake wa kijiji hicho wamekuwa wakiamka usiku wa manane kutembeza zaidi ya Kilometa saba kufuata maji kwenye kisima kilichopo jirani na kijiji chao.

Wanaeleza kuwa barabarani kumekuwa hakuna usalama, mapori ya kutisha lakini kwa kuwa shida yao ni maji wamekuwa wakitembea usiku kufuata maji ili shughuli zingine zifanyike na ndio maisha yao ya kila siku.

Juma Said, mkazi wa Kata ya Uyui anasema Wanawake kwenye kata hiyo wanateseka maana hutembea umbali mrefu zaidi.

Anasema “Kata yetu hii kabila kubwa hapa ni Wasukuma na Kimila Wasukuma huacha shughuli zote kwa Wanawake, sasa apike, afue, alime n.k kiukweli Wanawake wanateseka na kukosekana kwa maji kwenye eneo hili.

“Mbaya zaidi ni kwamba Wanawake wanatumia muda mrefu kufuata maji, hivyo iko haja kwa Serikali kufuatilia na kutusaidia maji kwenye eneo letu hili.”

Watoto nao huathirika na ukosefu wa maji safi na salama.

Kuna wakati Wanawake wanalazimika kuwachukua Watoto wakachote maji, hatua hiyo imekuwa ikiwafanya wengi wao kuchelewa kufika shule na wakati mwingine wanakosa masomo kutokana na kuamka kwenda kuchota maji, wakirejea nyumbani wanajikuta wamechelewa, hivyo kuamua kutokwenda shule.

Wanafanya hivyo kwa kuwa wakichelewa wanaweza kukumbana na adhabu mbalimbali kutoka kwa waalimu wao.

MAMLAKA ZINASEMAJE?
Uchunguzi ambao niliufanya nilibaini ya kwamba Kijiji cha Imalamihayo kina vitongoji 20 ambavyo vinatakiwa kupata maji lakini kati ya vijiji hivyo ni viwili tu ambavyo vimejengwa magati kwa ajili ya kusambazia maji lakini hayajafika, hivyo Wananchi hawawezi kupata maji.

Hata hivyo, Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Tabora imeshafuatwa na wawakilishi wa vijiji hivyo mara kadhaa lakini kumekuwa hakuna ushirikiano wa kueleweka ambao angalau ungeweza kutoa mwangaza ni jinsi gai wananchi hao wangeweza kupata maji safi na salama kutokana na bomba kubwa la maji kutoka ziwa Victoria kupita kwenye kata yao huku wakiwa hawanufaiki na maji hayo.

Anachosema Diwani
Diwani wa Kata ya Uyui, Julius Nyanda anasema amejaribu kuzifikisha kwenye vikao vya Halmashauri bila majibu mahususi kutolewa jambo ambalo limewafanya wananchi hao kuendelea kuteseka kwa kukosa maji safi na salama.

Anaeleza kuwa hali hiyo inawafanya watumie maji ya visima ambayo wakati mwingine sio salama kwa kuwa yanakuwa hayajapimwa na wataalamu kuyathibitisha kama yanaweza kutumika na binadamu.

Maji yasiyo salama huweza kusababisa magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu na magonjwa mengine ya tumbo, Serikali ichukue hatua dhidi ya Wananchi hawa.
UPINZANI NDO TATIZO.
 
Back
Top Bottom