Inafikirisha sana kuwa Serikali ilihitaji msaada wa TIGO kujua Lissu alipo

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825
Hoja inajegwa hapa kuwa TIGO ilifatilia na kuisaidia serikali kujua uelekeo na mahali Mh. Lissu alipokuwa.

Wakati Lissu amajenga hoja kuwa alishambuliwa akiwa mbuge, wakati wa vikao vya bunge, kwenye makazi ya viongozi waandamizi wa serikali.

Aidha wote tunajua kuwa baada ya Lissu kushabuliwa alipelekwa hospital na viongozi wa serikali, akapewa huduma ya kwanza na ya uokozi na madaktari wa serikali.

PIA SOMA
- Kupigwa risasi kwa Tundu Lissu: Kampuni ya simu ya Tigo yadaiwa ilivujisha mawasiliano yake kwa mamlaka
 
Aidha wote tunajua kuwa baada ya Lissu kushabuliwa alipelekwa hospital na viongozi wa serikali
🚮 🚮
Uongo,
Ni kwa nini wale waliokusanyika kumuombea kwa Mungu ili apone walikamatwa na policcm?

 
Hakuwa mgonjwa- nasema kuombea mgonjwa apone ni ujuha- nyinyi chadema kwani ni majuha?
 
Kwahiyo??? Unabishana na mahakama ya mzungu au?
Kwamba ilikua haijulikani yupo bungeni? Muda wa kuisha kikao? Gari yake pia ilikua haijulikani?

Hii story nadhani pengine ilikua na maana nyingine si hivi ambavyo tumeletewa. Lissu yupo bungeni wote wanaona, gari yake inajulikana, anapoishi panajulikana. Sasa hapo tigo inaingiaje?
 
Wamiliki wa tigo naona mmekuja kwa kasi. Si muwaache wajitete wenyewe huko London hapa hata judge wa His Majest the court of London hakusomi
 
Unaona akili yako ilivyo?...ndio maana ulikimbiwa bwashee....
Sema kwa uwezo wako huwezi kuelewa kilichoandikwa kwenye ile taarifa.
 
Waulize mahakama ya wazungu.
 
Hakuanza kufuatilia akiwa Dom. Alishatoa angalizo akiwa Dar juu ya gari kufuata kila aendapo. Labda upenyo wa kumshambulia haukupatikana kote huko ila Dom.
 
Hata walinzi ambao waliokuwa hawatumii silaha, (bunduki), waliondolewa kwenye eneo la tukio, aliye waondoa na kuwapangia zamu hajulikani pia
 
Hakuanza kufuatilia akiwa Dom. Alishatoa angalizo akiwa Dar juu ya gari kufuata kila aendapo. Labda upenyo wa kumshambulia haukupatikana kote huko ila Dom.
Tigo wanahusika vipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…