Kukua kwa uchumi (kama kunavyoshabikiwa na wachumi wa economic development kama world bank na IMF) kunapimwa na GDP, ongezeko la pato la taifa linaloakisi uzalishaji. Sasa kukua kwa uzalishaji hakuna uwiano wa moja kwa moja na mgawanyo sawa wa kilichozalishwa na wala hakuna uwiano wa moja kwa moja wa jinsi uzalishaji ulivyotokea katika population husika.
Kwa maana hiyo basi, GDP ikiongezeka aina maana kwamba moja kwa moja mwananchi amenufaika. Kadhalika upo uwezekano kwamba ni sekta chache tu ndio zimesababisha ongezeko hilo.
Wana uchumi wa development economics wao kwa kuondoa mkanganyiko huu wa kukua kwa GDP bila maendeleo ya watu, wakaja na vipimo tofauti vya maendeleo kama vile human development index, social index, human needs index, etc). Udhaifu wa vipimo hivi vya maendeleo ni kwamba vinapima matokeo tu ya zao la shughuli za uchumi bila kueleza jinsi ya kufikia au kupata zao hilo.
Mwisho wa siku, GDP ingawa haionyeshi uwiano wa moja kwa moja wa maendeleo ya watu ni kipimo pekee kinachoonyesha kukua kwa shughuli za kiuchumi katika nchi. Vipimo vingine vinapima matokeo tu ya kukua kwa GDP.
So kwanini kukua kwa uchumi kupitia GDP akuwiani na maendeleo ya watu? Jibu lake ni kwamba GDP inapima kukua kwa uchumi tu na sio maendeleo ya watu. Assumption isiyopingika ni kwamba GDP lazima ikuwe ndipo watu waendelee, lakini sio kila GDP inapokuwa basi watu wanaendelea; kwasababu GDP haina uhusiano wa moja kwa moja na maendeleo ya watu.