Nilibahatika kutembelea nchi fulani za Magharibi. Maduka yanayouza vitu vya ngono ni sehemu wanayoingia watu wazima tu.
Nikashanga nilipokuta siku hizi, hata sigara zinafungiwa kwenye makabati na hazionekani na ukitaka sigara lazima wakinahi kuwa u mtu mzima ndio wakuuzie. Hata vinywaji vikali maduka yake tofauti hata supermarket hukuti vinywaji vikali vimeanikwa, mpaka uende maduka ya vinywaji na uwe umefikia umri wa kuingia humo.
Hapa kwetu hata bar utakuta watu wanaingia na watoto wadogo, utakuta mtu anampa mwanae beer, tana huku anajisifu "huyu anakunywa chupa nzima ya bia".
Usione tunavaa tai na makoti makubwa na tunaendesha magari ya mitumba ukafikiri Watanzania ni watu wa maana na wameendelea, hizo ni "cosmetics" na hazibadilishi mawazo na fikra za mtu. Hatuna maana hata kidogo, bado tuko nyuma sana kwa kila kitu chetu, na hii inatokana na kuwa elimu ya madarasani pekee haitoshi. Inabidi tubadilishwe "genetically" namna tunavyofikiri.