Inakuwaje wanafunzi warudishwe nyumbani kwa kutokuwa na saa za mkononi ?

Ng'wanza Madaso

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2008
Posts
2,268
Reaction score
335
Ndugu wana jamvi,

Kuna mtoto wangu na wanafunzi wengine wamerudishwa nyumbani kwa kuwa hawakuwa na saa za mkononi na viatu vya kufunga, mimi kama mzazi imeniuma sana hasa hili la saa ya mkononi, na kuna michango inayofikia kiasi cha sh 150,00.

Kuna baadhi unalipia Bank na zingine unalipia shuleni.Kuna mchango wa tuition sh20,000 ni wa lazima hata kama mtoto hasomi hiyo Tuition.

Wana jamvi naombeni msaada wenu ni wapi nikalalamike na kama kuna mtu ana contact za kitengo maalum wizara ya Elimu anipatie niwasiliane nao.

Asanteni.
 
Niko mbali kidogo kikazi, nikamwagiza mdogo wangu aende pale shule akaambiwa bila hivyo mtoto hatapokelewa shuleni na yuko kidato cha nne.
 
Ingekuwa vema kama ungetutajia jina la shule husika and or if it is a government or private school, lakini pia utoe mchanganuo wa hiyo michango inayofikia 150,000/=
 
Ingekuwa vema kama ungetutajia jina la shule husika and or if it is a government or private school, lakini pia utoe mchanganuo wa hiyo michango inayofikia 150,000/=
Nyasaka Secondary school iliyopo wilayani Magu Mkoa wa Mwanza, ni shule ya Serikali.
 
Nenda shuleni ukaeleweshwe vizur ndugu kuhusu mchanganuo wa hiyo michango pamoja na matumizi ya msingi ya hiyo saa jazba za kupiga cm wizarani na nini siyo uamuzi wa busara na hawatakusaidia chochote.
 
kwa hili la saa naunga mkono hoja.

Ushauri.. omba Mungu aondoe ulimi wa kulalamika kinywani mwako.
 
Nenda shuleni ukaeleweshwe vizur ndugu kuhusu mchanganuo wa hiyo michango pamoja na matumizi ya msingi ya hiyo saa jazba za kupiga cm wizarani na nini siyo uamuzi wa busara na hawatakusaidia chochote.
Mkuu hapa tatizo ni kuwarudisha nyumbani watoto kwa kukosa hizo saa na kumbuka huko ni kijijini na kuna wazazi wengine hawana huo uwezo.
 
kuanzia mwakani elimu bure shule ya msingi na sekondari vumilia mwakani siyo mbali
 
Try to be specific, I know that school, iko ilemela na sio vijijini, abt saa na mengine ni muhim mzaz kwenda shule kujua.tatizo letu wazaz wa kizaz hik tunapeleka watot wetu shule then tunakaa kusubir matokeo mazur, without knowing how this can happen
 
Am sure huyu jamaa anahudumia mtoto so ye anapewa taarifa tu na mtoto au walezi na kwa kuwa wanataka cha juu baso ndo kama hivo tena coz hata hajui wilaya aliyo mwanae? How come? Utajuaje mengine? Jipange kama unayo toa tu
 
Mwanangu yuko Darasa la Tano. Saa ya Mkononi ni sehemu ya mavazi yake. Sio kwa ajili ya maandalizi ya Mitihani ya Kidato cha Nne kama ambavyo Mwanao anashurutishwa avae, bali ni kumjengea Mtoto hurka ya "Time Management" tangu akiwa mtoto, jambo ambalo kwa Watanzania ni "Janga la Taifa"! Suala la Mwanao kuwa na Saa ya Mkononi, hasa akiwa amebakiza miezi kadhaa afanye Mitihani ya Taifa sio la kulalamikia.

Viatu vya kufunga? Nadhani ni suala la Sare. Kama Sare za Shule hiyo ni pamoja na Viatu vya aina hiyo, unalalamika nini?

Acha kulalamika, fanya kazi, ongeza kipato, mjali Mwanao. Makoroboi, Mwanza, Saa nzuri ya Mkononi, digital, durable, dual powered for both solar and battery, shock and water resistant, etc. ni Sh. 10,000/- - 15,000/-. Viatu vya Mitumba vimetapakaa Mwanza nzima, mpaka vinatembezwa Baa, pure reather, ni Sh. 10,000/- - 25,000/-! (Angalizo: kwa ulalamishi uliona nao usijaribu Mlango Mmoja)!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…