Wakuu mu hali gani huko mlipo ? Poleni wooote wa mabondeni kwa mvua, hongereni wakulima kwa mvua na wale wooote wanaotafuta uzao hakika hali ya hewa inapendeza. Basi turudi kunako jamvi letu. Kuzungumza lugha moja bila kuchanganya na nyingine inapendeza sana lakini kuna wakati inaleta mfadhaiko.
Nitatoa mfano ili na sisi tusonge nayo.
Nilikuwa na DRIVE sasa ukijiona mswahili mzuri ukasema kwa kiswahili hakika utapewa pole. Watu watajua unaumwa.
Ebu na sisi tufunguke maneno yaliyo na utata....