Inasemekana Jonas Mkude kasinya kandarasi mwaka mmoja

ana impact kubwa sana, na kwasababu simba mlimtupilia mbali, atafanya juu chini ili awaonyeshe kwamba mlifanya makosa. though kwasababu amekuwa simba muda mrefu ni rahisi kurubuniwa ili asikaze.
 
Tunamtakia kila la kheri hatuna deni naye
 
sijawaelewa yanga kumsaini mkude,hivi umri wake nani anaujua?
 
Aina ya uchezaji wa Mkude anafaa tu pale timu pinzani inapopaki basi. Hapo utamuona Mkude bonge la kiungo kwani ni mpigaji pasi mzuri sana hakuna mfano. Lakini siku akikutana na timu inayopeleka moto mwanzo mwisho utamkataa Mkude kwa sababu kwanza hana kasi na pili hajui kukaba kabisa zaidi atacheza rafu hatarishi kwa timu yake.Ili.

Ili umfaidi Mkude we mwekee tu mtu anayejua kukaba basi utafurahi. Pale Simba kuna wakati alikuwa wa moto lakini watu walikuwa hawajui kuwa alikuwa anakabiwa na Fraga na wakati mwingine Tadeo Lwanga. Ukimuacha mwenyewe acheze kama kiungo mkabaji kulinda "back four" anakuwa sawa na kifaranga cha kuku kilichotelekezwa na mama yake.
 
Kutokana na uhaba wa wachezaji wa ndani wenye ubora na uzoefu wa mechi za ndani na zile za Kimataifa, sitashangaa hiyo taarifa ikiwa na ukweli ndani yake.
 
Una shida na mkude?
 
Nafikir Simba walimuacha kisa sio kiwango bali tabia.

Akibadili tabia ataitwa hadi ya taifa.

Jamaa anajua sema hajitambui tu.
 
Jamaa una uchambuzi ule wa kimtaa mtaa yaani wa kwenye vijiwe vya kahawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…