Inasikitisha sana kuona mchina Juma Sharobaro anakijali na kukithamini kiswahili kuliko sisi wazawa

Inasikitisha sana kuona mchina Juma Sharobaro anakijali na kukithamini kiswahili kuliko sisi wazawa

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Kiukweli katika vitu ambavyo vinasikitisha na kutia aibu ni kuona raia wa kigeni wakitukuza lugha yetu adhimu ya kiswahili huku sisi waswahili halisi tukipuuzia lugha yetu na kuiona kuwa ni lugha ya kishamba na badala yake tunang'ang'ana na lugha ya malkia ni aibu sana kwa kweli.

Huyu mchina anayejiita Juma Suluhu Sharobaro wa msanga anajitahidi sana kupaisha lugha yetu ya kiswahili sambamba na kupaisha utamaduni wetu wa kitanzania ila kwa sisi wazawa ndio kwaaanza tunatumia nguvu kubwa kukataa vya kwetu , inasikitisha sana kwa kweli.


20181103_174118.jpeg
jumasharobaro-20181103-0001.jpeg
 
Nimezisikiliza ngoma zake ni kali kiliko za kibamia
 
huyo ni marketing manager wa star times...
alivyofika bongo tu. mbinu yake ya kwanza ni kujua kiswahili fasta.. na kujichanganya. na hii imemsaidia sana kuipromote star times..

hata hiyo bongo star search anazingua tu kuweka ladha..

hii ndio inaonesha ubunifu... hii haofundishwi chuo kikuu.. ni ujanja wa kibiashara
 
huyo ni marketing manager wa star times...
alivyofika bongo tu. mbinu yake ya kwanza ni kujua kiswahili fasta.. na kujichanganya. na hii imemsaidia sana kuipromote star times..

hata hiyo bongo star search anazingua tu kuweka ladha..

hii ndio inaonesha ubunifu... hii haofundishwi chuo kikuu.. ni ujanja wa kibiashara
Yeeeeeah
 
Ukweli ni kwamba wengi wanaokiponda kingereza hawako fluent katika lugha hiyo!


Tukubali tu, kingereza kina wenyewe!
 
Wachina wana vichwa vyepesi hatari hadi wazungu huwa wanaogopa hivyo vichwa, nilishawahi kukaa na mzungu akasema chinese ni ma genius
 
Wachina wana vichwa vyepesi hatari hadi wazungu huwa wanaogopa hivyo vichwa, nilishawahi kukaa na mzungu akasema chinese ni ma genius
Wee huoni kwa bashite? Alienda ulaya kupandikiza mbegu holaa akaendamarekani holaa akatinga china maamae kitu kikatunga.

Mchina mshenzi sana
 
Wao wenyewe wakiwa wanaomba kura ili kuwa wabunge wa bunge la Afrika Mashariki wanatumia Kingereza na bado hawakiwezi, mie ni nani haswa hata nijifanye nakijua sana?
 
Mchina balaa, hakuna Mwafrika atakayepona enzi hizi, wapo kila kona, kuuza karanga wapo, kusukuma mikokoteni ndiyo usiseme, hakuna kitu kisichofanywa na Mchina Bongo, akili ni sisi twende kwao tufanye hayo hayo tu..
 
Mchina balaa, hakuna Mwafrika atakayepona enzi hizi, wapo kila kona, kuuza karanga wapo, kusukuma mikokoteni ndiyo usiseme, hakuna kitu kisichofanywa na Mchina Bongo, akili ni sisi twende kwao tufanye hayo hayo tu..
Weka picha ya mchina akisukuma mkokoteni
 
Back
Top Bottom