Uchaguzi 2020 Inaweza isiwe rahisi kwa CCM kuachia kiti cha Urais endapo watakosa kura za kutosha, kwanini?

Uchaguzi 2020 Inaweza isiwe rahisi kwa CCM kuachia kiti cha Urais endapo watakosa kura za kutosha, kwanini?

Mung Chris

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2017
Posts
3,391
Reaction score
3,849
Kuna mengi sana ambayo Huenda yalifanyika kwa kujiamini kuwa utawala utaendelea miaka yote kwa hiyo hamna shida, kifo tu ndio huwa hakimjulishi mwanadamu kuwa siku yako yaja, ila wale ambao ni wa kiroho huwa wanasema nimeambiwa niziungame dhambi zangu na kutubu maana muda wangu umefika.

Kwa dunia ya sasa hivi ni vema kuwa tayari na kujipanga kwa lolote, ukifanya kazi jaribu kurekebisha makosa na uishi vizuri na watu.

Kwa maoni yangu chama kinaweza kisikubali na hakipo tayari kukabidhi kwa sababu: huenda kuna vitu walifanya ambavyo wakiachia au kukabidhi itakuwa ndio mwisho wa maisha yao kama viongozi, wanachama na vizazi vyao.

Maoni yangu ni kwamba siku zote tuwe tayari likitokea ambalo Mungu amepanga lisituathiri kwa sababu ni wasafi, hatuna mabaya na tuna mengi ya kujivunia tumeyafanya.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Kuna mengi sana ambayo Huenda yalifanyika kwa kujiamini kuwa utawala utaendelea miaka yote kwa hiyo hamna shida, kifo tu ndio huwa hakimjulishi mwanadamu kuwa siku yako yaja, ila wale ambao ni wa kiroho huwa wanasema nimeambiwa niziungame dhambi zangu na kutubu maana muda wangu umefika....
Lissu ashasema uongozi wake hautakuwa wa visasi na chuki kama wa Jonijojoni
 
Kuna mengi sana ambayo Huenda yalifanyika kwa kujiamini kuwa utawala utaendelea miaka yote kwa hiyo hamna shida, kifo tu ndio huwa hakimjulishi mwanadamu kuwa siku yako yaja, ila wale ambao ni wa kiroho huwa wanasema nimeambiwa niziungame dhambi zangu na kutubu maana muda wangu umefika....
Umeongea vizuri lakini ni juu juu sana ilitakiwa kujaribu kuongelea vitu vya ndani kama ufisadi au ukiukwaji wa haki za binadamu
 
Kuna mengi sana ambayo Huenda yalifanyika kwa kujiamini kuwa utawala utaendelea miaka yote kwa hiyo hamna shida, kifo tu ndio huwa hakimjulishi mwanadamu kuwa siku yako yaja, ila wale ambao ni wa kiroho huwa wanasema nimeambiwa niziungame dhambi zangu na kutubu maana muda wangu umefika...
Nje ya mada, Bulembo kampeni meneja wa jiwe 2015 safari hii ametoswa?
 
Wale jamaa tegemeo lao la mwisho wao wamesema watakuwa upande wa wananchi wanataka nini awako tayari kutii maagizo ya wachache kwa hasara ya wengi.
 
Kuna mengi sana ambayo Huenda yalifanyika kwa kujiamini kuwa utawala utaendelea miaka yote kwa hiyo hamna shida, kifo tu ndio huwa hakimjulishi mwanadamu kuwa siku yako yaja, ila wale ambao ni wa kiroho huwa wanasema nimeambiwa niziungame dhambi zangu na kutubu maana muda wangu umefika...
Nimekuelewa Mkuu,

Umezungumza sahihi kabisa. Ila wasipotoka kwa hiari basi lazima itatumika tu.
 
Unamaana lisu anaweza kushinda uchaguzi ,hivi unatumia kiungo gani kufikiri
 
Hao ving'ang'anizi ni tone tu kwenye bahari. Ngoja tuone ladha ya chama kingine pia, sio tangu unazaliwa Hadi unakufa chama ni hicho hicho miaka yote la maana hakuna ni sawa na mapokezano ya nyani, ngedere, kima, sokwe, tumbili kwenye shamba hilo hilo siku zote.
Nchi sio chama nchi Ni katiba chama chochote chaweza kuongoza nchi kinapoaminiwa na wengi.
Na wengi wape.
 
Kuna mengi sana ambayo Huenda yalifanyika kwa kujiamini kuwa utawala utaendelea miaka yote kwa hiyo hamna shida, kifo tu ndio huwa hakimjulishi mwanadamu kuwa siku yako yaja, ila wale ambao ni wa kiroho huwa wanasema nimeambiwa niziungame dhambi zangu na kutubu maana muda wangu umefika...
Wengi wataishia jela.
 
Hili liko wazi sana...

Si rahisi wakakabidhi nchi kirahisi...

Tulilo na uhakika nalo ni hili; LAZIMA WATII MAMLAKA MPYA NA HALALI YA WANANCHI....!!

Na shida ni moja. Matendo yao mabaya waliyotenda miaka nenda rudi ndiyo yanayowashtaki...

Hawajui kuwa, kila tendo jema ama baya atendalo mtu katika maisha yake, lina matokeo yake aidha mazuri ama mabaya....

Nakumbuka namna Yesu Kristo alivyoshinda vita ya kutukomboa toka katika UTAWALA na NGUVU na MAMLAKA ya Ibilisi shetani...

Ilikuwa ngumu sana shetani kutema na kuachia madaraka yake....

Lakini NGUVU YA MUNGU ni ya MUNGU tu. Hakuna awezaye kuizuia.....

Kwani mwisho wa siku, alinyoosha mikono juu kama ishara ya ku - surrender.....

Tukawa huru na washindi pamoja naye sasa na hata milele....

Ndivyo itakavyokuwa kuanzia tarehe 29/10/2020. Itakuwa a litle bit chaos....

Maana hawataamini kuwa wameshindwa. Hawataamini kuwa, ile mizizi ya utawala wa CCM wa miaka karibu 60 imekwisha kung'ooka. Hawataamini kuwa hawana NGUVU wala MAMLAKA tena yale waliyokuwa nayo...

Tukumbuke kuwa tawala zote duniani katika nchi mbalimbali ziko hapo kwa ajili ya kusimamia ustawi wa mwanadamu, zinapata KIBALI na MAMLAKA hayo toka kwa Mungu muumba, aliyemuumba mwanadamu huyu kwa mfano wake....

Na kwamba serikali hizo hutenda na kutawala kwa niaba ya Mungu muumba mwenyewe not otherwise...

Utawala huo ukishakosa KIBALI, maana yake unakuwa umekataliwa na Mungu. Kwa lugha rahisi, unakuwa umefukia ukomo wake....

Sasa ni nani aweza kupambana ama kupingana na Mungu muumba? Absolutely, HAYUPO mbinguni wala duniani...!!

Utajitutumua na kujipa haki bandia isiyo na nguvu ya kisheria ya kutaka kuendelea kuwepo, lakini mwisho wa siku utaondoka kimya kimya na kupotea kabisa...

Dola kubwa ya Kirumi ilidondoka na kusahaulika na imebaki kwenye majumba ya historia, itakuwa CCM ya Magufuli???
 
Back
Top Bottom