Nyakwatory, mie naweza jaribu elezea nachokiona hapa kwa mtindo huu.
Kuna kitu kichokuvuta kwa huyu kaka, ndiyo maana unaanza kuelekea kutaka kuwa na mapenzi naye.
Kitu hicho chaweza kuwa chochote labda kujali kwake, pesa zake, chemistry kwake.
Lakini kutokana na maisha ya 'mwanamme wa kiafrika-Rejea uzi wa Babu
Dark City', baadhi ya wanawake wanapenda wanamme wawe viongozi wa familia hasa katika maamuzi. Hii imewafanya baadhi ya wanawake aidha kupenda au kuheshimu mwanamme anayemzidi 'uelewa wa mambo' ili katika maamuzi mengi ya kifamilia au kimahusiano mwanamme aweze kuchukua nafasi yake.
Ikitokea wakati katika mahusiano, mwanamke anakuwa 'smart' kuliko mwanamme maana yake ni kuwa, mambo mengi ya ushauri wa kifamilia au kimahusiano utatoka kwa mwanamke. Kwa watu ambao hawako biased na mfumo dume wala hawashangai na wala hawaoneni tofauti sababu kama mahusiano ni yenu wote na mnafurahia wote.
Kwa baadhi ya wanawake waliokubaliana na mfumo dume, hupenda wanamme watoe maamuzi ili uanamme wake uonekane.
Sasa wewe kikubwa ni kujichunguza, unakubaliana na mfumo dume bila labda hata kutambua??
Kama unakubaliana na mfumo dume, tafuta mwanamme atakayeweza kuwa mwanamme wa kiafrika kwako.
Kwa kifupi, huyu kaka ameshindwa ku-meet expectations zako za mwanamme anatakiwa aweje.
Pamoja sana, hata mie napenda mwanamme ataye-take charge kwenye maamuzi, mie naweza kutoa aidiaz tu
Lakini kufanya maamuzi ya familia afanye mwanamme, na ili uweze ridhika na maamuzi yake lazima awe na upeo aidha wa kulingana na wewe au akuzidi.
Kuna saa unakaa na mtu unajisemea tu moyoni " Dear God, bless his heart"