Inawezekana vipi Historia ya TANU na Kitabu cha Mwalimu Nyerere viandikwe bila kumtaja Iddi Faiz Mafungo?

Inawezekana vipi Historia ya TANU na Kitabu cha Mwalimu Nyerere viandikwe bila kumtaja Iddi Faiz Mafungo?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Naamini bila ya chembe ya wasiwasi kuwa kwa sasa historia ya Iddi Faiz Mafungo inafahamika na wengi.

Iddi Faiz Mafongo Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika aliyesimamia ukusanyaji wa fedha za safari ya kwanza ya Mwalimu Nyerere UNO mwaka wa 1955 na mmoja wa watu waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo Agosti 1955, alifariki tarehe 9 Januari, 1987, akiwa na umri wa miaka 75.

Mwaka 1959 alichaguliwa kuwa mweka hazina wa TANU ngazi ya taifa wakati huo huo akiwa mjumbe wa Kamati Kuu.

Ilikuwa kutokana na uadilifu wake ndiyo alichaguliwa kusimamia hazina ya TANU wakati ambapo uhuru ulipokuwa unakaribia chama kikiwa na fedha nyingi.

Iddi Faiz alikufa mtu masikini na aliyekuwa na kinyongo. Mategemeo yake kwa uhuru alioupigania hayakutimia.

Katika siku zake za mwisho baada ya kustaafu kutoka TANU Press, alikuwa akitumia muda wake mwingi akisoma Qur’an Tukufu.

Alipokufa, Mzalendo gazeti la kila Jumapili la chama alichokiasisi mwenyewe na kukijenga, lilitangaza kifo chake siku mbili baada ya kuzikwa.

Makala ndogo iliyotolewa ilieleza kifo cha mfanyakazi wa zamani na mchango wake katika harakati za kudai uhuru haukugusiwa hata kidogo.

Katika mazishi yake chama hakikupeleka mwakilishi kutoa rambirambi!

Kile kilichompata Abdulwahid Sykes kilimfika Iddi Faiz Mafongo; na kwa bahati wote wawili walikuwa viongozi katika Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na TANU.

Father James Lynch, muasisi wa St. Francis College alikufa Uingereza siku chache kabla ya Idd Faiz.

Kifo chake kilitangazwa katika gazeti la chama Uhuru (8 January, 1987) na gazeti la serikali, Daily News 8 January, 1987).

Magazeti hayo yakaandika kwa urefu mchango wake katika elimu wakati wa ukoloni.

Iddi Faiz, aliyeasisi TANU, akamuunga mkono Nyerere na kupigania uhuru wa Tanganyika, mauti yalimkuta katika hali ya ufukara nyumbani kwake Magomeni na si chama alichokijenga wala serikali aliyoiweka madarakani ilikuwa na habari ya kifo chake.

Huyu Father Lynch ndiye aliyemuandikia barua Mwalimu Nyerere ya kumtaka achague TANU au ualimu.

Picha: Kwanza kushoto ni Iddi Faiz Mafongo, Sheikh Mohamed Ramia, Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro na Haruna Taratibu.

Picha ya pili aliyesimama kulia kwa Julius Nyerere ni Iddi Faiz Mafongo.

342970586_1276220833101871_3161259045312753793_n.jpg
343047986_1587481635106277_5217572830896675614_n.jpg

 
Uhuru wa Tanganyika tulipewa tu na Waingereza, tusingeweza kupigana na bunduki na cannons za mzungu. Historia yetu muhimu zaidi ni baada ya Uhuru. Natamani sana kuona ukiandika mchango wa "wazee wako" katika uandishi wa katiba ya kwanza ya Tanganyika na kama walizingatia nchi hii kupata katiba bora.
 
Unayoyaandika yanapuuzwa kwa sababu umeandika kwa kujaribu kutetea nafasi uislamu ktk kupata uhuru wa kutunukiwa!!!

Ni nani mkristo alipigania uhuru lkn mchango wake haukutambulika kama ambavyo wazee wa kiislamu walipuuzwa baada ya uhuru!!
 
Uhuru wa Tanganyika tulipewa tu na Waingereza, tusingeweza kupigana na bunduki na cannons za mzungu. Historia yetu muhimu zaidi ni baada ya Uhuru. Natamani sana kuona ukiandika mchango wa "wazee wako" katika uandishi wa katiba ya kwanza ya Tanganyika na kama walizingatia nchi hii kupata katiba bora.
Yoda...
Kwa kawaida huandika historia ile ambayo ikiwa imefutwa historia ya kweli inakuwa imepotea.

Kwa ajili hii ikiwa umesoma kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza kuhusu katiba ya TANU ambayo historia rasmi inasema iliandikwa na Julius Nyerere.

Ukweli ni kuwa historia ya TANU ilinakiliwa kutoka katiba ya Convention People's Party (CPP) chama cha Kwame Nkrumah wa Ghana.

Sababu ya kufanya hivi ni kuwachenga Waingereza wasiikatae katibu ya TANU kwa kuwa katiba kama hiyo CPP tayari walishaikubali Ghana na kuipitisha.

Ushauri huu wa katiba ilikuwa fikra za Earle Seaton kwa Abdul Sykes miaka mingi nyuma hata Nyerere bado hajawa kiongozi wa TAA.

Kuhusu kunyanyua silaha kupigana na Waingereza hili halikuwapo katika fikra za waasisi wa African Association walipokiasisi chama mwaka wa 1929.

Waafrika walikuwa wanajua kuwa hapakuwa na haja ya kunyanyua silaha dhidi ya Waingereza kwani utawala wa Waingereza ulikuwa tofauti sana na Wajerumani.

Mbali na haya upepo ulikuwa umebadilika sana kwa Waingereza kuanzisha ''Indirect Rule.''

Ukoloni ulikuwa umetamalaki lakini nchi ilkikuwa imetulia ila kwa Tanganyika kuwa inatawaliwa.
 
Unayoyaandika yanapuuzwa kwa sababu umeandika kwa kujaribu kutetea nafasi uislamu ktk kupata uhuru wa kutunukiwa!!!

Ni nani mkristo alipigania uhuru lkn mchango wake haukutambulika kama ambavyo wazee wa kiislamu walipuuzwa baada ya uhuru!!
Mpaji...
Sijapata kupuuzwa hata kidogo.

Baada ya kitabu kuchapwa na kjuingia nchini gazeti la The East African (Nairobi) walifanya ''serialisation'' tatu ya kitabu.

Kitabu kikafanyiwa pitio na mabingwa wa Historia ya Afrika (John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan) na kuchapwa katika Cambridge Journal of African History 1998.

Oxford University Press, Nairobi wakanitia katika mradi wa kuandika vitabu vya historia ambavyo vinashomeshwa katika kufundisha lugha ya Kiingereza katika shule za msingi Afrika ya Mashariki na kwengineko.

OUP wakachapa kitabu changu, ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2006) na ''The Mermaid of Msambweni,'' hiki nikishirikiana na waandishi wengine kutoka nchi mbalimbali za Afrika.

Harvard na Oxford University Press, New York wakanitia katika kuandika Dictionary of African Biography (DAB) wakaniomba niandike historia ya Kleist Sykes na wanae katika kupigania ukombozi wa Tanganyika kutoka ukoloni wa Muingereza.

Hili kamusi limetoka 2011.

University of Iowa na Northwestern University wakanialika kuzungumza vyuoni kwao 2011.

Vyuo vingi vikanifungulia milango yao hapa nyumbani na kwengine: Kenyatta University, University of Ibadan, University of Johannesburg nk.

Unajua kitabu changu kilivutia wanafunzi wa historia ya Afrika kwa kuwa ndani kulikuwa na historia ya Mwalimu Nyerere ambayo haikuwa ikifahamika.

Kitabu kilibadili maisha yangu kwa njia ambayo sikutegemea kabisa.
Huu mwaka wa 25 kitabu kimechapwa matoleo manne kwa Kiingereza na Kiswahili.

Hizi si dalili ya mimi kupuuzwa.
Wewe umeshindwa kunipuuza uko hapa unanisoma.

1682508883544.jpeg


1682507410408.png

1682507464867.png

 
Mpaji...
Sijapata kupuuzwa hata kidogo.

Baada ya kitabu kuchapwa na kjuingia nchini gazeti la The East African (Nairobi) walifanya ''serialisation'' tatu ya kitabu.

Kitabu kikafanyiwa pitio na mabingwa wa Historia ya Afrika na kuchapwa katika Cambridge Journal of African History 1998.

Oxford University Press, Nairobi wakanitia katika mradi wa kuandika vitabu vya historia ambavyo vitashomeshwa katika kufundisha lugha ya Kiingereza katika shule za msingi Afrika ya Mashariki na kwengineko.

OUP wakachapa kitabu changu, ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2006) na ''The Mermaid of Msambweni,'' hiki nikishirikiana na waandishi wengine kutoka nchi mbalimbali za Afrika.

Harvard na Oxford University Press, New York wakanitia katika kuandika Dictionary of African Biography (DAB) wakaniomba niandike historia ya Kleist Sykes na wanae katika kupigania ukombozi wa Tanganyika kutoka ukoloni wa Muingereza.

Hili kamusi limetoka 2011.

University of Iowa na Northwestern University wakanialika kuzungumza vyuoni kwao 2011.

Vyuo vingi vikanifungulia milango yao hapa nyumbani na kwengine: Kenyatta University, University of Ibadan, University of Johannesburg nk.

Unajua kitabu changu kilivutia wanafunzi wa historia ya Afrika kwa kuwa ndani kulikuwa na historia ya Mwalimu Nyerere ambayo haikuwa ikifahamika.

Kitabu kilibadili maisha yangu kwa njia ambayo sikutegemea kabisa.
Huu mwaka wa 25 kitabu kimechapwa matoleo manne kwa Kiingereza na Kiswahili.

Hizi si dalili ya mimi kupuuzwa.
Wewe umeshindwa kunipuuza uko hapa unanisoma.

Kama vina ukweli na uhalisia, vinatambulika rasmi nchini kwanini havitumiki nchini katika kufundishia?

Basi hata kama sio kufundishia, kwann hvo vitabu havipo katika maktaba za vyuo vyetu ili watu wavisome wapate hyo historia ambayo we unaamin ni ya kwel?
 
Kama vina ukweli na uhalisia, vinatambulika rasmi nchini kwanini havitumiki nchini katika kufundishia?

Basi hata kama sio kufundishia, kwann hvo vitabu havipo katika maktaba za vyuo vyetu ili watu wavisome wapate hyo historia ambayo we unaamin ni ya kwel?
Mpaji...
Swali hilo ungewauliza wahusika kwa nini hawakifundishi kitabu changu pia waulize ilikuwaje historia ya TANU ikaandikwa ikiwa imejaa makosa?

Ninachojua ni kuwa kitabu cha Abdul Sykes kipo Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hali kadhalika kitabu kinachoeleza katika sura yake moja historia ya baba yake, Kleist Kleist kipo pia Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Kitabu hiki, ''Modern Tanzanians,'' (1973) kimehaririwa na John Iliffe na hiyo sura imeandikwa na mjukuu wa Kleist Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes akiwa mwanafunzi wa John Iliffe hapo chuoni University of East Africa, 1968.

Sura hiyo imeandikwa kutoka Seminar paper inayoeleza maisha ya Kleist Sykes hiyo paper ipo East Africana Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Si mimi naamini kuwa historia hii niliyoandika ni kweli hata Jopo la Prof, Issa Shivji wanaamini naliyoandika kwani walipokuwa wanaandika kitabu cha maisha ya Julius Nyerere: ''Nyerere Biography,'' (2020) walifanya mahojiano na mimi kuhusu historia ya Nyerere alipofika Dar es Salaam 1952.

Kitabu cha Mwalimu wameninukuu sehemu nyingi.

1682509887704.jpeg

1682510005086.jpeg

Vitabu hivi viwili viko Maktaba ya
Kikuu Cha Dar es Salaam

1682510599377.jpeg

Picha hizo hapo juu nikihojiwa na Jopo 2013 na zawadi ya kitabu walichonipa kwa kuwapa ushirikiano na katika kitabu wamesifia Maktaba yangu kuwa ni katika maktaba tatu bora zenye historia ya Mwalimu: Maktaba ya Dr. Salim Ahmed Salim, Brig, General Hashim Mbita na ya Mohamed Said​
 
Umejaribu kuandika chako na kumtaja yoyote unayetaka kumtaja wino ukagoma kuganda ?

Uzuri tupo kwenye enzi ambazo kuandika kitabu imekuwa virtually free ; kwahio uwanja ni wako ila kusema wamba historia hii ni ya uongo na ile ndio ya ukweli watu wakubaliane na wewe tu sababu umesema; nadhani it takes more than that...
 
Mpaji...
Swali hilo ungewauliza wahusika si kwa nini hawakifundishi kitabu changu bali waulize ilikuwaje historia ya TANU ikaandikwa ikiwa imejaa makosa?

Ninachojua ni kuwa kitabu cha Abdul Sykes kipo Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hali kadhalika kitabu kinachoeleza katika sura yake moja historia ya baba yake, Kleist Kleist kipo pia Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Kitabu hiki, ''Modern Tanzanians,'' kimehaririwa na John Iliffe na hiyo sura imeandikwa na mjukuu wa Kleist Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes akiwa mwanafunzi hapo chuoni University of East Africa, 1968.

Sura hiyo imeandikwa kutoka Seminar paper inayoeleza maisha ya Kleist Sykes ipo East Africana Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Si mimi naamini kuwa historia hii niliyoandika ni kweli hata Jopo la Prof, Issa Shivji wanaamini kwani walkipokuwa wanaandika kitabu cha maisha ya Julius Nyerere: ''Nyerere Biography,'' walifanya mahojiano na mimi kuhusu historia ya Nyerere alipofika Dar es Salaam 1952.

Siweziiiiiiii sema niwaulize mamlaka kwanini hawakitumii bali jibu sahihi ni kwamba relevancy ya yaliyomo ni ndogo....

Mbona kina Nyambari Nyangwine, Zisti kamili, salehe yasini na wengn ambao siwezii kuwakumbuka kwa haraka vitabu vyao vinatumika na vimejaa lukuki kwenye maktaba ya shule ya sekondari?
 
Siweziiiiiiii sema niwaulize mamlaka kwanini hawakitumii bali jibu sahihi ni kwamba relevancy ya yaliyomo ni ndogo....

Mbona kina Nyambari Nyangwine, Zisti kamili, salehe yasini na wengn ambao siwezii kuwakumbuka kwa haraka vitabu vyao vinatumika na vimejaa lukuki kwenye maktaba ya shule ya sekondari?
Mpaji...
Sina tatizo na fikra zako.

Kitabu changu kipo sasa robo karne lakini bado tunakijadili.

Vitabu hivyo ulivyovitaja viko wapi?

Kitabu kinapokosa kuwa na elimu huwa kinakufa kama tunavyokufa binadamu.
 
Abdul Kandoro ndo Yule Yule saadani Kandoro alieandika vitabu vya kiswahili??
 
Back
Top Bottom