Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu salam,
Inawezekana matukio haya hasa kwa wapinzani kutekwa na kuuliwa ikawa kitendawili kwa serikali, bado ikawa fumbo kubwa kwao kung'amua nani anahusika na maatukio haya dhalimu, lakini ukimya wao unasema vingine.
Walitakiwa kuwa mstari wa mbele kukemea na kuchukua hatua haraka pindi tu yanapotokea ama kuripotiwa na wananchi.
Lakini kila wakipelekewa ripoti majibu yamekuwa siyo ya kuridhisha na Spika alipigilia msumari majuzi kuwa matukio haya hayastahili kuangaliwa kwa jicho la tatu na kwa udharura kama wananchi wanavyopata taharuki.
Hitimisho mnalotuachia wananchi ni kuwa ninyi ndio wahusika wakubwa wa matukio haya.
Mkiendelea kukaa kimya wananchi watakuja na mbinu zao ili kupata suluhu.
Inawezekana matukio haya hasa kwa wapinzani kutekwa na kuuliwa ikawa kitendawili kwa serikali, bado ikawa fumbo kubwa kwao kung'amua nani anahusika na maatukio haya dhalimu, lakini ukimya wao unasema vingine.
Walitakiwa kuwa mstari wa mbele kukemea na kuchukua hatua haraka pindi tu yanapotokea ama kuripotiwa na wananchi.
Lakini kila wakipelekewa ripoti majibu yamekuwa siyo ya kuridhisha na Spika alipigilia msumari majuzi kuwa matukio haya hayastahili kuangaliwa kwa jicho la tatu na kwa udharura kama wananchi wanavyopata taharuki.
Hitimisho mnalotuachia wananchi ni kuwa ninyi ndio wahusika wakubwa wa matukio haya.
Mkiendelea kukaa kimya wananchi watakuja na mbinu zao ili kupata suluhu.