Indonesia: Mwalimu wa shule ya Kiislamu aliyebaka wanafunzi 13 ahukumiwa kifungo cha maisha jela

Indonesia: Mwalimu wa shule ya Kiislamu aliyebaka wanafunzi 13 ahukumiwa kifungo cha maisha jela

Robidinyo

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
4,043
Reaction score
8,686
ap22046308269502.jpg

Herry Wirawan (katikati) mkuu wa shule ya wasichana ya Kiislamu aliyepatikana na hatia ya kubaka wanafunzi, akisindikizwa na maafisa wa usalama wakati wa kusikilizwa kwa hukumu katika mahakama ya wilaya ya Bandung, Java Magharibi, Indonesia, Februari 15, 2022. Rafi Fadh / AP

Mahakama moja ya Indonesia siku ya Jumanne ilimuhukumu mwalimu wa somo la dini ya Kiislamu kifungo cha maisha jela kwa kuwabaka wanafunzi 13 wa kike.

Wanane kati yao walio na umri wa kati ya miaka 12 hadi 16 ni wajawazito kulingana na uchunguzi wa polisi.

Kesi hiyo inaangazia unyanyasaji katika baadhi ya shule za mabweni ambazo nyingi ni vituo vya mafunzo ya kiislamu.

Jaji aliamuru kwamba mwalimu Herry Wirawan, aliwanyanyasa kingono wanafunzi hao na kwamba baadhi yao walijeruhiwa vibaya.

Tabia ya Wirawan iligunduliwa mnamo mwezi Mei mwaka uliopita wakati mzazi wa msichana mmoja alipotangaza kwamba mwanawe wa kike ni mjamzito.

Viongozi wa mashtaka walimtaka mwalimu huyo kuhukumiwa kifo ama hata kuchinjwa kwasababu uhalifu alioutenda ulikuwa mbaya na ulifanyika kati ya mwaka 2016 hadi 2021.

Serikali ya Jakarta imetangaza kwamba itawalipa karibia dola 6000 kama fidia kila msichana aliyeathirika.
 
Ungesema mualimu....hamna haja ya kuweka somo lake analo fundisha, labda unatafuta kudhalilisha Dini.
 
Duh..!Hatari sana hii.
Dini zimegeuka kuwa mapango ya wahalifu.
M/Mungu awalaani wote wanaotumia kivuli chake kufanya mambo yanayoenda kinyume na maagizo yake.

Serikali ya Jakarta imetangaza kwamba itawalipa karibia dola 6000 kama fidia kila msichana aliyeathirika.
Kulipa fidia ni sawa, ila isije ikawa ni kichocheo cha watoto wengine kujilengesha kwa "maustaadh'.

Hakuna mkate mgumu mbele ya chai..wanaume ni dhaifu.
 
sidhani media za Indonesia kamwe zinaandika habari za wanafunzi walio repiwa na walimu wa shule za Tanzania....

mwafrika haishi kujibaraguza na mambo ya "mzungu"
 
Back
Top Bottom