Infinix Kiboko imeleta simu unaweza kuichaji kupitia Mwanga wa Jua 🌀️

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240
Infinix Imetisha imeleta simu unaweza kuichaji kupitia Mwanga wa Jua




πŸ’­ Ebu fikiria unatembea kwa miguu jua Kali na simu yako inakaribia kuzima, au huko kwenye gari mwanga wa Jua unakupiga tu usoni, utajisikiaje kutumia Hiyo fursa kuweza kuchaji simu yako ??🀫

πŸš€ Kampuni ya kichina yenye kutoa simu za Brandi aina ya Infinix wameendelea kuishikiria Dunia kwa namna yao Wenyewe, Kupitia onyesho la MWC ya mwaka huu wameleta simu Yenye uwezo wa kuchajiwa kupitia Mwanga wa Jua.



πŸ—£οΈ Infinix inakua kampuni ya kwanza kutoa Teknolojia hii kwenye matoleo ya simu Ulimwenguni ambapo kupitia paneli za jua zilizounganishwa kwa nyuma inakupa uwezo wa kuchaji simu yako pamoja na kava lake lenye uwezo wa kuchaji simu yako kupitia Mwanga wa Jua.



πŸ”† Teknolojia hii Infinix wameiita Solar energy Reserving Technology , hutumia seli za jua za Perovskite ambazo ni nyembamba kuweza kuzalisha seli ambazo inasaidia kuthibiti voltage. teknolojia hii inaweza kuchaji simu hadi 2W kwa dakika 10 na kukusaidia kulipia chaji iliyohifadhiwa ya simu wakati haitumiki.



πŸ’‘ Bila kusahau Ina Teknolojia ya E - COLOR yenye kubadili Rangi ya simu yako kutokana na unachofikiria yani rangi unayofikiria basi Yenyewe inajibadilisha.

Lakini kwa ujumla si si Vyema kuweka vifaa vya kieletroniki juani ila kwa Infinix wamekuja kubadilika dhana hii kwani unaiweka juani na wala haipati Joto kutokana na Teknolojia iliyoundwa Nayo.



Tuwape Maua yao @infinixmobiletz πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

#infinix #infinixmobiletz #simumpya #teknoloji #ai #infinixmobile #solarenergy #solarenergyresearch #solarpower #habari #showstoppersmwc #bongotech255
 
Hawa jamaa wako serious sana na wanachokifanya, nawafuatilia inaonekana kuna pahala wanataka kufika.
 
Kama Jua liko vizuri kama Jua la Dar, Moro, Lindi, Mtwara, Pwani...
Simu inaweza kujaa Full charge kwa muda gani..?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…