Inonga kama Dube, ameichoka Simba

Inonga kama Dube, ameichoka Simba

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Kuna watu wanamsema Inonga kuwa anafanya makosa mengi uwanjani siku hizi kuliko zamani bila kuangalia mambo muhimu. Ukweli ni kwamba Inonga hana raha kucheza Simba.

Inonga ni mchezaji mkubwa sana, anapata namba kikosi Cha kwanza Cha DRC ambacho kimesheheni wachezaji wanaolipwa fedha nyingi sana wanaocheza ulaya. Wachezaji hawa yawezekana wamemwambia mengi sana kule afcon yanayomvunja moyo kucheza timu kama Simba.

Kucheza kwenye timu ambayo imekosa ubingwa wa ligi kwa misimu 2 mfululizo ingawa yeye anacheza vizuri sana uwanjani inaweza kumvunja moyo wa kupambana.

Kufungwa goli 5 na Yanga inawezekana hakujamuondoka kichwaji.

Rafiki yake Mayelle kulipwa hela nyingi huko aliko pyramids kunaweza kumchanganya akili

Kuumia mara kwa mara kwenye timu ambayo haichukui makombe wala kuvuka robo finali za CAF kunamkatisha tamaa mchezaji anaejituma sana uwanjani.

Inawezekana mchezaji huyu ana uchovu mwingi sana kutokana na kucheza mechi nyingi sana za Simba na za timu ya taifaa, inawezekana ana maumivu mahali.

Hakuna mtu anaekaa na Inonga kumuuliza anapitia shida zipi kabla ya kumlaumu kila Kona mitandaoni.

Dube hakuwa na Raha kwenye timu ambayo anavuja jasho jingi sana na kuumia lakini hanyanyui makwapa yake kushangilia. Hakuna mchezaji anaitwa timu yake ya taifa anaependa kucheza timu isiyoshinda.

Kaeni na Inonga badala ya kumlaumu.
 
Mi nadhani kinachowachosha wachezaji ni ahadi za uwongo uwongo na tuhuma za mara kwa mara team inapofanya vibaya
Siasa za kwenye hizi team ni za hovyo sana ,unaweza kupewa jina baya mda wowote imagine Kuna siku walisema Mkude akapimwe akili na kupewa rehab
Imagine umekaa na familia Yako mara unasikia taarifa kama hiyo halafu kesho unatakiwa ukacheze kwa nguvu huku mshahara wako godfather mmoja asiejua hata kupiga danadana kaukata 40%
Pathetic Inonga aje yanga club above all
 
Mi nadhani kinachowachosha wachezaji ni ahadi za uwongo uwongo na tuhuma za mara kwa mara team inapofanya vibaya
Siasa za kwenye hizi team ni za hovyo sana ,unaweza kupewa jina baya mda wowote imagine Kuna siku walisema Mkude akapimwe akili na kupewa rehab
Imagine umekaa na familia Yako mara unasikia taarifa kama hiyo halafu kesho unatakiwa ukacheze kwa nguvu huku mshahara wako godfather mmoja asiejua hata kupiga danadana kaukata 40%
Pathetic Inonga aje yanga club above all
Eti mtu na kiongozi anajichukulia sheria mkononi kumtuhumu na kumhukumu mchezaji mbele ya kamera na mitandaoni na TFF na kamati ya haki za wachezaji inakaa kimya.
 
Back
Top Bottom