Intelejinsia ya Polisi inaishia kwenye mikutano ya CHADEMA, kwenye mikusanyiko ya kidini ya Mwamposa inakuwa imezibwa macho

Intelejinsia ya Polisi inaishia kwenye mikutano ya CHADEMA, kwenye mikusanyiko ya kidini ya Mwamposa inakuwa imezibwa macho

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Tumeshuhudia mara kadhaa mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani, hususan ya Chadema, ikizuiwa na Polisi, kwa maelezo kuwa kwa taarifa zao "walizozinusa" mikutano hiyo italeta machafuko na hivyo kusababisha hatari ya maafa.

Hata hivyo, mtumishi wa Mungu, anayejiita Mtume Boniface Mwamposa, katika mkusanyiko mkubwa wa kidini, tukio la ukanyagaji wa mafuta huko mjini Moshi, limesababisha maafa ya wakazi wa huko, wasiopungua 20.

Kuondokewa na uhai wa angalau mtu moja, ni tukio baya kabisa. Sembuse raia wasiopungua 20?

Tunalifahamu Jeshi letu la Polisi lilivyo na utaalamu wa hsli ya juu wa "kunusa" matukio yatakayofuata, ikiwa chama cha siasa cha upinzani kinataka kufanya mikutano wake wa kisiasa katika maeneo mbalimbali.

Haraka haraka huzuia mikutano hiyo kwa madai ya kwamba Jeshi la Polisi limebaini kwa "kunusa" kuwa mikutano hiyo utakuwa siyo salama kwa wananchi kuhudhuria na hivyo kuipiga marufuku.

Ninachojiuliza hivi intelejensia ya Polisi ilienda "likizo" wakati wa kutokea maafa hayo ya mkusanyiko wa Boniface Mwamposa, hadi washindwe "kunusa" kuwa mkusanyiko huo wa kudini uteleta maafa makubwa sana?
 
Yaani Mungu amewaumbua ingawa waziri anawatetea polisi ila bado mengi tutayaona.
 
PoliCCM intelijensia yao huwa ni kwa ajili ya kuwakandamiza wapinzani.
 
Tumeshuhudia mara kadhaa mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani, hususan ya Chadema, ikizuiwa na Polisi, kwa maelezo kuwa kwa taarifa zao "walizozinusa" mikutano hiyo italeta machafuko na hivyo kusababisha hatari ya maafa.

Hata hivyo, mtumishi wa Mungu, anayejiita Mtume Boniface Mwamposa, katika mkusanyiko mkubwa wa kidini, tukio la ukanyagaji wa mafuta huko mjini Moshi, limesababisha maafa ya wakazi wa huko, wasiopungua 20.

Kuondokewa na uhai wa angalau mtu moja, ni tukio baya kabisa. Sembuse raia wasiopungua 20?

Tunalifahamu Jeshi letu la Polisi lilivyo na utaalamu wa hsli ya juu wa "kunusa" matukio yatakayofuata, ikiwa chama cha siasa cha upinzani kinataka kufanya mikutano wake wa kisiasa katika maeneo mbalimbali.

Haraka haraka huzuia mikutano hiyo kwa madai ya kwamba Jeshi la Polisi limebaini kwa "kunusa" kuwa mikutano hiyo utakuwa siyo salama kwa wananchi kuhudhuria na hivyo kuipiga marufuku.

Ninachojiuliza hivi intelejensia ya Polisi ilienda "likizo" wakati wa kutokea maafa hayo ya mkusanyiko wa Boniface Mwamposa, hadi washindwe "kunusa" kuwa mkusanyiko huo wa kudini uteleta maafa makubwa sana?
Wanauwezo wa kunusa wapinzani bana! tena huwa wananusa kabla hata kuanza huo mkutano tena awamu ya 5 kiwango chao cha kunusa wapinzani kiko juu sana wanastihili pongezi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom