Intelijensia ya CHADEMA ilishindwaje kubaini mipango ya Msigwa kabla hajatoka?

Intelijensia ya CHADEMA ilishindwaje kubaini mipango ya Msigwa kabla hajatoka?

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Ni dhahiri, Msigwa alipojiunga CHADEMA, kama ilivyo kwa wengi waliokuja kukengeuka baadaye na kuamua kuwa mapandikizi, alikuwa ni mwanachama halisi aliyekuwa ameamua kuwa CHADEMA. Lakini wakati wa uongozi wa Magufuli, bila shaka, kwa hulka yake ya tamaa ya cheo, alishindwa kuhimili kuishi bila cheo na bila ya pesa. Akaamua kuwangukia CCM kwa namna ambayo aliamini haitamletea fedheha, akajisalimisha, na kwa kupitia yeye inaonekana kila taarifa za vikao vya ngazi za juu vya CHADEMA, Msigwa alizivujisha CCM. Na yeye akawa ndiye daraja la kuwaangamiza viongozi wenzake. Mawasiliano yake na hasimu wake wa sasa yanadhihirisha hilo.

Jambo la kujiuliza, je, intelijensia ya CHADEMA ni makini kiasi gani ili kuwatambua mapandikizi ya CCM ndani ya chama chao? Je, ndani ya CHADEMA, bado kuna akina Msigwa wangapi?

Ni dhahiri, kazi kubwa ambayo CCM ilimpa Msigwa ni kuipelekea CCM, mambo ya siri yanayojadiliwa na vikao vikuu vya CHADEMA. Hivyo baada ya kushindwa kuchaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa kanda, nafasi ambayo ingemwezesha kuingia kwenye vikao vyote vya ngazi ya juu, hakuwa tena asset kwa CCM, na hivyo akalazimika kuomba kwenda kuhifadhiwa na wale ambao amekuwa akiwatumikia.

Msigwa_Polepole.jpg
 
Wanasema walishamshtukia kitambo na wakaanza kumpunguza kidogo kidogo, sijui tumuamini nani sasa.
 
Binafsi naona siasa za Tanzania ni za kitoto saaana, Leo hii tunamuita Msigwa pandikizi lakini tunasahau Lowassa alikuja CDM tukampa nafasi ya kugombea Urais na team yake wengi wakawa wagombea ubunge na kuanzia hapo tukamuita Dr Slaa msaliti.

Kwanini pia tusiamini Mbowe naye ni pandikizi hapo CDM?
 
Hili jambo la Msigwa kuhamia CCM halipaswi kuangaliwa mwa macho mepesi. Tatizo ni kwamba Watanzania wengi hawaoni mbali zaidi ya urefu wa pua zao!
 
..sio kazi ya vyama vya siasa kuwa na idara za Intelijensia.

..tukatae siasa za kijinga na kishamba zinazoendekezwa na Ccm.
 
Binafsi naona siasa za Tanzania ni za kitoto saaana, Leo hii tunamuita Msigwa pandikizi lakini tunasahau Lowassa alikuja CDM tukampa nafasi ya kugombea Urais na team yake wengi wakawa wagombea ubunge na kuanzia hapo tukamuita Dr Slaa msaliti.

Kwanini pia tusiamini Mbowe naye ni pandikizi hapo CDM?
Umeandika point sana
 
Binafsi naona siasa za Tanzania ni za kitoto saaana, Leo hii tunamuita Msigwa pandikizi lakini tunasahau Lowassa alikuja CDM tukampa nafasi ya kugombea Urais na team yake wengi wakawa wagombea ubunge na kuanzia hapo tukamuita Dr Slaa msaliti.

Kwanini pia tusiamini Mbowe naye ni pandikizi hapo CDM?
Ushahidi unaonesha wa meseji kuwa alikuwa pandikizi lakini hawezi kufanikiwa. Hata CCM wako mapandikizi wanayajua? Na pia huko CCM siyo Salama Msigwa atafanya kazi kama aliyotumwa Chadema chawa ni chawa tu.
 
Wanasema walishamshtukia kitambo na wakaanza kumpunguza kidogo kidogo, sijui tumuamini nani sasa.
Huyu hakustahili kuachwa ajiondoe bali alistahili kufukuzwa.
 
Ushahidi unaonesha wa meseji kuwa alikuwa pandikizi lakini hawezi kufanikiwa. Hata CCM wako mapandikizi wanayajua? Na pia huko CCM siyo Salama Msigwa atafanya kazi kama aliyotumwa Chadema chawa ni chawa tu.
Upo sahihi. Ni sawa uamue kuwa na rafiki muuaji, ukakosa kujua kuwa siku mkikorofishana, atakuua na wewe pia.
 
Hiyo imetengenezwa kaka sikubaliani na msigwa but that tweet was faked and edited

Account ya Polepole iko deactivated na X kitambo hata ukichek tarehe wanazosema siyo sahihi

Pia pitia account ya Msigwa ya X hakuna ujumbe Kama huo


Britanicca
 
Back
Top Bottom