Nyumba ya mbao kuna vitu havitakuwepo
Gharama ya kubeba tofali ulikozinunulia au kama umefyatulia nyumbani hakutakuwepo na wasaidizi wengi wa fundi unaweza kuwa mwenyewe msaidizi,
Kokoto na mchanga hazitakuwepo labda tu kama utaweka msingi wa chini, nondo hazitakuwepo matumizi ya maji mambo ya kupiga plasta no, eleza na wewe
Je? Ni kweli gharama zitapungua au ndo wanasema fanya ujionee mwenyewe
Mkuu umekuwa mzungu, maUlaya Ulaya huko?
Nyumba ya mbao labda banda la kiosk!
Kuna mahitaji ya gharama pamoja na vifaa vya ujenzi havikwepeki kwenye ujenzi wa nyumba ya mbao.
Mawe, kokoto, saruji, nondo, bati, misumari, ceilling board za kufa mtu, wiring na rangi.
Mbao zinazotakiwa hapo ni mbao za mtiki, mninga au mkola, mbao ghali grade1 zisizotetereka na hali ya hewa na wadudu kwa muda mrefu.
Unaelewa bei ya square ft ya ubao wa mninga grade1 bei ya sokoni leo?
Usije kusema nakukatisha tamaa, nakushauri ifuatavyo:
Shirikisha mafundi kwa kutafuta hesabu ya gharama za ujenzi wa boma la tofari pekee laweza kutumia gharama gani.
Kisha pima sucumphrance ya huo mzunguko kutafuta idadi ya mbao na gharama zitakazotumika kununulia mbao kwa ujenzi wa boma la mbao, ukianza na beam(nguzo) za nondo ama za mbao 8×8 ndiyo uelewe utatumia mbao kiasi gani.
Ukishamaliza utafiti huo ndiyo utaelewa wapi kuna taafifu.
Gharama za msingi pamoja na paa vinalingana.