MIXOLOGIST
JF-Expert Member
- Mar 1, 2016
- 14,311
- 36,056
Habari wana JF,
Nimesikiliza hotuba ya muheshimiwa Raisi kwa uzuri kabisa nikamwelewa, lakini lugha hii yetu pendwa (kiswahili) hajazungumzwa mahala popote.
Hapo awali kiswahili kilitiliwa mkazo kwa sababu zinazojulikana na utawala uliopita. Lugha ya kiingereza ilionekana ni anasa au kielelezo cha kuukubali na kuukiri ubeberu. Watawala walijinasibu kuongea kiswahili kwenye halaiki zenye watu wasiokijua. Mipango iliwekwa ili hukumu za mahakama zitolewe kwa lugha yetu, pia na mitaala yetu ya shule iwe ya kiswahili.
Ukimya huu, kuhusu lugha yetu unaashiria nini? Embu wadodosi wa mambo mtujuze
Nimesikiliza hotuba ya muheshimiwa Raisi kwa uzuri kabisa nikamwelewa, lakini lugha hii yetu pendwa (kiswahili) hajazungumzwa mahala popote.
Hapo awali kiswahili kilitiliwa mkazo kwa sababu zinazojulikana na utawala uliopita. Lugha ya kiingereza ilionekana ni anasa au kielelezo cha kuukubali na kuukiri ubeberu. Watawala walijinasibu kuongea kiswahili kwenye halaiki zenye watu wasiokijua. Mipango iliwekwa ili hukumu za mahakama zitolewe kwa lugha yetu, pia na mitaala yetu ya shule iwe ya kiswahili.
Ukimya huu, kuhusu lugha yetu unaashiria nini? Embu wadodosi wa mambo mtujuze