Iramba hatumtaki tena Mwigulu Nchemba

Lyambalyetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2021
Posts
278
Reaction score
255
Huyu bwana Dkt. Mwigulu amekuwa akija hapa bila majibu ya maana kwa manufaa ya Jimbo na Wilaya yetu ya Iramba. Huyu hatufai tena kwani kiu yake ni kufanya siasa za KiTaifa ili aje amtoe Mama Samia mwaka 2025.

Tunafanya utafiti ni nani sasa atafaa kuiwakilisha Iramba bungeni kuanzia Mwaka 2025. Mama Samia hebu mwangalie sana huyu mtu 2025, jimboni ameandaa watu wanaomuunga mkono kwa nguvu zote na hata kabla JPM hajachukuliwa kwa mapenzi ya Mungu alishajisema 2025 lazima awe.

Haya mawazo na plan yake hajaibatilisha hata pamoja na kujua 2025 hastahili kutia pua yake.

Tafadhali Rais Samia ukibahatika kutoangushwa na hawa watu 2025 basi huyu peleka ubalozi wa mbali ili jimbo letu lipate mwakilishi anayeipenda Iramba kwa dhati badala ya Mfia URais huyu!
 
Huyu muuaji ndio anataka aje kua amilijeshi kweli Tanzania imekua uwanja wa majalibio ya viongozi ndio maana tukafikia mpaka kuongozwa na vichaa Katiba mpyaa ndio kipaumbele chetu
 
Mshafuta majina yake kwenye mawe nchi nzima?
 
Kwa hulka aliyoonyesha Mwigulu hivi karibuni..ni aina ya mtu ambae atakuwa tayari hata kupoteza maisha ya mtu yoyote ambae atakuwa kikwazo kwake ili awe Kiongozi...huyu hafai hata kidogo.
 
Mwigulu mnamtajataja na kumuongezea umaarufu bure tu, hana uwezo huo mnaompa hapa, ni mtu anayetegemea huruma ya Rais aliyepo madarakani kwa wakati husika, zaidi ya hapo hamna kitu. Wanasiasa wanamkakati na wakuogopewa kwa mikakati yao walikuwa ni Kikwete, Lowassa na Rostam, sidhani kama watakuja kutokea wanasiasa kama hao siku za karibuni. Hawa wengine wote wanaishi kwa huruma za Mkiti, Samia akiamua kumpoteza huyo Mwigulu kwenye siasa ni jambo la saa moja tu. Wapo wapi Bashite, Polepole na Bashiru leo hii?
 
Asipewe hata huo ubapozi.akae pembeni kabisa.
Huko Iramba tafuteni diwani mzuri mwenye hoja ambae mnaishi nae hukohuko,Mwigulu atakuja kuwauza
 


Lyambalyetu fanya kuwawakilisha wanairamba bungeni wewe mwenyewe
Katiba inakuruhusu kabisaaa
 
Na ukizingatia ameshachemka suala la kodi za miamala, kishaminywa ko..dani!
 
Shida Tanzania mwananchi hana maamuzi kwenye kuchagua viongozi, chungunza asilimia kubwa kama sio wote wabunge na madiwani hawakuchaguliwa na watu, ndio maana watu wanaojiandikisha ni wengi ila wanaenda kupiga kura ni wachache
Kwaiyo unavyosema iramba hawamtaki mwigulu hayo ni maoni tu ila Tanzania tunasafari ndefu sana kuwa na uchaguzi unaotoa nguvu kwa wananchi
 
Asipewe hata huo ubapozi.akae pembeni kabisa.
Huko Iramba tafuteni diwani mzuri mwenye hoja ambae mnaishi nae hukohuko,Mwigulu atakuja kuwauza
Madiwani wote amewaweka wa kwake. Hata Mwenyekiti wa Halmshauri ni wa kijijini kwake wakati ni Form 4 failure kabisa!
 
Ukiona Bavicha hawamtaki mtu ujue huyo ni mtu sahihi
 

kwa nini ampeleke ubalozini. Apigwe chini tu, kwani kuna shida gani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…