Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Kuelekea kuanza kwa zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura Mkoani Iringa imeelezwa kuwa kuna vituo vipya vipatavyo 140 vimeongezwa.
Taarifa iliyotolewa leo Desemba 15, 2024 na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Mtibora Seleman katika Mkutano wa Tume na wadau wa uchaguzi Mkoani Iringa, imeeleza kuwa vituo vitavyotumika katika uandikishaji ni 1,367 sawa na ongezeko la vituo 140 ukilinganisha na idadi ya vituo mwaka 2019/20 ambapo kulikuwa na vituo 1,227.
Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Iringa zilizopo Manispaa ya Iringa chini ya uangalizi wa Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Mbarouk Mbarouk.
Zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura Mkoani Iringa linatarajiwa kuanza Desemba 27 na kufika tamati Januari mbili mwaka 2025 huku likiongozwa na kauli mbiu ya "Kujiandikisha kuwa Mpiga ni Msingi wa Uchaguzi Bora"
Taarifa iliyotolewa leo Desemba 15, 2024 na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Mtibora Seleman katika Mkutano wa Tume na wadau wa uchaguzi Mkoani Iringa, imeeleza kuwa vituo vitavyotumika katika uandikishaji ni 1,367 sawa na ongezeko la vituo 140 ukilinganisha na idadi ya vituo mwaka 2019/20 ambapo kulikuwa na vituo 1,227.
Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Iringa zilizopo Manispaa ya Iringa chini ya uangalizi wa Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Mbarouk Mbarouk.
Zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura Mkoani Iringa linatarajiwa kuanza Desemba 27 na kufika tamati Januari mbili mwaka 2025 huku likiongozwa na kauli mbiu ya "Kujiandikisha kuwa Mpiga ni Msingi wa Uchaguzi Bora"