Iringa: Wananchi walia kwa uchungu baada ya mgambo kuvamia na kubomoa nyumba zao saa 10 usiku

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Iringa wanalalamikia kundi la watu waliotajwa kama Mgambo kuvamia na kuvunja Vibanda, nyumba na kuharibu mali mbalimbali ikiwamo na kuvunja jiwe la msingi la CCM na kuchana picha ya Rais Samia Suluhu Hassan na Hayati Magufuli.

Zoezi hili linadaiwa kufanyika majira ya saa 10 usiku huku baadhi ya wananchi wakimtuhumu Mkurugenzi wa Halmashauri ya ya Manispaa ya Iringa Kastori Msigala kuratibu zoezi hilo.

Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa MR Bi Kalinga ameonesha kushangazwa na tukio hilo huku akidai hana taarifa yeyote kuhusu zoezi hilo la kubomoa Vibanda na uharibifu wa Mali.

"Hii ni Ajenda ya kutuchonganisha na wananchi tuonekane hatufai, wamevunja jiwe la msingi la CCM hapa na kuchana picha ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kikao chetu cha Mwisho na Mkuu wa Wilaya" tulikubaliana kwa matukio kama haya yasifanyike bila Mwenyekiti kijulishwa"

My Take:

MAMA ANATEKELEZA, CCM MITANO TENA


Your browser is not able to display this video.
 
Huyo DED nampata ni mbabe kweli kweli
 
Msigwa anasemaje au yuko na kibuyu cha asali Dodoma
 
MNahenyeka na migambo.uoga mbaya sana.tena ilikua usiku wangekuja mitaa yangu wangejuta
 
Mgambo ni extended arm tu msiwasingizie wametekeleza amri halali ...aulizwe Raisi na Waziri kama haki imetendeka...
 
Watanganyika tuache kulalamika, tuheshimu na kufuata taratibu za nchi
 
Kwa hiyo walifikiri hizo picha zilizo chanwa zingewaokoa na hiyo bomoa bomoa siyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…