Irving Wallace angeweza kuandika riwaya ya kuvutia katika Uchaguzi wa Rais wa Zanzibar

Irving Wallace angeweza kuandika riwaya ya kuvutia katika Uchaguzi wa Rais wa Zanzibar

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Uchaguzi wa Urais Zanzibar uko njiani unakuja.

Historia ya uchaguzi visiwani inazidi kupambika na kuwa ya kugusa hisia ya kila mwanafunzi wa somo la historia ya siasa za Zanzibar na Afrika.

Dkt. Hussein Mwinyi mtoto wa Rais Ali Hassan Mwinyi ni mgombea wa pili kuchukua fomu za kugombea urais wa Zanzibar kutoka koo zilizotoa rais wa Zanzibar.

Ali Karume, baba yake Sheikh Abeid Amani Karume alikuwa rais wa Zanzibar (1964 - 1972)na mwanae Amani Abeid Karume akawa rais pia (2000 - 2010)na hivi sasa mdogo wake Amani Karume, Ali Karume kachukua fomu anataka kugombea urais.

Nini sifa ya kuwa rais wa Zanzibar?

Yawezekana kuwa moja ya kigezo ni kuwa baba alikuwa rais?

Katika hali kama ile iliyopelekea Amani Karume kuwa rais, wagombea wengine ambao baba zao hawakukalia kiti cha urais wa Zanzibar wana nafasi na tegemeo gani la kuweza kuchaguliwa kugombea?

Tuje katika fikra ndani ya bongo za watoto wa marais wanaotaka na wao kama baba zao wawe marais.

Wanaijua kwa uhakika wake nguvu ya wananchi wa Zanzibar wapiga kura pale wanapokuwa peke yao ndani ya kizimba kupiga kura?

Haiyumkiniki kuwa hawajui na hawahitaji kuingia maktaba kusoma historia ya chaguzi za Zanzibar baada ya vyama vingi.

Rejea za wao kuzisoma wanazo ndani ya familia zao achilia mbali kuwa wao wenyewe siku zote wamekuwa sehemu ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Wagombea hawa watoto wa marais waliopita wanajua kinachowakabili.

Hivi inawezekana kuwa hawa watoto wa marais ikiwa watapitishwa kugombea watakuja na mbinu mpya ya kuteka nyoyo za Wazanzibari ili washinde uchaguzi kwa amani na salama?

Kuwa mtoto wa rais anaegombea urais wa Zanzibar ni mtaji kwao au ni kubebeshwa gunia zito la misumari yenye ncha kali mchana wa jua kali?

Maswali kama haya na "plot," mfano wa hizi ndizo Irving Wallace alizokuwa akitumia kuandika vitabu vilivyouzwa nakala milioni na kitabu kutengenezwa senema za kusisimua.
 
I salute you mkuu vijana na wasomi wa zamani kama wewe mnafahamu mengi sana wengi wenu ni watu wa kutegemewa na wenye uzalendo mkubwa na nchi yao
Swali je ? Kuna yeyote uliemwandaa angalau avae viatu vyako huko mbeleni? Ama na wewe kuna watu waliokutia hamasa na bado hujafikia kuwa kama wao sababu kila uchwao nao wanakuwa tofauti na Jana?

Nirudi kwenye mada huyu Hussein Mwinyi alitabiriwa kuwa rais kitambo sana kuna bwana mmoja 2014 wakati tunajadili siasa akasema huyu Jamaa lazima atakuja kuiongoza Tanzania!! Baada ya Magufuli kuchukua nchi ikaonekana 2025 kijiti atakabidhiwa huyu Mwinyi.

Kilichonishtua Leo ni kwanini kachukua fomu muda huu? Na sio 2025? Kwa nini Zanzibar ? Sio Tanzania Bara? 2025 Tanzania Bara Rais atakuwa nani?? Mdogo wake Karume kwa wakati huu anaweza kutupiliwa mbali kwa kufuata historia kwani ni mtu ambaye anaweza kuja kuleta tena hoja ya serikali Tatu na kusababisha kuvunja Muungano haya ni maono yangu binafsi## Hoja ya serikali 3 haitakiwi kuanzishwa kwa namna yeyote ile na yeyote atakaekuwa na hoja ya kuvunja muungano wa Tanganyika na Zanzibar ashitakiwe kwa kosa la Uhaini#

Sheria yeyote imewekwa kusudi itekelezwe na kupunguza uvunjwaji wa sheria husika ila kama sheria IPO na watu hawaijui Na hawaivunji sheria hiyo basi uwepo wa hiyo sheria hauna tija mpaka pale itakapovunjwa.
 
I salute you mkuu vijana na wasomi wa zamani kama wewe mnafahamu mengi sana wengi wenu ni watu wa kutegemewa na wenye uzalendo mkubwa na nchi yao
Swali je ? Kuna yeyote uliemwandaa angalau avae viatu vyako huko mbeleni? Ama na wewe kuna watu waliokutia hamasa na bado hujafikia kuwa kama wao sababu kila uchwao nao wanakuwa tofauti na Jana?

Nirudi kwenye mada huyu Hussein Mwinyi alitabiriwa kuwa rais kitambo sana kuna bwana mmoja 2014 wakati tunajadili siasa akasema huyu Jamaa lazima atakuja kuiongoza Tanzania!! Baada ya Magufuli kuchukua nchi ikaonekana 2025 kijiti atakabidhiwa huyu Mwinyi.

Kilichonishtua Leo ni kwanini kachukua fomu muda huu? Na sio 2025? Kwa nini Zanzibar ? Sio Tanzania Bara? 2025 Tanzania Bara Rais atakuwa nani?? Mdogo wake Karume kwa wakati huu anaweza kutupiliwa mbali kwa kufuata historia kwani ni mtu ambaye anaweza kuja kuleta tena hoja ya serikali Tatu na kusababisha kuvunja Muungano haya ni maono yangu binafsi## Hoja ya serikali 3 haitakiwi kuanzishwa kwa namna yeyote ile na yeyote atakaekuwa na hoja ya kuvunja muungano wa Tanganyika na Zanzibar ashitakiwe kwa kosa la Uhaini#

Sheria yeyote imewekwa kusudi itekelezwe na kupunguza uvunjwaji wa sheria husika ila kama sheria IPO na watu hawaijui Na hawaivunji sheria hiyo basi uwepo wa hiyo sheria hauna tija mpaka pale itakapovunjwa.
Tape Measure,
Ahsante sana.
Hili la kuandaa mtu kwa kweli sina jibu.

Umenishangaza unaposema kuwa fulani atachukua uongozi wa nchi.
Uongozi wa nchi unapatikana kwa kuachaguliwa katika sanduku la kura na wananchi.

Labda ungetufahamisha uwezo wa mgombea kuweza kupata kura za Wazanzibari kiasi we kuona kuwa keshashinda uchaguzi.
 
Ushindi katika chaguzi kwa wagombea wa CCM hutokana na tume pamoja na nguvu ya dola.
Huyo Hussein Mwinyi hana uwezo hata wakupata 20% ya kura Zanzibar
 
Kilichonishtua Leo ni kwanini kachukua fomu muda huu? Na sio 2025? Kwa nini Zanzibar ? Sio Tanzania Bara? 2025 Tanzania Bara Rais atakuwa nani?? Mdogo wake Karume kwa wakati huu anaweza kutupiliwa mbali kwa kufuata historia kwani ni mtu ambaye anaweza kuja kuleta tena hoja ya serikali Tatu na kusababisha kuvunja Muungano haya ni maono yangu binafsi## Hoja ya serikali 3 haitakiwi kuanzishwa kwa namna yeyote ile na yeyote atakaekuwa na hoja ya kuvunja muungano wa Tanganyika na Zanzibar ashitakiwe kwa kosa la Uhaini#

mbona unahasira sana na wanaoukosoa Muungano? Umelishwa nini mkuu?
 
Mgombea ambaye anatakwa na CCM bara ndiye huwa Rais wa Zanzibar na huchaguliwa Dodoma. Zanzibar huenda kukamilisha tu taratibu za upigaji Kura .ila Rais tayari anakuwa amechaguliwa.


Tape Measure,
Ahsante sana.
Hili la kuandaa mtu kwa kweli sina jibu.

Umenishangaza unaposema kuwa fulani atachukua uongozi wa nchi.
Uongozi wa nchi unapatikana kwa kuachaguliwa katika sanduku la kura na wananchi.

Labda ungetufahamisha uwezo wa mgombea kuweza kupata kura za Wazanzibari kiasi we kuona kuwa keshashinda uchaguzi.
 
Back
Top Bottom