Ishi kijamaa kwenye mtaa wako, na usiishi kibepari

Ishi kijamaa kwenye mtaa wako, na usiishi kibepari

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kuna baadhi ya watu huwa wanakubalika sana, kwenye mitaa wanayoishi; kutokana na kujichanganya kwao au kushiriki kwenye matukio ya hapa na pale yanayohusu mitaa waliopo.

Ila kuna wengine, wanajulikana kama vipanga; hawajulikani kama mtaani wapo ama hawapo; kutokana na kila mmoja kuishi kivyake vyake; hakuna kusemeshana au kushiriki tukio lolote linalohusu mtaa. Mtu akiingia kwake, anafunga geti lake na hataki mawasiliano na mtu wa nje hata jirani.

Kwa uoefu wa hapa na pale; nimekuja kugundua, maisha ya kijamii (kijamaa) yana umuhimu sana, hasa maeneo tulipojenga makazi (nyumba) zetu za kuishi.

Sehemu ulipojenga nyumba yako na kuishi, ni muhimu kupafanya pawe na furaha, na ili furaha iwe kubwa zaidi itakulazimu kuishi kijamaa.

Na waliofanikisha hili, watakuja na ushuhuda wa namna wanavyofurahia maisha ya hapo mtaani.

Majirani ndio wanakuwa ndugu zako wa karibu.

Inawezekana miaka yote huwa unatamani, uchanganyikane na jamii ya mtaani kwako, ila unakosa pa kuanzia.

Unaweza kubuni namna ya kuwakutanisha pamoja, mfano; kwenye matukio ya mwisho wa mwaka; unaweza ukawashawishi watoe mchango kidogo ili msherehekee kwa pamoja, kwa kuchinja mifugo n.k Na katika makutano yenu, mkaazimia baadhi ya vitu vitakavyokuwa na faida maishani mwenu.

Naamini; wote mtafurahia hiyo kukutana kwenu, na mtajiuliza siku zote mlikuwa wapi kufanya tukio la namna hiyo?​
 
Kujichanganya kupitiliza napo Kuna madhara yake, mtaani Kuna mambo mengi sana na wakati mwingine kukaa mbali kiasi na watu kunaepusha vitu Fulani,
Binafsi nashiriki vitu vya Jamii ila Ile deep socialization Bado nafikiria.
 
Kuna baadhi ya watu huwa wanakubalika sana, kwenye mitaa wanayoishi; kutokana na kujichanganya kwao au kushiriki kwenye matukio ya hapa na pale yanayohusu mitaa waliopo.

Ila kuna wengine, wanajulikana kama vipanga; hawajulikani kama mtaani wapo ama hawapo; kutokana na kila mmoja kuishi kivyake vyake; hakuna kusemeshana au kushiriki tukio lolote linalohusu mtaa. Mtu akiingia kwake, anafunga geti lake na hataki mawasiliano na mtu wa nje hata jirani.

Kwa uoefu wa hapa na pale; nimekuja kugundua, maisha ya kijamii (kijamaa) yana umuhimu sana, hasa maeneo tulipojenga makazi (nyumba) zetu za kuishi.

Sehemu ulipojenga nyumba yako na kuishi, ni muhimu kupafanya pawe na furaha, na ili furaha iwe kubwa zaidi itakulazimu kuishi kijamaa.

Na waliofanikisha hili, watakuja na ushuhuda wa namna wanavyofurahia maisha ya hapo mtaani.

Majirani ndio wanakuwa ndugu zako wa karibu.

Inawezekana miaka yote huwa unatamani, uchanganyikane na jamii ya mtaani kwako, ila unakosa pa kuanzia.

Unaweza kubuni namna ya kuwakutanisha pamoja, mfano; kwenye matukio ya mwisho wa mwaka; unaweza ukawashawishi watoe mchango kidogo ili msherehekee kwa pamoja, kwa kuchinja mifugo n.k Na katika makutano yenu, mkaazimia baadhi ya vitu vitakavyokuwa na faida maishani mwenu.

Naamini; wote mtafurahia hiyo kukutana kwenu, na mtajiuliza siku zote mlikuwa wapi kufanya tukio la namna hiyo?​
Kama mtaani kuna msiba shiriki, otherwise ishi kibepari.
Kama ni ndugu au marafiki wa kukuzika unao tayari.

Usijesema hatukukuambia

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Kushiriki matukio kama misiba na sherehe kiasi..pili usijaribu kuwafanya nao mazoea hadi kwako..mazoea yakomee kitaa tuna vijiweni.
Kwenye biashara au kazi zako usilete nao mazoea...usiwakopeshe.


#MaendeleoHayanaChama
 
Ni kwa baadhi ya mitaa..kuna mitaa mengine ukiishi kibepari unakuwa safe zaidi despite usikose Misibani na ltk shughuli za kujjitolea...otherwise ukiishi sana kijamaa wote sio wema unaweza kutengenezewa mchoro na mazingira mazuri ukaja kuibiwa vitu ndani
 
Back
Top Bottom