Ishi maisha kulingana na kipato chako

ZeeZoe

Member
Joined
Dec 29, 2018
Posts
18
Reaction score
12
Habari wanajukwaa,
Natumai mwaka tumeuanza Salama Salmini.Mwanzoni mwa mwaka mambo hua mengi baada ya mapumziko kuna Ada za Watoto kuna mambo ya Kodi na kadhalika, Inabidi kujipanga vizuri kuhakikisha mambo yanaenda sawa. Zingatia yafuatayo yatakusaidia kidogo.
*Peleka watoto shule ambayo unauwezo wa kulipa Ada yake bila matatizo. Ada kubwa sio kipimo cha ufaulu wa mtoto.
*Panga chumba/nyumba ambayo Kodi yake unaweza kuilipa bila kujitutumua sana.kuna maeneo yana nyumba nzuri na bei ni nafuu pia.
*Sio lazima uende Na fashion kila nguo inayotoka unayo.fua nguo zako ulizonazo piga pasi vizuri,chana nywele zako utapendeza tu.
*Kula mlo kamili kuhakikisha afya yako inakua Imara vitu kama mbogamboga Na matunda ya msimu si gharama sana.jilinde dhidi ya mbu waenezao malaria kuepusha kwenda hospital mara kwa mara.
*kua Na marafiki wachache wenye Maana.
*Zaidi mkumbuka Mungu kwa kufanya ibada na pia kujituma muhimu.
*Usiige maisha ya jirani Yako (hii kwa wanawake zaidi) jirani yako na wewe maisha yenu Na vipato vyenu havifanani.
Tujitahidi kuishi maisha yaliyo ndani ya mwezi wetu huku tukiendelea kupambana kutafuta pesa tuweze kuishi maisha tunayotamani hii itapunguza misongo isiyo ya lazima.Wanawake pia tukumbuke kujikinga na mimba zisizotarajiwa kuna njia nyingi za uzazi wa mpango Ahsanteni.
Heri ya mwaka Mpya.. Mbarikiwe wote!
 
madame umeongea kitu kikubwa hapa, Nakutakia mwaka mpya wenye mafanikio.
 
Unampeleka mwanao shule ya gharama , mambo yakikushinda unamleta shule ya akina Kayumba , atajisikiaje ? Kama ni kayumba kubaliana tu na hiyo hali . Don't desire for what you cannot be !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usisahau kwa wanywaji wale, kunywa kakinywaji unakokaweza kubudget, Bingwa, ndovu, Balimi, na Jidude lile....
 
Tatizo watu wengi wanapenda kutumia hela wasizonazo kugharamia vitu wasivyohitaji ili kujionyesha mbele ya watu wasio na umuhimu katika maisha yao. Na hapo ndio maisha yanapokuwa magumu.
 
Amina

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ujumbe mzuri sana, nimekuelewa vyema, napenda sana kuishi ndani ya uwezo wangu, kitu ninacho feli ni mazoezi na sala, ntajitaidi sana huu mwaka nibadilike izo sehemu mbili.
 
Tatizo watu wengi wanapenda kutumia hela wasizonazo kugharamia vitu wasivyohitaji ili kujionyesha mbele ya watu wasio na umuhimu katika maisha yao. Na hapo ndio maisha yanapokuwa magumu.
kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…