Ismael Haniyeh ni kiongozi wa mfano kuigwa na wapigania uhuru duniani

Ismael Haniyeh ni kiongozi wa mfano kuigwa na wapigania uhuru duniani

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Katika kuthamini mchango wa kiongozi mkuu wa Hamas aliyefariki, Ismael Haniyeh tunaweza kuchukua mafunzo machache katika uongozi wake.

Kutokana na huzuni ya kumpoteza kiongozi huyo sitokwenda mbali kuangalia historia yote ya maisha yake.Machache ninayoweza kuyataja ni kama ifuatavyo.

Alizaliwa mwaka 1962 na mpaka anauliwa alikuwa na miaka 62. Alizaliwa kwenye kambi ya wakimbizi huko Gaza kutokana na wazee waliohamishwa na Israel kutoka mji wa Ashkelon mwaka 1948.

Alisoma shule za msingi na sekondari huko huko Gaza na hatimae kujiunga na chuo kikuu cha kiislamu huko huko Gaza ambako alifaulu kwa kiwango cha juu katika faisihi ya lugha ya kiarabu.

Baadae alikuwa muhadhiri katika chuo kikuu hicho na kuwa karibu na muasisi wa kundi hilo,sheikh Ahmed Yasin

Akiwa na miara 25 akiwa sekondari aliwahi kuwekwa gerezani na Israel kutokana na harakati zake za kupinga uvamizi wa ardhi za Palestina unaofanywa na Israel.Aliwekwa gerezani kwa mara nyengine mbili ikiwemo kukaaa kwa miaka mitatu kabla ya kuachiwa huru akaishi Lebanon.

Alirudi Gaza mwaka 1993 na kujiunga na vuguvugu la siasa ambapo hatimae aliwahi kuwa waziri mkuu wa Palestina chini ya Fatah.Baadae mwaka 2006 Fatah ilikataa kufanya kazi na Hamas na akaondoka madarakani kurudi Gaza ambapo chama cha Hamas katika uchaguzi wa mwaka 2007 kilishinda dhidi ya fatah na kuanzisha serikali yao.

Mwaka 2019 kwa hekima za uongozi alikubaliana na makundi yanayofanya kazi Gaza kuachia uongozi na kuondoka Gaza ili kuongoza kisiasa akiwa nje ya nchi hiyo.Mpango huo ulileleta faida kubwa sana kwani walifanikiwa kuiimarisha Gaza kijeshi na kisiasa.

Katika maisha yake amenusurika mara kadhaa na majaribio ya kumuua kabla ya shambulio la juzi huko Teheran ambapo alliuliwa kutoka na shambuliwa ambaklo kwa mujibu wa Iran na Hamas yenyewe lililofanywa kwa ushirikiano wa Israel na Marekani.

Katikati ya vita vya Gaza Israel iliwauwa kwa makusudi mke,watoto na wajukuu zake wengi na baadae dada na watu kadhaa wa familia yake.Kitu cha kushangaza kwa watu wengi ni kwamba mauwaji hayo hayakumbadilisha chochote Ismail Haniye na hakufa kwa ugonjwa wa moyo wala kuacha harakati za kuitetea Palestina na wala hakulegeza misimamo dhidi ya Israel.

Pamoja na kuuliwa kwa idadi kubwa ya wapalestina na wapiganaji wake huko Gaza lakini kiongozi huyo kwa nguvu kubwa ya kiimani ya kiislamu hakuamrisha kusalimu amri kwa harakati zao za mapigano dhidi ya Israel.
Masaa machache kabla ya kuuliwa kwa shambulio la ndege huko Iran bado Ismael Haniye alionekana akiwa na afya nzuri na mcheshi japo alipatwa na misiba mingi sana katika maisha yake.

1722492835571.png

Who was Ismail Haniyeh, the Hamas political chief killed in Iran?

 
Nanukuu ''Masaa machache kabla ya kuuliwa kwa shambulio la ndege huko Iran''

Maswali
1. Ameuliwa kwa shambulio la ndege ya nchi gani?
2. Nani aliyetoa taarifa kuwa ameuwawa kwa shambulio la ndege?
3. Kama ndege ni kutoka nje ya Iran iliwezaje kufika Tehran?
 
Kama ambavyo nchi zingine za Afrika na duniani zilivyopambana Kwa mishale, bunduki na mizinga kuuondoa ukoloni wa Uingereza, Ufaransa na nk.

Palestine Ina haki ya kupambana kuonesha hawafurahishwi na ukoloni wa kiyahudi usaidiwao na Western powers. Ndio! Bila kuchoka wapalestina hawataacha kupigana dhidi ya udhalimu? Hata pakiwa na kitisho Cha wao kufutika kabisa watainua mawe, bunduki na mizinga kumuelekezea adui mwenye nguvu. Keep fighting my brothers. Israel itaikalia Palestine lakini hawataishi Kwa Raha.

Maisha Yao hapo makombora, na mabomu itakuwa na itaendelea kuwa chai, chakula Cha usiku hata chakula Cha mchana. Viva Kwa vijana wasioogopa kifo HAMAS.
 
Kama ambavyo nchi zingine za Afrika na duniani zilivyopambana Kwa mishale, bunduki na mizinga kuuondoa ukoloni wa Uingereza, Ufaransa na nk.

Palestine Ina haki ya kupambana kuonesha hawafurahishwi na ukoloni wa kiyahudi usaidiwao na Western powers. Ndio! Bila kuchoka wapalestina hawataacha kupigana dhidi ya udhalimu? Hata pakiwa na kitisho Cha wao kufutika kabisa watainua mawe, bunduki na mizinga kumuelekezea adui mwenye nguvu. Keep fighting my brothers. Israel itaikalia Palestine lakini hawataishi Kwa Raha.

Maisha Yao hapo makombora, na mabomu itakuwa na itaendelea kuwa chai, chakula Cha usiku hata chakula Cha mchana. Viva Kwa vijana wasioogopa kifo HAMAS.
Israel imechimbia kwenye handaki.Hakuna ulinzi utakaondelea kwake na hata mataifa yaliyoanza kulegeza misimamo na kutaka kurejesha uhusiano nayo kwa sasa hawatafanya tena hivyo huku wenyewe wakianza kuona kitisho kwa tawala zao kwa kukaa kimya wakati Gaza ikiangamizwa.
 
Nanukuu ''Masaa machache kabla ya kuuliwa kwa shambulio la ndege huko Iran''

Maswali
1. Ameuliwa kwa shambulio la ndege ya nchi gani?
2. Nani aliyetoa taarifa kuwa ameuwawa kwa shambulio la ndege?
3. Kama ndege ni kutoka nje ya Iran iliwezaje kufika Tehran?
Ndege za kisasa na makombora ambayo yanamilikiwa na wanyonge kama Houth si ajabu kufika Tehran kutoka Israel kama yalivyofika makombora ya Iran ndani ya Telaviv miezi mitatu iliyopita,
Kinachotakiwa ni kuacha dhulama na kuheshimiana na wala si kuoneshana ubabe.
 
Katika kuthamini mchango wa kiongozi mkuu wa Hamas aliyefariki, Ismael Haniyeh tunaweza kuchukua mafunzo machache katika uongozi wake.

Kutokana na huzuni ya kumpoteza kiongozi huyo sitokwenda mbali kuangalia historia yote ya maisha yake.Machache ninayoweza kuyataja ni kama ifuatavyo.

Alizaliwa mwaka 1962 na mpaka anauliwa alikuwa na miaka 62.Alizaliwa kwenye kambi ya wakimbizi huko Gaza kutokana na wazee waliohamishwa na Israel kutoka mji wa Ashkelon mwaka 1948.

Alisoma shule za msingi na sekondari huko huko Gaza na hatimae kujiunga na chuo kikuu cha kiislamu huko huko Gaza ambako alifaulu kwa kiwango cha juu katika faisihi ya lugha ya kiarabu.

Baadae alikuwa muhadhiri katika chuo kikuu hicho na kuwa karibu na muasisi wa kundi hilo,sheikh Ahmed Yasin

Akiwa na miara 25 akiwa sekondari aliwahi kuwekwa gerezani na Israel kutokana na harakati zake za kupinga uvamizi wa ardhi za Palestina unaofanywa na Israel.Aliwekwa gerezani kwa mara nyengine mbili ikiwemo kukaaa kwa miaka mitatu kabla ya kuachiwa huru akaishi Lebanon.

Alirudi Gaza mwaka 1993 na kujiunga na vuguvugu la siasa ambapo hatimae aliwahi kuwa waziri mkuu wa Palestina chini ya Fatah.Baadae mwaka 2006 Fatah ilikataa kufanya kazi na Hamas na akaondoka madarakani kurudi Gaza ambapo chama cha Hamas katika uchaguzi wa mwaka 2007 kilishinda dhidi ya fatah na kuanzisha serikali yao.

Mwaka 2019 kwa hekima za uongozi alikubaliana na makundi yanayofanya kazi Gaza kuachia uongozi na kuondoka Gaza ili kuongoza kisiasa akiwa nje ya nchi hiyo.Mpango huo ulileleta faida kubwa sana kwani walifanikiwa kuiimarisha Gaza kijeshi na kisiasa.

Katika maisha yake amenusurika mara kadhaa na majaribio ya kumuua kabla ya shambulio la juzi huko Teheran ambapo alliuliwa kutoka na shambuliwa ambaklo kwa mujibu wa Iran na Hamas yenyewe lililofanywa kwa ushirikiano wa Israel na Marekani.

Katikati ya vita vya Gaza Israel iliwauwa kwa makusudi mke,watoto na wajukuu zake wengi na baadae dada na watu kadhaa wa familia yake.Kitu cha kushangaza kwa watu wengi ni kwamba mauwaji hayo hayakumbadilisha chochote Ismail Haniye na hakufa kwa ugonjwa wa moyo wala kuacha harakati za kuitetea Palestina na wala hakulegeza misimamo dhidi ya Israel.

Pamoja na kuuliwa kwa idadi kubwa ya wapalestina na wapiganaji wake huko Gaza lakini kiongozi huyo kwa nguvu kubwa ya kiimani ya kiislamu hakuamrisha kusalimu amri kwa harakati zao za mapigano dhidi ya Israel.
Masaa machache kabla ya kuuliwa kwa shambulio la ndege huko Iran bado Ismael Haniye alionekana akiwa na afya nzuri na mcheshi japo alipatwa na misiba mingi sana katika maisha yake.

Who was Ismail Haniyeh, the Hamas political chief killed in Iran?

Kwenye hayo mauaji bado tu mnaamini magaidi wenu wanauwezo wakupambana israel mimi naona mnapambana na israel ili mfe tu mje mlalamike
 
Gaidi is no more
Gaidi kwako lakini ni mpigania uhuru kuliko wapigania uhuru unaowajua wewe.
Katika historia ya Palestina wameshauliwa wengi sana na hakuna dalili kuwa mbinu ya kuuwa wanaharakati imeisaidia Israel kupata utulivu inaoutaka hapo mashariki ya kati,
 
Ismail Haniyeh alikuwa mzalendo aliyeuawa akiipigania nchi yake, nimeumia sana juu ya kifo chake. Mungu aliangazie nuru kaburi lake, Amen.

Naikumbuka video fupi wakati akipewa taarifa ya kuuawa kwa wanawe pamoja na wajukuu zake mwezi June, alinigusa ambavyo alibaki kuwa imara licha ya kupewa taarifa ngumu.

Nimejifunza kwake kubaki katika njia ya mapambano licha ya vikwazo, uimara ndio nyenzo kuu katika mapambano.
 
Ndege za kisasa na makombora ambayo yanamilikiwa na wanyonge kama Houth si ajabu kufika Tehran kutoka Israel kama yalivyofika makombora ya Iran ndani ya Telaviv miezi mitatu iliyopita,
Kinachotakiwa ni kuacha dhulama na kuheshimiana na wala si kuoneshana ubabe.
You are right, mataifa yaache dhuluma na yaheshimiane.

Jambo la pili, kuna kutuma kombora likafika popote bila kuwa na target maalum ya madhara, hili lililomuua Haniyeh, kama lilikuwa kombora basi lilikuwa na target maalumu kwa mtu maalumu. Hapa maswali ni mengi, Haniyeh alikwenda Tehran, ilikuwaje waliopanga shambulizi kuwa ''precise'' kwa kiwango hichi? Hapa analyst wa Al-jazeera akasema;
Al Jazeera’s Defence Editor Alex Gatopoulos says the intelligence used to locate and assassinate Haniyeh “suggests the possible help of the US”. “Intelligence is key. Any weapon in the world is only as good as the intelligence that guides it. It can be as accurate as it likes,” Gatopoulos said.

Sababu ya kuuliza ni kwa sababu naona kama taarifa ya nini kilichotokea ama aliuliwa kwa kitu gani zimekuwa nyingi kiasi.

1. Al-jazeera - ''...At around 2am local time (22:30 GMT) on Wednesday, Haniyeh was killed by an “airborne guided projectile.” His bodyguard was also killed..''

Sawa ba Nournews

2. NourNews, an outlet affiliated with Iran's Supreme National Security Council, said Haniyeh's residence was hit by an airborne projectile. The assassination was "a dangerous gamble to undermine Tehran's deterrence", it said.
 
Gaidi kwako lakini ni mpigania uhuru kuliko wapigania uhuru unaowajua wewe.
Katika historia ya Palestina wameshauliwa wengi sana na hakuna dalili kuwa mbinu ya kuuwa wanaharakati imeisaidia Israel kupata utulivu inaoutaka hapo mashariki ya kati,
Uhakika. Wamekufa wengi sana akina Arafat, shekh Yassin na wengine makumi kama viongozi wa harakati za mapambano lakini pia wamekufa wapiganaji wa kipalestina maelfu lakini Wala hata dalili ya wao ( Palestine) kumuachia nafasi adui japo ya kuinjoy maisha angalau Kwa wiki bila kombora kwenye miji ya adui haijawahi kutolewa. Wayahudi huishi Kwa wasiwasi muda wote mara kutoka Lebanon mara Syria mara Houth mara hamas. Na itakuwa hivyo dahari Kwa dahari
 
Nanukuu ''Masaa machache kabla ya kuuliwa kwa shambulio la ndege huko Iran''

Maswali
1. Ameuliwa kwa shambulio la ndege ya nchi gani?
2. Nani aliyetoa taarifa kuwa ameuwawa kwa shambulio la ndege?
3. Kama ndege ni kutoka nje ya Iran iliwezaje kufika Tehran?
swali la tatu ni la kipuuzi
 
Ismail Haniyeh alikuwa mzalendo aliyeuawa akiipigania nchi yake, nimeumia sana juu ya kifo chake. Mungu aliangazie nuru kaburi lake, Amen.

Naikumbuka video fupi wakati akipewa taarifa ya kuuawa kwa wanawe pamoja na wajukuu zake mwezi June, alinigusa ambavyo alibaki kuwa imara licha ya kupewa taarifa ngumu.

Nimejifunza kwake kubaki katika njia ya mapambano licha ya vikwazo, uimara ndio nyenzo kuu katika mapambano.
Sawa
 
Ismail Haniyeh alikuwa mzalendo aliyeuawa akiipigania nchi yake, nimeumia sana juu ya kifo chake. Mungu aliangazie nuru kaburi lake, Amen.

Naikumbuka video fupi wakati akipewa taarifa ya kuuawa kwa wanawe pamoja na wajukuu zake mwezi June, alinigusa ambavyo alibaki kuwa imara licha ya kupewa taarifa ngumu.

Nimejifunza kwake kubaki katika njia ya mapambano licha ya vikwazo, uimara ndio nyenzo kuu katika mapambano.
Aamina
 
Uhakika. Wamekufa wengi sana akina Arafat, shekh Yassin na wengine makumi kama viongozi wa harakati za mapambano lakini pia wamekufa wapiganaji wa kipalestina maelfu lakini Wala hata dalili ya wao ( Palestine) kumuachia nafasi adui japo ya kuinjoy maisha angalau Kwa wiki bila kombora kwenye miji ya adui haijawahi kutolewa. Wayahudi huishi Kwa wasiwasi muda wote mara kutoka Lebanon mara Syria mara Houth mara hamas. Na itakuwa hivyo fahari Kwa dahari
Sasa ndio itakuwa hali mbaya zaidi kwao.Kwa kujua silaha kama droni zinamilikiwa na mataifa mengi na kila nchi imeamka kufundisha vijana wake kusomea coding na kuchakata semiconductors.
Mfano hao Hamas hata wakiondoka viongozi wao wakuu vijana wako makini sana na matumizi ya teknolojia za kisasa.Achana na wajinga kama Saudia.
 
Back
Top Bottom