Ismail Jussa na mchanganyiko wa Ton Ton Macoute na Gestapo

Ismail Jussa na mchanganyiko wa Ton Ton Macoute na Gestapo

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Screenshot_20201210-233019.jpg



POSTA HIZI ZINASEMA NINI KUHUSU ZANZIBAR?

Nimeitazama picha ya Ismail Jussa akipokelewa uwanja wa ndege Zanzibar akitokea Nairobi kwenye matibabu.

Ismail yuko kwenye kiti cha magurudumu.
Yaliyomsibu sote tunayajua.

Unaweza kusema ni mchanganyiko maalum wa Ton Ton Macoute na Gestapo.

Nikimwangalia Jussa akiombewa dua vidole vikawa vinaniwasha niandike kitu kuhusu yeye.

Nikajiwa na fikra ya kiasi ya miaka 10 iliyopita wakati wa SUK na niko Zanzibar wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2010.

Nilipiga picha moja ya posta tatu za kampeni ikiwaonyesha vijana watatu wa Kizanzibari wakigombea nafasi kupitia CCM na CUF.

Katika hawa vijana watatu wawili nikifahamiana nao - Cholo Mughery na Jussa.

Licha ya kuwajua hawa wagombea posta zile zilikuwa zimebeba ujumbe mzito sana katika historia ya Zanzibar.

Hii ndiyo sababu nikapenda kuwa na picha hii.

Msomaji wangu tafadhali angalia posta hizi za uchaguzi wa mwaka wa 2010 kisha uniambie wewe unaona nini katika hizi posta na zinakupa ujumbe gani?

Picha inaongea maneno elfu moja.
 
Hatujakuelewa Mohamed Said fungua hiyo code
Muda...
Angalia hizo posta tatu za hawa vijana wa Kizanzibari.

Wote wamechanganya damu lakini wote ni Wazanzibari.

Bahati mbaya sana kuna watu hawawataki walichanganya damu.
Wanadai kuna kabila Zanzibar inaitwa, ''Waafrika.''

Hawa wanadai wao ndiyo Wazanzibari.
 
Muda...
Angalia hizo posta tatu za hawa vijana wa Kizanzibari.

Wote wamechanganya damu lakini wote ni Wazanzibari.

Bahati mbaya sana kuna watu hawawataki waliochanganya damu.

Wanadai kuna kabila Zanzibar inaitwa, ''Waafrika.''

Hawa wanadai wao ndiyo Wazanzibari.
Picha
Screenshot_20201211-002634.jpg
 
Mzee kachanganyikiwa na mambo yake ya uarabu na udini, kuliko hata waarabu wenyewe
Tangawizi,
Huwa kawaida nionapo mtu ananitambulisha kwa umri wangu najua kaghadhibika basi nachukua tahadhari.

Nikisoma "Mzee," najua hiyo ni shari.
Ungeweza kuandika, "Mzee Mohamed."

Hii ingeonyesha heshima na adabu kwangu.
 
Tangawizi,
Huwa kawaida nionapo mtu ananitambulisha kwa umri wangu najua kaghadhibika basi nachukua tahadhari.

Nikisoma "Mzee," najua hiyo ni shari.
Ungeweza kuandika, "Mzee Mohamed."

Hii ingeonyesha heshima na adabu kwangu.
ukichanganya damu inakusaidia nini wewe?
 
Nitashangaa sana Kama atakuwa na yeye kula kiapo

Kwa hio Hali aliyonayo

Nitashangaa sana
 
Uyo ni yule jussa walitoleanaga maneno na yule mama wakati wa katiba mpya
 
Kinacho wasumbua wale ndio kile kile kinacho mtatiza huyu!

Ila kuna wajanja na wengine ..maboya.... .

Akili kumkichwa... . .. na fitna ni mbaya akheri ya mchawi... .. na kuna kauli na maneno yatayokuja kuwaumbua watu. .. hata iwe kwa miaka iyami...!

Kujua ukweli na kuuishi... ni vitu viwili tofauti...

Njaa mwanamme bwana... ..acha maskhara...!

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
View attachment 1646616


POSTA HIZI ZINASEMA NINI KUHUSU ZANZIBAR?

Nimeitazama picha ya Ismail Jussa akipokelewa uwanja wa ndege Zanzibar akitokea Nairobi kwenye matibabu.

Ismail yuko kwenye kiti cha magurudumu.
Yaliyomsibu sote tunayajua.

Unaweza kusema ni mchanganyiko maalum wa Ton Ton Macoute na Gestapo.

Nikimwangalia Jussa akiombewa dua vidole vikawa vinaniwasha niandike kitu kuhusu yeye.

Nikajiwa na fikra ya kiasi ya miaka 10 iliyopita wakati wa SUK na niko Zanzibar wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2010.

Nilipiga picha moja ya posta tatu za kampeni ikiwaonyesha vijana watatu wa Kizanzibari wakigombea nafasi kupitia CCM na CUF.

Katika hawa vijana watatu wawili nikifahamiana nao - Cholo Mughery na Jussa.

Licha ya kuwajua hawa wagombea posta zile zilikuwa zimebeba ujumbe mzito sana katika historia ya Zanzibar.

Hii ndiyo sababu nikapenda kuwa na picha hii.

Msomaji wangu tafadhali angalia posta hizi za uchaguzi wa mwaka wa 2010 kisha uniambie wewe unaona nini katika hizi posta na zinakupa ujumbe gani?

Picha inaongea maneno elfu moja.

Mzee Mohamed Said,
Kwanza nikupongeze kwa kuandika na kupenda kuandika.
Binafsi nikuwa sijaelewwa maneno hay Ton ton macoute na ikabidi niende kwa mwalimu google.
Binafsi nimekuelewa!!
 
Muda...
Angalia hizo posta tatu za hawa vijana wa Kizanzibari.

Wote wamechanganya damu lakini wote ni Wazanzibari.

Bahati mbaya sana kuna watu hawawataki walichanganya damu.
Wanadai kuna kabila Zanzibar inaitwa, ''Waafrika.''

Hawa wanadai wao ndiyo Wazanzibari.
Wote ni ndugu tofauti ni rangi za mashairt tu
 
Back
Top Bottom