5523
JF-Expert Member
- Nov 13, 2014
- 2,275
- 2,410
Wakuu,
Israel itakata rufaa kupinga hati ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na waziri wa zamani wa ulinzi Yoav Gallant.
Majaji wiki iliyopita walitoa vibali kwa watu hao wawili pamoja na kamanda wa kijeshi wa Hamas Mohammed Deif, wakisema kuna sababu za kuridhisha za kuamini kuwa watu hao watatu waliwajibika kwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu huko Gaza.
Serikali ya Israel, pamoja na Netanyahu na Gallant, walikanusha vikali shutuma hizo.
Siku ya Jumatano, ofisi ya waziri mkuu ilisema ilikuwa imefahamisha ICC kuhusu "nia yake ya kukata rufaa mahakamani pamoja na kutaka kuzuia utekelezaji wa hati za kukamatwa".
Ofisi ya Netanyahu pia ilisema Seneta wa Marekani Lindsey Graham amemjulisha Netanyahu "juhudi anazoendeleza katika Bunge la Marekani dhidi ya ICC na nchi ambazo zimeshirikiana nayo".
Rais wa Marekani Joe Biden alitaja hati hizo kuwa za "chukizo" wiki iliyopita. "Chochote ICC inaweza kumaanisha, hakuna usawa kati ya Israel na Hamas. Daima tutasimama na Israel dhidi ya vitisho kwa usalama wake," alisema.
Nchi wanachama wa ICC, ambazo hazijumuishi Israel au Marekani , zinalazimika kuchukua hatua katika kumzuia mshtakiwa anayesakwa iwapo atapatikana kuwa katika mamlaka yao.
Baadhi ya nchi za Umoja wa Ulaya zimedokeza kuwa zitaheshimu uamuzi wa ICC, huku nyingine zikikataa kusema zitafanya nini iwapo Netanyahu ataingia katika eneo lao.
Serikali ya Uingereza imedokeza kuwa Netanyahu atakamatwa iwapo atasafiri kwenda Uingereza.
Source: BBC Swahili
Israel itakata rufaa kupinga hati ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na waziri wa zamani wa ulinzi Yoav Gallant.
Majaji wiki iliyopita walitoa vibali kwa watu hao wawili pamoja na kamanda wa kijeshi wa Hamas Mohammed Deif, wakisema kuna sababu za kuridhisha za kuamini kuwa watu hao watatu waliwajibika kwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu huko Gaza.
Serikali ya Israel, pamoja na Netanyahu na Gallant, walikanusha vikali shutuma hizo.
Siku ya Jumatano, ofisi ya waziri mkuu ilisema ilikuwa imefahamisha ICC kuhusu "nia yake ya kukata rufaa mahakamani pamoja na kutaka kuzuia utekelezaji wa hati za kukamatwa".
Ofisi ya Netanyahu pia ilisema Seneta wa Marekani Lindsey Graham amemjulisha Netanyahu "juhudi anazoendeleza katika Bunge la Marekani dhidi ya ICC na nchi ambazo zimeshirikiana nayo".
Rais wa Marekani Joe Biden alitaja hati hizo kuwa za "chukizo" wiki iliyopita. "Chochote ICC inaweza kumaanisha, hakuna usawa kati ya Israel na Hamas. Daima tutasimama na Israel dhidi ya vitisho kwa usalama wake," alisema.
Nchi wanachama wa ICC, ambazo hazijumuishi Israel au Marekani , zinalazimika kuchukua hatua katika kumzuia mshtakiwa anayesakwa iwapo atapatikana kuwa katika mamlaka yao.
Baadhi ya nchi za Umoja wa Ulaya zimedokeza kuwa zitaheshimu uamuzi wa ICC, huku nyingine zikikataa kusema zitafanya nini iwapo Netanyahu ataingia katika eneo lao.
Serikali ya Uingereza imedokeza kuwa Netanyahu atakamatwa iwapo atasafiri kwenda Uingereza.
Source: BBC Swahili