Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Klabu ya Simba Sc imethibitisha kuridhia ombi la mchezaji Israel Mwenda kuondoka klabuni hapo baada ya nyota huyo kudai kuwa amepata timu nyingine
Taarifa ya Wekundu hao wa Msimbazi imebainisha kuwa nyota huyo alisaini mkataba mpya wa miaka miwili lakini kabla ya kuanza kuutumikia, aliandika barua ya kuondoka kwa madai ya kuwa amepata timu sehemu nyingine.
“Simba kwa kujali na kuheshimu maslahi ya mchezaji ilimpa sharti la kurejesha fedha zote na tayari amerejesha. Simba ina thamini mchango wa Israel katika miaka yote mitatu aliyodumu nasi.
“Uongozi wa klabu unamtakia kila la kheri katika maisha yake mapya ya soka.” imesema Simba Sc
Taarifa ya Wekundu hao wa Msimbazi imebainisha kuwa nyota huyo alisaini mkataba mpya wa miaka miwili lakini kabla ya kuanza kuutumikia, aliandika barua ya kuondoka kwa madai ya kuwa amepata timu sehemu nyingine.
“Simba kwa kujali na kuheshimu maslahi ya mchezaji ilimpa sharti la kurejesha fedha zote na tayari amerejesha. Simba ina thamini mchango wa Israel katika miaka yote mitatu aliyodumu nasi.
“Uongozi wa klabu unamtakia kila la kheri katika maisha yake mapya ya soka.” imesema Simba Sc