Uchaguzi 2020 It is a fait accompli


CCM inafuata rules za political contest za wachina.

1) ukikaribia wakati wa contest unatakiwa umchukie opponent wako kuliko sumu ya cynide.

2) Usimtafutie silaha ya kimo chake, tumia silaha ambayo ya mwisho na kubwa na yenye kufanya uharibifu kuliko silaha zote unazo zimiliki

3) Lazima ujitayarishe sana kama contest hiyo na usitoe nafasi yeyote ile ya kushindwa. Na ikitokea kashindwa basi uhai wake kisiasa upotee. Na kushindwa kwako ujue uhai wako kisiasa unapotea.

4) Mashambulizi yawe ya mazito sana ya muda mfupi with precision ambayo yatamuingia mwilini yote.

5) Katika contest hiyo kipigo hicho kiwe cha kummaliza na kummvuruga, na lazima kimuingie sawa sawa kiasi asijitambue.
Na ikitokea akapona basi lazima awe amechakaa sana hata achukue muda kuanza kupumua. Na hata akiweza kujikusanya lazima awe na hali mbaya kiasi akirudisha shambulizi liwe hafifu sana kiasi haliwezi kukudhuru.

6) Uhakikishe udhaifu uliomuingizia mwilini mwake uwe umenyong'onyea kwa maisha yake yote ya kisiasa na awe anaogopa political contest siku yeyote ile aambiwapo anapambana na wewe.
 
Yaani politics zetu za vyama vingi ni utoto tu, bora kureset na kuanza upya. Nikikumbuka vyama vyenyewe namna vilivyoanza eti vilihitaji support ya serikali (kupitia ruzuku) ili kuviimarisha.

Seriously? Yaani chama kilicho madarakani kikubali kuwapa support mahasimu wake ili mahasimu wapate nguvu ya kukishinda? Na hilo ndilo lililosababisha utitiri wa vyama maana kila chama kilitegemea ruzuku serikalini.

Ni upuuzi mtupu. Maana ukiachilia kwamba wenye vyama vyao kutumia ruzuku kama ujasiriamali fulani, haiingii akilini kwa nchi zetu hizi zisizo na uchumi mkubwa kutumia mabilioni ya pesa kila mwezi (kodi za watu maskini) kusustain makundi ya watu. Vyama vya siasa vinapaswa kuwa grassroot movements, na vinapaswa kuwa sustained na wanachama wenyewe iwapo hao wanachama watashawishika na nia, dira na malengo yaliyokianzisha chama.

CCM (kabla yake TANU) ina advantage ya kwamba ilianzishwa kwa nia njema kabisa (kujitawala kutoka kwa wakoloni), na kwa bahati njema waanzilishi wake walikuwa wameshiba kimaono, kimikakati na kidira. Na bado hiki chama kinatembelea nyota za waanzilishi wake.

Sasa ni nini kilichosukuma kuanzishwa kwa Chadema, au CUF, au NCCR? Kwamba tunahitaji mabadiliko tofauti na CCM haiwezi kuwa hoja ya yenye mashiko, maana ni kweli watu wanataka mabadiliko lakini kama tutabadilisha lazima tuwe na uhakika kwamba tunaweka kitu bora zaidi. Demokrasia ndani ya vyama inawashinda seuze kuongoza nchi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…