IT WA Mwananchi communications vipi?

IT WA Mwananchi communications vipi?

mperwa

Member
Joined
Sep 3, 2009
Posts
28
Reaction score
0
Ni zaidi ya miezi miwili sasa , kila nikijaribu kutembelea website ya the citizen ile sehemu ya JOBS na TENDERS, nakutana na post za tangu june, Ina maana hao watu hawajui tatizo hilo au wanaamua tu kuiacha hivyo? na kama labda hao ma IT wana uzembe fulani vipi kuhusu hao mabosi wao? ina maana hawajaliona hilo?
Hata kusoma gazeti online inakuwa shida kabisa, hawapo fasta katika kuweka updates zao, kama vipi bora wangeachana na website maana badala ya kuwatangaza inakuwa inadissapint customers kutokana na huduma kutokuwa vizuri online.
 
Ndugu yangu makampuni na shule hata vyuo vingi huku kwe2 hili ni tatizo kubwa.
Wao hufkiria kuwa na website ni hatua kubwa technologically, suala la kuzi-update wanaona si muhimu kabisa. Mi huwa nachoka niki-visit websites za makampuni hapa kwe2 nchini. Kaazi kwelikweli
 
Kuhusu board hapo kuna element za uzembe na kutoipa priority website, inaonekana wanaona website ni more of a liability than an asset. Overall, even with the belowsaid, I think the original acusations have a nugget of truth because I remember the site had a nagging virus pproblem for some time.Actually the demise of Mwananchi boards and to an extent YoungAfrican.com contributed a lot to JFs success.


Kuhusu habari, hili swala tumeshalizungumza hapa, na pengine kumrukia "IT wa Mwananchi" ni kurukia hitimisho.

Magazeti ya Tanzania yenye content online yana face a dilemma in that wakiweka habari online mauzo ya magazeti yanapungua sana.Hili si mimi nanyesema, hata mimi nilikuwa sijui wakaja wenyewe kusema hapa (tunao watu wa magazeti kibao humu).Tatizo ni kwamba teknolojia yetu inaendelea kwa kasi kubwa kuliko uchumi wetu. Katika nchi zilizoendelea - ambako nako kuna mjadala mkubwa kuhusu kuanza ku charge watu ili waweze kupata online content- magazeti hutumia model ya kupata fedha kutoka matangazo ya biashara, nchini mwetu model hii haiwezi kufanya kazi kutokana na audience na "circulation" ya internet Tanzania kuwa ndogo.

Kwa hiyo kama kuna tatizo, huususan kuhusu habari, si kwa nini hawa watu hawaweki habari mtandaoni, bali kwa nini wameshindwa kuli articulate hili tatizo kwa watu, pengine suluhisho lililo uniquely Tanzanian -kama lilivyo tatizo- lingeweza kupatikana.
 
Back
Top Bottom