Game Theory, ili nisiende nje ya mada naomba kuelimishwa kabla ya kuanza kuchangia, hiyo Red Phone ni ya kazi gani hasa? Ni ya rais kuitumia tu kuwapigia watu simu, ni ya rais kuitumia tu kupokea simu alizopigiwa au anaitumia rais tu kupiga na kupigiwa simu? Ina extension za kwenda kwa wasaidizi wake wengine? Usinione ni mbumbumbu, naonmba kupata elimu. Mwisho, hiyo sinema fupi inayoandamana na maandiko yako ikionyesha hao warumi wanaokatana miguu, vichwa na mikono inatisha, yaweza athiri kisaikolojia baadhi ya wasomaji wa JF; sijui kama waweza kuiondoa!! Samahani kwa usumbufu, mimi Mama Mdogo aka dada yako. Ni hayo tu.