Its My Wedding Annivesary

Its My Wedding Annivesary

RealMan

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2010
Posts
2,367
Reaction score
1,394
Wana JF nimeona nisikae kimya bila kuwajuza wema wa Mungu kwangu.

Najua wengine mtakuwa mmevaa kijani/njano kusherekea "chama chetu cha mapinduziiii chajenga nchi" (itikia ni wimbo) huku wengine (pengine) mmevaa nguo nyeusi kuashiria maombolezo kitaifa.

Leo ninatimiza miaka 11 toka nimekula kiapo cha kuishi (kama mume na mke) na huyu mdada.
Tulikutana 1994 na ndoa ikafungwa miaka 6 baadae
Ndani ya miaka hii 11 Mungu kanijalia kuwa baba wa boy-10 na girl-7 na ukiwaangalia ni dhahiri hakunichakachua labda awe amechakachua na mdogo wangu, hahaahahaaa!!!

Ni miaka ya kuishi na mwanamke ambaye alichukua nafasi ya mama na dada yangu katika maisha.

Miaka 11 imenifundisha nisimwamini kila mtu ninaposigana na mke wangu. Nakumbuka in our early years niliwahi kushare na mchungaji juu ya tofauti zangu na mke wangu only for the pastor to use my story in his preaching the next sunday. Siku hizi nayasovu mwenyewe tu, no outsiders!

Miaka 11 ya kutambua kwamba vitu vidogo sana (thanks, sorry, karibu, darling..) vinajenga uhusiano na vitu vidogo pia huwasha moto.

Jamani wakati mwenzenu nashereheka 11 years kuna experience zipi (nzuri/mbaya/vituko) umewahi pitia kwenye mahusiano yako.

Karibuni tuzungumze!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hongera mkuu.

Mi nna aka 10 ya ndoa. Ikifika 14/10 ntaifikia rekodi yako...tuombe Mungu.

Nlistuka kidogo ulivosema boy-10, girl 7....nikajua mzee una totoz 17! LOL

Kila la heri mkuu
 
Hongera mkuu.

Mi nna aka 10 ya ndoa. Ikifika 14/10 ntaifikia rekodi yako...tuombe Mungu.

Nlistuka kidogo ulivosema boy-10, girl 7....nikajua mzee una totoz 17! LOL

Kila la heri mkuu

Hahahahaaaaaaa Totoz 17 sina ubavu huo

Asante sana Mkuu. Miaka inavyokwenda muda si mrefu tutakaribishwa kutoa nasaha kwenye send off au harusi.

Its just like yesterday!!!!!!
 
Hongera mkuu mimi ndo kwanza nina miaka minne(4) ya ndoa lakini mambo yanakwenda sawa, Mungu jalia.

Umenichekesha kwamba Mchungaji alitumia matatizo yako uliyomsimulia kama sehemu ya mahuburi Jpili iliyofuata. Lakini usijali pengine yaliokoa na kurekebisha wanandoa wengine.
 
Mkuu hongera sana!
ninamiaka kama 8 kukufikia mkuuu!
HONGERA SANA MKUU!
 
Hongera mkuu, miaka 11 ya ndoa sio kazi ndogo! Ni wazi utakuwa umepitia ups and downs nyingi sana. Nakutakieni maisha marefu na mafanikio zaidi katika ndoa yenu.
 
Hongera sana mkuu, Mungu azidi kukupigania na kuwatunza, Tuombee na sisi masingle tusije angukia mikononi mwa wanyanganyi!!
 
Congratulations RealMan.....hapo si padogo wengi huwa hawafiki hapo

kama ni gari basi tunaweza sema kwa sasa mpo comfortably kwenye overdrive, au kama ni ndege basi mpo kwenye Autopilot sehemu za kash kash zimeshapita

Again keep it up
 
Hongera mkuu mimi ndo kwanza nina miaka minne(4) ya ndoa lakini mambo yanakwenda sawa, Mungu jalia.

Umenichekesha kwamba Mchungaji alitumia matatizo yako uliyomsimulia kama sehemu ya mahuburi Jpili iliyofuata. Lakini usijali pengine yaliokoa na kurekebisha wanandoa wengine.

Safi sana mkuu, 4yrs si mchezo.

Nilikuwa embarrassed kwa kufanya nionekane hakuna harmony kwenye ndoa.
Later nikatambua baadhi ya wanawake hu-behave tofauti wanapokuwa na mimba.

Ni kweli kabisa inawezekana wapo waliosaidika maana Mungu ana njia nyingi za kutusaidia binadamu.
 
Hongera mkuu, miaka 11 ya ndoa sio kazi ndogo! Ni wazi utakuwa umepitia ups and downs nyingi sana. Nakutakieni maisha marefu na mafanikio zaidi katika ndoa yenu.

Ups and Downs tumezipitia kwa kweli.

Ujauzito wake wa kwanza was like hell to me, she was too moody.
Kaka nimewahi kuamka saa 8 usiku nikatafute kuku wa kuchoma, mwanaume nikaingia mtaani!!
 
Hongera sana mkuu, Mungu azidi kukupigania na kuwatunza, Tuombee na sisi masingle tusije angukia mikononi mwa wanyanganyi!!

May God grant the desires of your heart.

Ni kweli siku hizi hujui binadamu ni yupi na nyang'au ni lipi.
 
Congratulations RealMan.....hapo si padogo wengi huwa hawafiki hapo

kama ni gari basi tunaweza sema kwa sasa mpo comfortably kwenye overdrive, au kama ni ndege basi mpo kwenye Autopilot sehemu za kash kash zimeshapita

Again keep it up

Asante sana Kaizer!!

Ukweli ni kwamba sasa tumefahamiana vya kutosha.
I can predict her next move.. Kwa sasa tuko kwenye kipindi muhimu ambacho watoto wanajifunza kutoka kwetu.
Its a moment unauhisi upendo ndani ya nyumba yako.

Tuna kanuni moja ambayo hatuivunji siku zote "Dont Yell in front of Kids"
 
Hongera na daima mdumu ktk ndoa yenu,
Mh mi bado nachungulia nianzie mguu gani kuungana kwenye chama chenu, searching kidogo mkuu.
 
Hongera na daima mdumu ktk ndoa yenu,
Mh mi bado nachungulia nianzie mguu gani kuungana kwenye chama chenu, searching kidogo mkuu.

Asante mkuu!

Ni maombi yetu pia kwamba ambao processor bado zinascan basi mpate the right partners.
Adam na Eva wenyewe hawakuwa perfect ila walifanana.

Kambi hii ni kutamu sana, mkielewana mnatengeneza paradise yenu hapa duniani lakini it can also be more than hell msipochanga karata vizuri.
Changamoto zipo lakini thats what we were created for ili kukabiliana nazo!!!!!
 
Ups and Downs tumezipitia kwa kweli.

Ujauzito wake wa kwanza was like hell to me, she was too moody.

Kaka nimewahi kuamka saa 8 usiku nikatafute kuku wa kuchoma, mwanaume nikaingia mtaani!!

hongera sana mkuu na pole kwa masahibu uliokumbana nayo kwa muda huo wa miaka 11.
 
hongera sana mkuu na pole kwa masahibu uliokumbana nayo kwa muda huo wa miaka 11.

Asante JN,

Masaibu ktk uhusiano hayakosekani lakini uzuri wake ni kwamba yanawa-bond kila mkiyashinda.
 
Funny Stuff:

Moja ya funny stuff kwenye ndoa yangu ni pale Boy (now 10yrs) hakuweza kuniita baba until when he was 5yrs.

Alikuwa akiniita "Dear" thinking ndio jina langu kwa vile mama yake hulitumia kuniita.
 
Hongera sana mkuu.
Sina mengi ya kusema maana
mimi ndo kwanza nina miezi 8 kwenye hiyo club.
Nawatakia siku njema.
 
Back
Top Bottom