Iwapo kina TANROADS tunawanyima Creme de la Creme na kuwapa PPPs, Je watapata wapi Pesa na Vyanzo vya kumaintain Makombo ?

Iwapo kina TANROADS tunawanyima Creme de la Creme na kuwapa PPPs, Je watapata wapi Pesa na Vyanzo vya kumaintain Makombo ?

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Kwanza kabisa sio kwamba napinga PPPs, bali kwenye huduma ambazo hazina alternative ni vema likafanywa na UMMA kwa gharama ambayo itakuwa ni affordable, ukizingatia ni huduma, unapomuongezea raia gharama za TOLL wakati bado analipa Kodi nyingine ni kumtwisha mzigo mkubwa (pia hana alternative) vilevile bora kama hio TOLL ingekuwa inakwenda kwenye maintanance na kugharamia huduma nyingine na sio faida za wachache...

Sasa hivi karibuni nimesikia barabara ya Tanga kutoka Bandarini ambayo wamesema ni muhimu sana na ni potential ya kuweza kupata faida.., sasa kama ndivyo kwanini kina TANROADS au Taasisi ya UMMA isifanye ili hio faida ya ziada isiende kujenga nyingine ?

Hizi PPPs kwanini tusizipeleke huko kwenye alternatives au luxury au ambapo hatuna mpango wa kuboresha au hakuna wateja tayari ?

Ukiniambia Gharama na Serikali haina Pesa..., Nitakuuliza...

 
Back
Top Bottom