Jack patrick chupuchupu auwe mtu

Jack patrick chupuchupu auwe mtu

MaxShimba

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2008
Posts
35,771
Reaction score
4,065
jack+1.jpg
STAA wa Bongo anayetesa kwenye mitindo, Jacqueline Patrick anakabiliwa na msala wa kumtwanga na chupa nusu kumuua mrembo anayejulikana kwa jina la Hafsa Sasya,
Habari zilizopenyezwa na chanzo chetu kutoka eneo la tukio zinasema kwamba, ishu ilitokea usiku wa kuamkia Jumamosi ya Januari 26, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Elements Lounge uliopo Masaki, Dar.
CHANZO KINATIRIRIKA
Huku sharti la kutotajwa jina lake likisisitizwa na chanzo hicho, kilisema: “Unajua yule dada (Hafsa) anasoma Kurasini na anaishi Kijitonyama, namfahamu vizuri sana. Walipokutana na Jack pale ukumbini palitokea kutokuelewana kidogo.
“Baada ya muda hali ikawa sawa, watu wakajua yamekwisa. Jack akaenda zake chooni, aliporudi alikuwa na chupa na kwenda kumpiga nayo Hafsa. Mabaunsa wakamwondoa Jack ukumbini na kumwingiza Hafsa kwenye gari lake kwa lengo la kumpeleka hospitalini. Kilichoendelea hapo sijui.”

PEKUPEKU ZETU
Mwandishi wetu aliingia mzigoni rasmi na kuanza kuichimba kwa kina habari hiyo ambapo alipata uhakika wa kutokea kwa tukio hilo na Jack kufikishwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay ambapo alifunguliwa kesi yenye jalada namba OB/RB/1678/13 KUJERUHI.
Baada ya kujiridhisha kwa hilo, zoezi lililofuata lilikuwa ni kuwatafuta wawili hao ili waeleze wanachokijua kuhusu tukio hilo. Wa kwanza kupatikana alikuwa ni Jack.

KAULI YA JACK
“Ni kweli kulitokea ugomvi siku ile...na ni kweli nilihojiwa na Polisi wa Kituo cha Oysterbay, lakini nimetoka kwa dhamana na kesi imekwenda mahakamani.”

HUYU HAPA HAFSA
“Mimi na Jack tulikuwa marafiki lakini nashangaa amenipiga na chupa bila sababu. Nimeshonwa nyuzi tatu. Siku ile alinikuta nimesimama na rafiki yangu mara akanipiga kikumbo kisha akaenda chooni, aliporudi akanikumba tena, nilipomuuliza ikawa kosa; akanipiga na chupa.
“Imeniuma sana maana amenipa jeraha usoni mwangu bila sababu ya msingi, maana sina ugomvi naye. Kwa sababu hili suala lipo mikononi mwa sheria, naamini itachukua mkondo wake.”
 
Dada uliepigwa chupa husikubali,pambana haki itendeke hao masuper star wa kuunga unga wanataka kujifanya nchi yao,husikubali komaaa aende jela liwe fundisho kwa wengine wenye akili mbovu kama zake
 
Ajidanganye ampige mywife wangu (kwa sauti ya kihaya)
Nitamfunga
 
Mshedede tu. Labda huyo jamaa atakuwa mlemavu yaani zaidi ya inch 7
 
Hapo kwenye nyekundu hapo!!.. Kwa nini? Ikiwa sio inch 7 hawaigombanii??
Kwa sababu engine nyingi tayari zinaitaji overhaul. Mashine zimetumika na ni kama zimekufa
 
Warembo wetu: Physical Beauty + Monster Brain + Ignorance = 0
 
Huyu Jackline si mke wa mtu huyu...s kaolewa huyu?!Au alishapigwa chini?!Mmmh,kwa experience nliyonayo juu ya wake za watu, huwa wana hekima na busara nyingi, sasa huyu hayo matope kchwan kayatoa wapi? Hafsa, hilo kovu la usoni ndo lako tena, hakikisha na wewe unampeleka jela .... shuwain!
 
Aiseeeee babayangu kweli uume unambo mpaka mnatowana ngeu kisa uume
 
wanaume tukioa tusiangalia sura na umaarufu,ona mme wake na jacq yuko jela,na ona anachokifanya jacq,
 
Hasira hasara jela hiyoo inamkaribisha
 
Back
Top Bottom