Jaji atumia ubaya ubwela ya simba ugomvi wa ndugu wanaogombea jina

Jaji atumia ubaya ubwela ya simba ugomvi wa ndugu wanaogombea jina

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Snapinsta.app_457183660_483035314516931_2923226577291541096_n_1080.jpg

Jaji Frank Mahimbali wa Mahakama Kuu kanda ya Sumbawanga, ametumia msemo wa sasa wa mashabiki wa timu ya Simba wa ‘Ubaya Ubwela’ kufananisha sakata la watoto wawili wa familia moja wanaogombea jina la Kura.

Jaji alisema usemi huo unaomaanisha ‘ubaya umerudi tena’, kwa mtazamo wa kwanza, mtu anaweza asithamini suala la uhalifu linalowahusisha wawili hao, wakiwa ndugu, kiasi cha kukabana koo kwa matumizi ya majina hayo.

Hata hivyo, akitoa hukumu iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) dhidi ya Kasanda Mayuma au Machimu, Jaji alikubaliana na sababu za rufaa hiyo na kueleza kuwa kwa ushahidi uliopo,Kasanda ana hatia ya makosa manne ya jinai.

Kulingana na hukumu hiyo aliyoitoa Agosti 26,2024, Jaji Mahimbali ameyataja makosa hayo kuwa ni kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi wa umma, kula kiapo cha uongo, kujifanya ni Kura na kujipatia usajili wa ardhi kwa njia ya udanganyifu.


 
Back
Top Bottom