Jaji kiongozi Fakh Jundu amjibu Lissu kuhusu tuhuma zilizotolewa dhidi ya Mahakama Bungeni

mkuu henge ndo umeshuka leo kutoka sayari ya mars nini? jaji wa mahakama ya rufaa ya tz aitwaye mbarouk salim mbarouk fr6 zenji kumbe ana diploma ya law ya ud na bachelor of arts. sasa hivi ndo anaitafuta LLB pale pa professor mbwete(open university)

mkuu kunahabari zingine sijui hata huwa zinanipitaje,
Imenisikitisha sana mkuu!
 
kwa hili sijaona hoja ya lissu kujibiwa....halafu kwa nini mtu aongezewe wakati tuna wasomi wengi wanazurula na vyeti mtaan......MTU AKISTAAFU AKAPUMZIKE JAMANI SIO KUSHIKILIA TU NA HUU UONGOZI WA NCHI HIIHABARI ZA KUPEANA VYEO KWA URAFIKI KAMA ANAOFANYA BABA MWANAASHA HATUWEZI KUFIKA NA NDIO MAANA NCHI INAYUMBA JAMANI
 
HANA JIPYA, HANA SIFA. SIJUI ni mwanasheria gani huyu? Aaaaaaaa nimekumbuka, siyo mwanasheria ndiyo maana analopoka. ETI HAKUJITETEA? MBONA hata mahakamani watu huwa utetezi wao unatupiliwa mbali, kwa hiyo wanakuwa hawajajitetea. BUNGE ni mahali pa siasa, pa kuzungungumzia, neno parliament limetokana na neno parlour yaani sebule mahali pa kuzungumza, siyo mahakamani ambapo ni mahali pa kutolea ushahidi ambao unaweza kupokelewa au kutupiliwa mbali: JUNDU hajui anachokisema, anajundua tu.

UBAYA wa CCM wanaamini kuwa RAIS ni MUNGU NA WATEULE WAKE, KAMA HAWA MAJAJI FEKI NI WANA WA MUNGU, HAWAKOSEI. Wapi na wapi, hakuna kitu kama hicho. WANAMSHAMBULIA LISSU bure, ye2 anatafiti wao wanalopoka tu ... JIREKEBISHENI
 
Kwa hiyo, mtu asiye na degree ya Sheria kapewa uajaji wa mahakama ya rufaa yenye uweze kutoa hukumu ya kifo kwa mtu ye yote na mtu mzima na degree yake kichwani anakaa JF anamtetea Kikwete siku nzima.


ukisema ujaji wa rufaa, hapa unaongelea nafasi ambayo bado ni kubwa mno, kwani kesi zote toka mahakama kuu zikikatiwa rufaa hupelekwa huko. na rufaa ikitupwa basi ndio ujue mtu hana bahati tena.....mahakama ya rufaa sio ndogo kama inavyodhaniwa.
 
Du! Huyu Lissu ni BONGE LA TUNDU. Pengine yafaa aitwe LITUNDU kwani tundu lake si lakawaida. Anamfanya Jaji mzima aweweseke na asijue chakujibu? Tundu kweli kiboko ya sheria Tanzania. Sidhani kama huyu jaji alijua alichokua akiongea kwani hajajibu hoja hata moja. In fact, amempandisha chati Tundu Lissu. Du! I admire Lissu jamani
 
Huyu jaji bwana kama angeongezewa mkataba angeongezewa kama jaji wa kawaida na siyo kuteuliwa katika wadhifa mkubwa wa jaji kiongozi. Kama Kikwete hakumwona anafaa kushika wadhifa mkubwa yungali ndani ya umri (miaka 60) iweje sasa ateuliwe akiwa na miaka 63 kama siyo kumwandalia marupurupu tu? Huyu Jaji hajajibu kabisa hoja za mh. Lissu akajipange upya na huyo aliyembeba.
 

Kama sikosei mwananchi yoyote anaweza kuwa summoned na kamati ya Bunge au kulalamika kuhusu yaliyosemwa ndani ya Bunge dhidi yake, je majaji wamekuwa-excluded?
 
Nimekumbuka mfano ni Kesi ya Bwana Mengi na Adam Malima ambayo ilishughulikiwa na Bunge, sasa yeye ni kitu gani kimemzuia?! Au ndio umbumbumbu?
 

Wanasheria wengi na mawakili wengi wamejazana ktk law firms hapa nchini wakilipwa mishahara kiduchu kwa sababu hamna kazi. Wengine anastaafu halafu anapewa kazi kisa uzoefu. Je, hawa wengine watapataje uzoefu?
Katiba mpya ni muhimu sana kuweka mambo mengi sawa.
 
Mimi nadhani Kikwete anajua anachokifanya. Ana ajenda ambayo madhara yake tutakuja kuyaona miaka mingi ijayo.
Ukishashusha hadhi ya mahakama kuu kwa kuweka watu ambao sio qualified kuwa mahakimu wa rufaa ni kwamba umeshaondoa nguvu za mhimili wa pili wa mamlaka katika dola. Kwenye usalama wa taifa hali ni hiyo hiyo.Dr. Slaa hakukosea aliposema kuwa Kikwete ni janga la taifa.
 
Duu!!!!!!
Ni bora umuite Jundu, lile la kwanza linasikika vibaya kwa kidhungu, naamini wewe ndiye.

Hawa huwa wanakuja kupotosha mjadala ukishamjibu ndo lengo lake limetimia. Mpotezee. Maana anatutoa kwenye hoja ya Aweda ya majaji feki
 

Mwenye kumbukumbu sahihi ma akili timamu atajua nini kinaendelea na. hasa ikizingatiwa kuwa kesi ya kibaragashia ilitokea lini. Just time will tell.
 
Aweda kwa kuleta habari zenye mrengo wa Chama chako uko juu. Lakini jitahidi kubalance mambo.
 

Hapo kwenye red; nina uhakika 100% mkuu wa ule mhimili yuko kwenye usingizi wa pono kuhusu hiyo kitu. Teh teh teh teh! Burdani kweli kweli.
 
Huyu jaji kiongozi Fakhi Jundu nakumbuka uteuzi wake ulizua malumbano sana hapa JF back in a days. Hatimaye TL ametusaidia kukata mzizi wa fitna. Na katika kudhihirisha jinsi alivyo dhaifu kama walivyodai watumishi wa mahakama, majibu yake juu ya sakata hili yanamuelezea kinagaubaga.
 
[h=2][/h] Ijumaa, Agosti 31, 2012 06:30 Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam

*Ashangazwa na tuhuma zinazoelekezwa kwake
*Asema viongozi wa aina hiyo ni hatari mno
JAJI Kiongozi, Fakhi Jundu amesema mjadala wa uteuzi wa majaji uliotokea hivi karibu ni dalili mbaya, inayoonyesha kuna watu fulani kama wakipewa nafasi ya kuongoza nchi, watawaangamiza wengine.

Licha ya kutotaja jina la kiongozi yeyote, kauli ya Jaji Jundu imekuja kufuatia Mbunge wa Singida Mashariki, ambaye ni Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Waziri Kivuli wa Wizara ya Katiba na Sheria, Lissu kutoa ushahidi mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kuthibitisha alichokisema bungeni Julai 13, mwaka huu kuhusu uteuzi wa majaji na sifa zao.

Jaji Jundu alisema hayo jana, alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari ofisini kwake, kuhusu tuhuma zilizotolewa kwake, kuwa wadhifa wake aliupata kinyemela.

“Nawatoa hofu wananchi, aliyekuwa kitini wakati nateuliwa ni Jaji Augustino Ramadhani, ambaye anaheshimika sana, amesifiwa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), atawezaje kupitisha mkataba wa aina hiyo.

“Hoja kama hizi, zinapotolewa bungeni, hatuna namna ya kujitetea, tumenyamaza kimya kwa sababu habari za bungeni tutamjibu nani, wataendelea kuchafua majina yetu, lakini wenye akili watajua.

“Hatutaki majibizano yasiyo na faida, sijui yalizungumzwa hayo kwa kumlenga Rais au majaji, Bunge halina ubavu wa kujadili mahakama wala majaji kwa majina, kwa sababu hatuna nafasi ya kujitetea,” alisema Jaji Jundu.

Alisema hiyo, ni dalili mbaya inayoonyesha kuna watu fulani kama wakifanikiwa kutawala nchi hii, watawakandamiza wengine bila kuwapa nafasi ya kujitetea.

Alisema jaji anapostaafu, Rais akimuona anafaa kwa manufaa ya taifa, basi humuomba kushika wadhifa mwingine.

“Rais ana watu wake na wanasheria wanaohusika katika uteuzi, haiingii akilini watu wote hao wanyamazie makosa,” alisema.

Alisema kama upo mkataba wake aliopata kinyemela, yupo tayari kuona unachapishwa kwenye magazeti.

Alisema anatuhumiwa kuwa na ubia na Jaji, Kassimu Nyangarika jambo ambalo halina ukweli wowote.

Hivi karibuni Mbunge wa Singida Mashariki ambaye ni Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Waziri Kivuli wa Wizara ya Katiba na Sheria, Lissu alitoa ushahidi mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kuthibitisha alichokisema bungeni Julai 13, mwaka huu kuhusu uteuzi wa majaji na sifa zao.

Akizungumzia ajira ya Jaji Jundu, alisema iko katika kundi la watu wasiokuwa majaji kwa mujibu wa Katiba.

Alisema Julai 29, 2009, Jaji Jundu wakati huo akiwa Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Iringa, alitoa taarifa ya kustaafu kwa mujibu wa sheria.

Hata hivyo, mara baada ya kutoa taarifa hiyo, Jaji Jundu si tu alipewa mkataba wa ujaji kwa miaka mitatu, bali pia alipandishwa cheo na kuwa Jaji Kiongozi.

Alisema inasemekana sasa, Jaji Kiongozi Jundu ameongezewa mkataba mwingine tena wa miaka miwili, ili aendelee kushika wadhifa huo, hadi Julai 29, 2012.

Kabla ya kujibu tuhuma hizo, Jaji Jundu alimwapisha John Kayoza kuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu. Kayoza kabla ya uteuzi huo, alikuwa Msajili wa Mahakama ya Rufaa.

“Dhamira ya kufanya uteuzi wa wasajili ni kuwapa muda wa kutosha kushughulikia mambo ya mahakama tofauti na zamani, ambapo wasajili walikuwa wakifanya kazi za utawala na mahakama,” alisema.

Alisema Serikali iliahidi kutenga Sh bilioni 20, kwa ajili ya mahakama lakini kiasi kilichowekwa ni Sh bilioni 14.5 kwa mazingira hayo kuweka asilimia ni ngumu.


[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]

[h=3][/h]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…